< 2 Wakorintho 8 >

1 Basi sasa ndugu, nataka ninyi mjue kuhusu ile neema ambayo Mungu amewapa makanisa ya Makedonia.
De plus, frères, nous vous faisons connaître la grâce de Dieu qui a été accordée dans les assemblées de Macédoine,
2 Pamoja na majaribu makali na taabu walizopata, furaha waliyokuwa nayo ilikuwa kubwa, ingawa walikuwa maskini kupindukia, kwa upande wao walifurika kwa wingi wa ukarimu.
comment, dans une dure épreuve de détresse, l'abondance de leur joie et leur profonde pauvreté ont abondé jusqu'à la richesse de leur générosité.
3 Kwa maana nashuhudia kwamba wao walitoa kwa kadiri wawezavyo, hata na zaidi ya uwezo wao, kwa hiari yao wenyewe,
Car, selon leur pouvoir, je l'atteste, oui et au-delà de leur pouvoir, ils ont donné de leur propre chef,
4 wakitusihi kwa bidii wapewe fursa ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watakatifu.
nous suppliant avec beaucoup d'insistance de recevoir cette grâce et la communion dans le service des saints.
5 Wala hawakufanya tulivyotazamia, bali walijitoa wao wenyewe kwa Bwana kwanza na ndipo wakajitoa kwa ajili yetu, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
Cela ne s'est pas passé comme nous l'avions prévu, mais ils se sont d'abord donnés au Seigneur et à nous par la volonté de Dieu.
6 Kwa hiyo tulimsihi Tito, kwa kuwa ndiye alianzisha jambo hili, akamilishe tendo hili la neema kwa upande wenu.
Nous avons donc exhorté Tite à achever en vous cette grâce, comme il l'avait commencée auparavant.
7 Lakini kama vile mlivyo mbele sana katika yote: Katika imani, katika usemi, katika maarifa, katika uaminifu wote na katika upendo wenu kwetu sisi, vivyo hivyo tunataka pia mzidi katika neema hii ya kutoa.
Or, comme vous abondez en toutes choses, dans la foi, dans la parole, dans la connaissance, dans tout ce qui est sérieux, et dans votre amour pour nous, faites en sorte que vous abondiez aussi dans cette grâce.
8 Siwaamrishi, lakini nataka kujaribu unyofu wa upendo wenu kwa kuulinganisha na bidii ya wengine.
Je ne parle pas comme un commandement, mais comme une preuve, par le sérieux des autres, de la sincérité de votre amour.
9 Kwa maana mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo, kwamba ingawa alikuwa tajiri, kwa ajili yenu alikubali kuwa maskini, ili kwa umaskini wake ninyi mpate kuwa matajiri.
Car vous connaissez la grâce de notre Seigneur Jésus-Christ, qui, bien que riche, s'est fait pauvre à cause de vous, afin que vous deveniez riches par sa pauvreté.
10 Ushauri wangu kuhusu lile lililo bora kwenu juu ya jambo hili ni huu: Mwaka uliopita ninyi mlikuwa wa kwanza si tu kutoa lakini pia mlikuwa na shauku ya kufanya hivyo.
Voici le conseil que je vous donne: il est opportun que vous, qui avez commencé les premiers il y a un an, non seulement fassiez, mais encore ayez la volonté.
11 Sasa ikamilisheni kazi hii kwa shauku kama mlivyoanza, jitoleeni kulingana na uwezo wenu.
Mais maintenant, achevez aussi de faire, afin que, comme il y a eu la volonté de faire, il y ait aussi l'achèvement selon votre capacité.
12 Kwa kuwa kama nia ya kutoa ipo, kitolewacho kinakubalika kulingana na kile mtu alicho nacho, wala si kwa kile ambacho hana.
En effet, si l'empressement est là, c'est en fonction de ce que vous avez, et non en fonction de ce que vous n'avez pas.
13 Nia yetu si kwamba wengine wasaidike wakati ninyi mnateseka, bali pawe na uwiano.
Ce n'est pas, en effet, pour que les autres soient soulagés et vous affligés,
14 Kwa wakati huu, wingi wa vitu mlivyo navyo usaidie kutosheleza mahitaji yao, ili wakati wao watakapokuwa na wingi wa vitu, nao wapate kutosheleza mahitaji yenu.
mais pour qu'il y ait égalité. En effet, l'abondance dont vous disposez en ce moment comble leur manque, afin que leur abondance comble aussi votre manque, et qu'il y ait égalité.
15 Ndipo patakuwa na usawa, kama ilivyoandikwa: “Aliyekusanya zaidi hakuwa na ziada, wala aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”
Selon qu'il est écrit: « Celui qui amassait beaucoup ne manquait de rien, et celui qui amassait peu ne manquait de rien. »
16 Ninamshukuru Mungu ambaye amemtia Tito moyo wa kuwajali ninyi kama mimi ninavyowajali.
Mais grâces soient rendues à Dieu, qui met dans le cœur de Tite le même zèle pour vous.
17 Si kwamba Tito amekubali tu ombi letu, bali anakuja kwenu akiwa na shauku kuliko wakati mwingine, tena kwa hiari yake mwenyewe.
En effet, il a bien accueilli notre exhortation, mais étant lui-même très sérieux, il est allé vers vous de son propre chef.
18 Nasi tunamtuma pamoja naye ndugu ambaye anasifiwa na makanisa yote kwa huduma yake ya kuhubiri Injili.
Nous avons envoyé avec lui le frère dont la louange de la Bonne Nouvelle est connue dans toutes les assemblées.
19 Zaidi ya hayo, alichaguliwa na makanisa ili asafiri pamoja nasi tulipokuwa tunapeleka matoleo ya ukarimu, kwa ajili ya utukufu wa Bwana mwenyewe, na ili kuonyesha hisani yetu kuwasaidia.
Non seulement cela, mais il a aussi été désigné par les assemblées pour voyager avec nous dans cette grâce, qui est servie par nous à la gloire du Seigneur lui-même, et pour montrer notre empressement.
20 Tunataka kuepuka lawama yoyote kuhusu jinsi tunavyosimamia matoleo haya ya ukarimu.
Nous évitons cela, afin que personne ne nous blâme au sujet de cette abondance qui est administrée par nous.
21 Kwa kuwa tunakusudia kufanya kile kilicho haki si machoni mwa Bwana peke yake, bali pia machoni mwa watu wengine.
Ayant égard aux choses honorables, non seulement aux yeux du Seigneur, mais aussi aux yeux des hommes.
22 Pamoja nao, tunamtuma ndugu yetu ambaye mara kwa mara ametuthibitishia kwa njia nyingi kwamba ana shauku, naam, zaidi sana sasa kwa sababu analo tumaini kuu kwenu.
Nous avons envoyé avec eux notre frère, dont nous avons souvent prouvé le sérieux en bien des choses, mais qui l'est encore plus maintenant, à cause de la grande confiance qu'il a en vous.
23 Kwa habari ya Tito, yeye ni mwenzangu na mtendakazi pamoja nami miongoni mwenu. Kwa habari za ndugu zetu, wao ni wawakilishi wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
Quant à Tite, il est mon associé et mon compagnon de travail pour vous. Quant à nos frères, ils sont les apôtres des assemblées, la gloire de Christ.
24 Kwa hiyo waonyesheni wazi hawa ndugu uthibitisho wa upendo wenu na sababu inayotufanya tujivune kwa ajili yenu, mbele ya makanisa, ili yapate kuona.
Témoigne donc de ton amour pour eux devant les assemblées, et de notre vantardise en ta faveur.

< 2 Wakorintho 8 >