< 2 Wakorintho 9 >

1 Hakuna haja yangu kuwaandikia kuhusu huduma hii itolewayo kwa ajili ya watakatifu.
Car de vous écrire touchant la collecte qui se fait pour les Saints, ce me serait une chose superflue.
2 Kwa kuwa ninajua mlivyo na shauku ya kusaidia, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili ya jambo hilo kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana na shauku yenu imewachochea wengi wao katika kutoa.
Vu que je sais la promptitude de votre zèle, en quoi je me glorifie de vous devant ceux de Macédoine, [leur faisant entendre] que l'Achaïe est prête dès l'année passée; et votre zèle en a excité plusieurs.
3 Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusiwe maneno matupu, bali mpate kuwa tayari kama nilivyosema mngekuwa tayari.
Or j'ai envoyé ces frères, afin que ce en quoi je me suis glorifié de vous, ne soit pas vain en cette occasion, et que vous soyez prêts, comme j'ai dit.
4 Kwa maana kama nikija na Mmakedonia yeyote na kuwakuta hamjawa tayari, tutaona aibu kusema chochote juu yenu katika matoleo.
De peur que ceux de Macédoine venant avec moi, et ne vous trouvant pas prêts, nous n'ayons de la honte, (pour ne pas dire vous-mêmes) de l'assurance avec laquelle nous nous sommes glorifiés de vous.
5 Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kwenu kabla yangu, wafanye mipango ya hayo matoleo ya ukarimu mliyokuwa mmeahidi, ili yawe tayari kama matoleo ya hiari wala si kama ya kutozwa kwa nguvu.
C'est pourquoi j'ai estimé qu'il était nécessaire de prier les frères d'aller premièrement vers vous, et d'achever de préparer votre bénéficence que vous avez déjà promise; afin qu'elle soit prête comme une bénéficence, et non pas comme une chicheté.
6 Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye kwa uchache pia atavuna kwa uchache, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.
Or je vous dis ceci: que celui qui sème chichement, recueillera aussi chichement; et que celui qui sème libéralement, recueillera aussi libéralement.
7 Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa uchoyo au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo mkunjufu.
[Mais] que chacun [contribue] selon qu'il se l'est proposé en son cœur, non point à regret, ou par contrainte; car Dieu aime celui qui donne gaiement.
8 Naye Mungu aweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili katika mambo yote kila wakati, mwe na kila kitu mnachohitaji, ili mweze kushiriki kwa wingi katika kila kazi njema.
Et Dieu est puissant pour faire abonder toute grâce en vous, afin qu'ayant toujours tout ce qui suffit en toute chose, vous soyez abondants en toute bonne œuvre:
9 Kama ilivyoandikwa: “Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele.” (aiōn g165)
Selon ce qui est écrit: il a répandu, il a donné aux pauvres; sa justice demeure éternellement. (aiōn g165)
10 Yeye ampaye mpanzi mbegu kwa ajili ya kupanda na mkate kuwa chakula, atawapa na kuzizidisha mbegu zenu za kupanda na kuongeza mavuno ya haki yenu.
Or celui qui fournit de la semence au semeur, veuille aussi vous donner du pain à manger, et multiplier votre semence, et augmenter les revenus de votre justice.
11 Mtatajirishwa kwa kila namna ili mpate kuwa wakarimu kila wakati, na kupitia kwetu, ukarimu wenu utamletea Mungu shukrani.
Etant pleinement enrichis pour [exercer] une parfaite libéralité, laquelle fait que nous en rendons grâces à Dieu.
12 Huduma hii mnayofanya si tu kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watakatifu, bali huzidi sana kwa shukrani nyingi apewazo Mungu.
Car l'administration de cette oblation n'est pas seulement suffisante pour subvenir aux nécessités des Saints, mais elle abonde aussi de telle sorte, que plusieurs ont de quoi en rendre grâces à Dieu.
13 Kwa sababu ya huduma ambayo mmejithibitisha wenyewe, watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utiifu ufuatanao na ukiri wenu wa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wenu wa kushiriki pamoja nao na pia wengine wote.
Glorifiant Dieu pour l'épreuve qu'ils font de cette assistance, en ce que vous vous soumettez à l'Évangile de Christ; et de votre prompte et libérale communication envers eux, et envers tous.
14 Nao katika maombi yao kwenu mioyo yao itawaonea shauku kwa sababu ya neema ipitayo kiasi mliyopewa na Mungu.
Ils prient Dieu pour vous, et ils vous aiment très affectueusement à cause de la grâce excellente que Dieu vous a accordée.
15 Ashukuriwe Mungu kwa karama yake isiyoelezeka.
Or grâces soient rendues à Dieu à cause de son don inexprimable.

< 2 Wakorintho 9 >