< 2 Wakorintho 9 >
1 Hakuna haja yangu kuwaandikia kuhusu huduma hii itolewayo kwa ajili ya watakatifu.
Now concerning the relief intended for the saints, it is superfluous for me to write to you:
2 Kwa kuwa ninajua mlivyo na shauku ya kusaidia, nami nimekuwa nikijivuna kwa ajili ya jambo hilo kwa watu wa Makedonia, nikiwaambia kuwa ninyi wa Akaya mmekuwa tayari kutoa tangu mwaka jana na shauku yenu imewachochea wengi wao katika kutoa.
for I know your readiness of mind, which I boast of concerning you to the Macedonians, that Achaia was ready a year ago; and your zeal hath excited many.
3 Lakini sasa nawatuma hawa ndugu ili kujivuna kwetu kuhusu mchango wenu kusiwe maneno matupu, bali mpate kuwa tayari kama nilivyosema mngekuwa tayari.
But I have sent the brethren, that our boasting of you might not become vain in this respect, but that ye might be ready, as I had said:
4 Kwa maana kama nikija na Mmakedonia yeyote na kuwakuta hamjawa tayari, tutaona aibu kusema chochote juu yenu katika matoleo.
least if the Macedonians should come with me, and find you unprepared, we should be ashamed (not to say you also) in this confident boasting.
5 Kwa hivyo niliona ni muhimu niwahimize hawa ndugu watangulie kuja huko kwenu kabla yangu, wafanye mipango ya hayo matoleo ya ukarimu mliyokuwa mmeahidi, ili yawe tayari kama matoleo ya hiari wala si kama ya kutozwa kwa nguvu.
Therefore I thought it necessary to exhort the brethren to go first to you, and before our coming to collect your bounty beforementioned, that it may be ready, as of munificence, and not of force.
6 Kumbukeni kwamba: Yeyote apandaye kwa uchache pia atavuna kwa uchache, naye apandaye kwa ukarimu pia atavuna kwa ukarimu.
But this I say, He that soweth sparingly shall reap also sparingly; and he that soweth bountifully shall also reap bountifully.
7 Kila mtu atoe kama anavyokusudia moyoni mwake, si kwa uchoyo au kwa kulazimishwa, kwa maana Mungu humpenda yeye atoaye kwa moyo mkunjufu.
Let every one give as he chuses in his own heart; not with reluctance, or constraint: for God loveth a chearful giver.
8 Naye Mungu aweza kuwapa kila baraka kwa wingi, ili katika mambo yote kila wakati, mwe na kila kitu mnachohitaji, ili mweze kushiriki kwa wingi katika kila kazi njema.
And God is able to make all grace abound towards you; that having always all sufficiency in every thing, ye may abound in every good work:
9 Kama ilivyoandikwa: “Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele.” (aiōn )
(as it is written, "He hath dispersed, he hath given to the poor, his righteousness continueth for ever." (aiōn )
10 Yeye ampaye mpanzi mbegu kwa ajili ya kupanda na mkate kuwa chakula, atawapa na kuzizidisha mbegu zenu za kupanda na kuongeza mavuno ya haki yenu.
And may He, who supplieth seed to the sower, and giveth bread for food, furnish and multiply your sowing, and increase the fruits of your bounty: )
11 Mtatajirishwa kwa kila namna ili mpate kuwa wakarimu kila wakati, na kupitia kwetu, ukarimu wenu utamletea Mungu shukrani.
being in every thing enriched to all liberality, which produceth through us thanksgiving to God.
12 Huduma hii mnayofanya si tu kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya watakatifu, bali huzidi sana kwa shukrani nyingi apewazo Mungu.
For the ministration of this service not only supplieth the wants of the saints, but aboundeth also, through many thanksgivings, to the glory of God.
13 Kwa sababu ya huduma ambayo mmejithibitisha wenyewe, watu watamtukuza Mungu kwa ajili ya utiifu ufuatanao na ukiri wenu wa Injili ya Kristo, na kwa ukarimu wenu wa kushiriki pamoja nao na pia wengine wote.
(While from the experience of this ministration they glorify God for your professed subjection to the gospel of Christ, and the liberality of your communication to them, and to all men.)
14 Nao katika maombi yao kwenu mioyo yao itawaonea shauku kwa sababu ya neema ipitayo kiasi mliyopewa na Mungu.
And in their prayer for you, who long after you because of the transcendent grace of God towards you.
15 Ashukuriwe Mungu kwa karama yake isiyoelezeka.
Thanks be to God for his inexpressible gift!