< 2 Wakorintho 6 >

1 Kama watendakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure.
Mi vas potem kot delavci skupaj z njim tudi rotimo, da Božje milosti niste prejeli zaman.
2 Kwa maana asema: “Wakati wangu uliokubalika nilikusikia, siku ya wokovu nilikusaidia.” Tazama, wakati uliokubalika ndio huu, siku ya wokovu ndiyo sasa.
(Kajti pravi: »Uslišal sem te v sprejemljivem času in na dan rešitve duše sem ti pomagal; glej, sedaj je odobren čas; glej, sedaj je dan rešitve duše.«)
3 Hatuweki kitu cha kukwaza katika njia ya mtu yeyote, ili huduma yetu isionekane kuwa na lawama.
Ne dajemo nobene spotike v nobeni stvari, da služba ne bo ošteta.
4 Bali kama watumishi wa Mungu tuonyeshe kwa kila njia: katika saburi nyingi; katika dhiki, katika misiba, na katika shida;
Toda v vseh stvareh se priporočamo kakor Božji služabniki, v veliki potrpežljivosti, v stiskah, v potrebah, v tegobah,
5 katika kupigwa, katika kufungwa gerezani na katika ghasia; katika kazi ngumu, katika kukesha na katika kufunga;
v bičanjih, v ječah, pri uporih, v naporih, v bedenjih, v postih,
6 katika utakatifu, katika ufahamu, katika uvumilivu, na katika utu wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli;
s čistostjo, s spoznanjem, s potrpežljivostjo, s prijaznostjo, s Svetim Duhom, z nehlinjeno ljubeznijo,
7 katika maneno ya kweli na katika nguvu za Mungu, kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;
z besedo resnice, z Božjo močjo, z bojno opremo pravičnosti na desni roki in na levi,
8 katika utukufu na katika kudharauliwa; katika sifa mbaya na katika sifa nzuri; tukiwa kama wadanganyaji, lakini tukiwa wakweli;
s spoštovanjem in nespoštovanjem, na slabem in dobrem glasu; kakor sleparji, pa vendar iskreni;
9 tukiwa maarufu, lakini tukihesabiwa kama tusiojulikana; tukiwa kama wanaokufa, lakini tunaishi; tukipigwa, lakini hatuuawi;
kakor neznani, pa vendar dobro znani; kakor umirajoči in glej, živimo; kakor kaznovani, pa ne ubiti;
10 tukiwa kama wenye huzuni, lakini siku zote tukifurahi; tukionekana maskini, lakini tukitajirisha wengi; tukiwa kama wasio na kitu, lakini tuna vitu vyote.
kakor žalostni, vendar vedno veseli; kakor ubogi, vendar mnoge bogatimo; kakor ne bi imeli nič, pa vendar posedujemo vse stvari.
11 Tumesema nanyi wazi, enyi Wakorintho na kuwafungulieni mioyo yetu wazi kabisa.
Oh vi Korinčani, naša usta so vam odprta, naše srce je širokosrčno.
12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu kwetu.
Vi niste omejeni v nas, temveč ste omejeni v svojih lastnih notranjostih.
13 Sasa nasema, kama na watoto wangu: Ninyi pia ifungueni mioyo yenu kabisa.
Torej za povračilo v enakem (govorim vam kakor svojim otrokom), bodite tudi vi širokosrčni.
14 Msifungiwe nira pamoja na watu wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa, kwa maana pana uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
Ne bodite neenako vpreženi skupaj z neverniki, kajti kakšno družbo ima pravičnost z nepravičnostjo? Ali kakšno udeležbo ima svetloba s temo?
15 Kuna mapatano gani kati ya Kristo na Beliari? Yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?
In kakšno soglasje ima Kristus z Beliálom? Ali kakšen delež ima, kdor veruje, z neverniki?
16 Kuna mapatano gani kati ya Hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi tu Hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema: “Nitakaa pamoja nao na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
In kakšno strinjanje ima Božji tempelj z maliki? Kajti vi ste tempelj živega Boga; kakor je rekel Bog: »Prebival bom v njih in hodil v njih in jaz bom njihov Bog in oni bodo moji ljudje.
17 “Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, mkatengwe nao, asema Bwana. Msiguse kitu chochote kilicho najisi, nami nitawakaribisha.”
Zatorej pridite ven izmed njih in bodite oddvojeni, « govori Gospod »in nečiste stvari se ne dotikajte; in jaz vas bom sprejel
18 “Mimi nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”
in vam bom Oče in vi boste moji sinovi in hčere, « govori Gospod Vsemogočni.

< 2 Wakorintho 6 >