< 2 Wakorintho 1 >

1 Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
PAULOS, apostle of Jeshu Meshiha, by the will of Aloha; and Timotheos a brother: to the church of Aloha which is in Kurinthos, and to all the saints who are in all Akaia.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace be with you and peace, from Aloha our Father, and from our Lord Jeshu Meshiha.
3 Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
Blessed be Aloha, the Father of our Lord Jeshu Meshiha, the Father of mercies, and the God of all consolation, who consoleth us in all our afflictions,
4 Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
that we may be able to console those who are in all afflictions by that consolation by which we are consoled of Aloha.
5 Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.
For as the sufferings of the Meshiha abound in us, so, through the Meshiha, our consolation aboundeth also.
6 Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata.
But if we are afflicted, it is for your consolation and for your salvation that we be afflicted: and if we are consoled, it is that you may be consoled, that there may be in you perseverance to endure those sufferings which we also suffer.
7 Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.
And our hope concerning you is steadfast: for we know that if you participate in the sufferings, you also participate in the consolation.
8 Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi.
FOR I would have you to know, my brethren, of the affliction that befell us in Asia: for we were greatly pressed beyond our strength, until our life was nigh to be dissolved,
9 Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu.
and because of these we had concluded (for) death; that we should not have hope in ourselves, but in Aloha, who raiseth the dead:
10 Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
who from deaths of violence delivered us, and who will again, we trust, deliver us,
11 Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.
through the help of your prayers for us; that his gift towards us may be a benefit effected for many, and many may praise him on our behalf.
12 Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu.
For our glorying is this, the testimony of our conscience, that in simplicity and purity, and by the grace of Aloha, we are conversant in the world; and not with the wisdom of the flesh, and especially with you yourselves.
13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba,
For we write no other (things) to you than those which you know and acknowledge, and which I am confident you will acknowledge unto the end:
14 kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.
even as you have in part acknowledged that we are your glorying, as you also are ours in the day of our Lord Jeshu Meshiha.
15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili.
And in this confidence I have willed from the first to come to you, that doubly you may receive benefit,
16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi.
and that I may pass by you to Makedunia, and again from Makedunia I may come to you, and you may lead me forth unto Jihud.
17 Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?
This then that I have purposed, have I purposed boastingly? or are they things of the flesh that I purpose, that I should have in them Yes, yes, or No, no?
18 Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.”
Faithful is Aloha that our word with you was not Yes and No.
19 Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.”
For the Son of Aloha, Jeshu Meshiha, who by us hath been preached unto you, by me and by Sylvanas and by Timotheos, was not Yes and No, but it was Yes in him.
20 Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu.
For all the promises of Aloha in him, in the Meshiha, are Yes; for which by him we give Amen to the glory of Aloha.
21 Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta
But Aloha himself confirmeth us with you in the Meshiha, who himself hath anointed us,
22 kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.
and hath sealed us, and given us the earnest-pledge of his Spirit in our hearts.
23 Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho.
BUT I testify to Aloha on my soul that because I am sparing of you, I have not come to Kurinthos.
24 Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.
Not because we are lords of your faith, but are helpers of your joy; for by faith you stand.

< 2 Wakorintho 1 >