< 2 Wakorintho 6 >

1 Kama watendakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure.
Men som Medarbejdere formane vi ogsaa til, at I ikke forgæves maa have modtaget Guds Naade;
2 Kwa maana asema: “Wakati wangu uliokubalika nilikusikia, siku ya wokovu nilikusaidia.” Tazama, wakati uliokubalika ndio huu, siku ya wokovu ndiyo sasa.
(han siger jo: „Paa en behagelig Tid bønhørte jeg dig, og paa en Frelsens Dag hjalp jeg dig.” Se, nu er det en velbehagelig Tid, se, nu er det en Frelsens Dag; )
3 Hatuweki kitu cha kukwaza katika njia ya mtu yeyote, ili huduma yetu isionekane kuwa na lawama.
og vi give ikke i nogen Ting noget Anstød, for at Tjenesten ikke skal blive lastet;
4 Bali kama watumishi wa Mungu tuonyeshe kwa kila njia: katika saburi nyingi; katika dhiki, katika misiba, na katika shida;
men i alting anbefale vi som Guds Tjenere os selv ved stor Udholdenhed i Trængsler, i Nød, i Angester,
5 katika kupigwa, katika kufungwa gerezani na katika ghasia; katika kazi ngumu, katika kukesha na katika kufunga;
under Slag, i Fængsler, under Oprør, under Besværligheder, i Nattevaagen, i Faste,
6 katika utakatifu, katika ufahamu, katika uvumilivu, na katika utu wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli;
ved Renhed, ved Kundskab, ved Langmodighed, ved Velvillighed, ved den Helligaand, ved uskrømtet Kærlighed,
7 katika maneno ya kweli na katika nguvu za Mungu, kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;
ved Sandheds Ord, ved Guds Kraft, ved Retfærdighedens Vaaben baade til Angreb og Forsvar;
8 katika utukufu na katika kudharauliwa; katika sifa mbaya na katika sifa nzuri; tukiwa kama wadanganyaji, lakini tukiwa wakweli;
ved Ære og Vanære, ved ondt Rygte og godt Rygte; som Forførere og dog sanddrue;
9 tukiwa maarufu, lakini tukihesabiwa kama tusiojulikana; tukiwa kama wanaokufa, lakini tunaishi; tukipigwa, lakini hatuuawi;
som ukendte og dog velkendte; som døende, og se, vi leve; som de, der tugtes, dog ikke til Døde;
10 tukiwa kama wenye huzuni, lakini siku zote tukifurahi; tukionekana maskini, lakini tukitajirisha wengi; tukiwa kama wasio na kitu, lakini tuna vitu vyote.
som bedrøvede, dog altid glade; som fattige, der dog gøre mange rige; som de, der intet have, og dog eje alt.
11 Tumesema nanyi wazi, enyi Wakorintho na kuwafungulieni mioyo yetu wazi kabisa.
Vor Mund er opladt over for eder, Korinthiere! vort Hjerte er udvidet.
12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu kwetu.
I have ikke snæver Plads i os, men der er snæver Plads i eders Hjerter.
13 Sasa nasema, kama na watoto wangu: Ninyi pia ifungueni mioyo yenu kabisa.
Men ligesaa til Gengæld (jeg taler som til mine Børn), maa ogsaa I udvide eders Hjerter!
14 Msifungiwe nira pamoja na watu wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa, kwa maana pana uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
Drager ikke i ulige Aag med vantro; thi hvad Fællesskab har Retfærdighed og Lovløshed? eller hvad Samfund har Lys med Mørke?
15 Kuna mapatano gani kati ya Kristo na Beliari? Yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?
Hvad Samklang er der mellem Kristus og Belial? eller hvad Delagtighed har en troende med en vantro?
16 Kuna mapatano gani kati ya Hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi tu Hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema: “Nitakaa pamoja nao na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
Hvad Samstemning har Guds Tempel med Afguder? Thi vi ere den levende Guds Tempel, ligesom Gud har sagt: „Jeg vil bo og vandre iblandt dem, og jeg vil være deres Gud, og de skulle være mit Folk.”
17 “Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, mkatengwe nao, asema Bwana. Msiguse kitu chochote kilicho najisi, nami nitawakaribisha.”
„Derfor gaar ud fra dem og udskiller eder fra dem, siger Herren, og rører ikke noget urent; og jeg vil antage mig eder,”
18 “Mimi nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”
„og jeg vil være eders Fader, og I skulle være mine Sønner og Døtre, siger Herren, den Almægtige.”

< 2 Wakorintho 6 >