< 2 Wakorintho 6 >

1 Kama watendakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msipokee neema ya Mungu bure.
ܘܐܝܟ ܡܥܕܪܢܐ ܒܥܝܢܢ ܡܢܟܘܢ ܕܠܐ ܬܤܬܪܩ ܒܟܘܢ ܛܝܒܘܬܐ ܕܐܠܗܐ ܕܩܒܠܬܘܢ
2 Kwa maana asema: “Wakati wangu uliokubalika nilikusikia, siku ya wokovu nilikusaidia.” Tazama, wakati uliokubalika ndio huu, siku ya wokovu ndiyo sasa.
ܐܡܪ ܓܝܪ ܕܒܙܒܢܐ ܡܩܒܠܐ ܥܢܝܬܟ ܘܒܝܘܡܐ ܕܚܝܐ ܥܕܪܬܟ ܗܐ ܗܫܐ ܙܒܢܐ ܡܩܒܠܐ ܘܗܐ ܗܫܐ ܝܘܡܐ ܕܚܝܐ
3 Hatuweki kitu cha kukwaza katika njia ya mtu yeyote, ili huduma yetu isionekane kuwa na lawama.
ܠܡܐ ܒܡܕܡ ܬܬܠܘܢ ܠܐܢܫ ܥܠܬܐ ܕܬܘܩܠܬܐ ܕܠܐ ܢܗܘܐ ܡܘܡܐ ܒܬܫܡܫܬܢ
4 Bali kama watumishi wa Mungu tuonyeshe kwa kila njia: katika saburi nyingi; katika dhiki, katika misiba, na katika shida;
ܐܠܐ ܒܟܠ ܡܕܡ ܢܚܘܐ ܢܦܫܢ ܕܡܫܡܫܢܐ ܚܢܢ ܕܐܠܗܐ ܒܡܤܝܒܪܢܘܬܐ ܤܓܝܐܬܐ ܒܐܘܠܨܢܐ ܒܐܢܢܩܤ ܒܚܒܘܫܝܐ
5 katika kupigwa, katika kufungwa gerezani na katika ghasia; katika kazi ngumu, katika kukesha na katika kufunga;
ܒܢܓܕܐ ܒܐܤܘܪܐ ܒܫܓܘܫܝܐ ܒܠܐܘܬܐ ܒܫܗܪܐ ܒܨܘܡܐ
6 katika utakatifu, katika ufahamu, katika uvumilivu, na katika utu wema; katika Roho Mtakatifu na upendo wa kweli;
ܒܕܟܝܘܬܐ ܒܝܕܥܬܐ ܒܢܓܝܪܘܬ ܪܘܚܐ ܒܒܤܝܡܘܬܐ ܒܪܘܚܐ ܕܩܘܕܫܐ ܒܚܘܒܐ ܕܠܐ ܢܟܠܐ
7 katika maneno ya kweli na katika nguvu za Mungu, kwa silaha za haki za mkono wa kuume na za mkono wa kushoto;
ܒܡܠܬܐ ܕܩܘܫܬܐ ܒܚܝܠܐ ܕܐܠܗܐ ܒܙܝܢܐ ܕܙܕܝܩܘܬܐ ܕܒܝܡܝܢܐ ܘܒܤܡܠܐ
8 katika utukufu na katika kudharauliwa; katika sifa mbaya na katika sifa nzuri; tukiwa kama wadanganyaji, lakini tukiwa wakweli;
ܒܫܘܒܚܐ ܘܒܨܥܪܐ ܒܩܘܠܤܐ ܘܒܓܘܢܝܐ ܐܝܟ ܡܛܥܝܢܐ ܘܫܪܝܪܐ
9 tukiwa maarufu, lakini tukihesabiwa kama tusiojulikana; tukiwa kama wanaokufa, lakini tunaishi; tukipigwa, lakini hatuuawi;
ܐܝܟ ܠܐ ܝܕܝܥܐ ܘܝܕܝܥܝܢܢ ܐܝܟ ܡܝܬܝܢܢ ܘܗܐ ܚܝܝܢ ܚܢܢ ܐܝܟ ܕܡܬܪܕܝܢܢ ܘܠܐ ܡܝܬܝܢܢ
10 tukiwa kama wenye huzuni, lakini siku zote tukifurahi; tukionekana maskini, lakini tukitajirisha wengi; tukiwa kama wasio na kitu, lakini tuna vitu vyote.
ܐܝܟ ܕܟܪܝܐ ܠܢ ܘܒܟܠܙܒܢ ܚܕܝܢܢ ܐܝܟ ܡܤܟܢܐ ܘܠܤܓܝܐܐ ܡܥܬܪܝܢܢ ܐܝܟ ܕܡܕܡ ܠܝܬ ܠܢ ܘܟܠ ܡܕܡ ܐܚܝܕܝܢܢ
11 Tumesema nanyi wazi, enyi Wakorintho na kuwafungulieni mioyo yetu wazi kabisa.
ܦܘܡܢ ܦܬܝܚ ܗܘ ܠܘܬܟܘܢ ܩܘܪܢܬܝܐ ܘܠܒܢ ܪܘܝܚ
12 Sisi hatujizuii kuwapenda, bali ninyi mmeuzuia upendo wenu kwetu.
ܠܐ ܐܠܝܨܝܬܘܢ ܒܢ ܐܠܝܨܝܬܘܢ ܕܝܢ ܒܪܚܡܝܟܘܢ
13 Sasa nasema, kama na watoto wangu: Ninyi pia ifungueni mioyo yenu kabisa.
ܐܝܟ ܕܠܒܢܝܐ ܕܝܢ ܐܡܪ ܐܢܐ ܦܘܪܥܘܢܝ ܚܘܒܠܝ ܕܠܘܬܟܘܢ ܘܪܘܚܘ ܚܘܒܟܘܢ ܠܘܬܝ
14 Msifungiwe nira pamoja na watu wasioamini, kwa jinsi isivyo sawasawa, kwa maana pana uhusiano gani kati ya haki na uovu? Au kuna ushirika gani kati ya nuru na giza?
ܘܠܐ ܬܗܘܘܢ ܒܢܝ ܙܘܓܐ ܠܐܝܠܝܢ ܕܠܐ ܡܗܝܡܢܝܢ ܐܝܕܐ ܓܝܪ ܫܘܬܦܘܬܐ ܐܝܬ ܠܙܕܝܩܘܬܐ ܥܡ ܥܘܠܐ ܐܘ ܐܝܢܐ ܚܘܠܛܢܐ ܐܝܬ ܠܢܗܝܪܐ ܥܡ ܚܫܘܟܐ
15 Kuna mapatano gani kati ya Kristo na Beliari? Yeye aaminiye ana sehemu gani na yeye asiyeamini?
ܐܘ ܐܝܕܐ ܫܠܡܘܬܐ ܐܝܬ ܠܡܫܝܚܐ ܥܡ ܤܛܢܐ ܐܘ ܐܝܕܐ ܡܢܬܐ ܐܝܬ ܠܕܡܗܝܡܢ ܥܡ ܕܠܐ ܡܗܝܡܢ
16 Kuna mapatano gani kati ya Hekalu la Mungu na sanamu? Kwa kuwa sisi tu Hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu alivyosema: “Nitakaa pamoja nao na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
ܐܝܕܐ ܕܝܢ ܐܘܝܘܬܐ ܐܝܬ ܠܗܝܟܠܗ ܕܐܠܗܐ ܥܡ ܕܫܐܕܐ ܐܢܬܘܢ ܕܝܢ ܗܝܟܠܗ ܐܢܬܘܢ ܕܐܠܗܐ ܚܝܐ ܐܝܟܢܐ ܕܐܡܝܪ ܕܐܥܡܪ ܒܗܘܢ ܘܐܗܠܟ ܒܗܘܢ ܘܐܗܘܐ ܐܠܗܗܘܢ ܘܗܢܘܢ ܢܗܘܘܢ ܠܝ ܥܡܐ
17 “Kwa hiyo tokeni miongoni mwao, mkatengwe nao, asema Bwana. Msiguse kitu chochote kilicho najisi, nami nitawakaribisha.”
ܡܛܠ ܗܢܐ ܦܘܩܘ ܡܢ ܒܝܢܬܗܘܢ ܘܐܬܦܪܫܘ ܡܢܗܘܢ ܐܡܪ ܡܪܝܐ ܘܠܛܡܐܐ ܠܐ ܬܬܩܪܒܘܢ ܘܐܢܐ ܐܩܒܠܟܘܢ
18 “Mimi nitakuwa Baba kwenu, nanyi mtakuwa wanangu na binti zangu, asema Bwana Mwenyezi.”
ܘܐܗܘܐ ܠܟܘܢ ܠܐܒܐ ܘܐܢܬܘܢ ܬܗܘܘܢ ܠܝ ܠܒܢܝܐ ܘܠܒܢܬܐ ܐܡܪ ܡܪܝܐ ܕܟܠ ܐܚܝܕ

< 2 Wakorintho 6 >