< 2 Wakorintho 5 >

1 Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios g166)
We know that if the earthly dwelling that we live in is destroyed, we have a building from God. It is a house not made by human hands, but an eternal house, in heaven. (aiōnios g166)
2 Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
For in this tent we groan, longing to be clothed with our heavenly dwelling.
3 kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.
We long for this because by putting it on we will not be found to be naked.
4 Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
For indeed while we are in this tent, we groan, being burdened. We do not want to be unclothed. Instead, we want to be clothed, so that what is mortal may be swallowed up by life.
5 Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.
The one who prepared us for this very thing is God, who gave us the Spirit as a guarantee of what is to come.
6 Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana,
Therefore always be confident. Be aware that while we are at home in the body, we are away from the Lord.
7 kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.
For we walk by faith, not by sight.
8 Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana.
So we have confidence. We would rather be away from the body and at home with the Lord.
9 Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana.
So we make it our goal, whether we are at home or away, to please him.
10 Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.
For we must all appear before the judgment seat of Christ, so that each one may receive what is due for the things done in the body, whether for good or for bad.
11 Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia.
Therefore, knowing the fear of the Lord, we persuade people. What we are is clearly seen by God. I expect that it is also clear to your conscience.
12 Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni.
We are not trying to persuade you again to view us as sincere. Instead, we are giving you a reason to be proud of us, so you may have an answer for those who boast about appearances but not about what is in the heart.
13 Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu.
For if we are out of our minds, it is for God; and if we are in our right minds, it is for your sake.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa.
For the love of Christ compels us, because we are certain of this: That one person died for all, and that therefore all have died.
15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.
He died for all, so that those who live should live no longer for themselves but for him who for their sake died and was raised.
16 Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo.
For this reason, from now on we do not judge anyone according to human standards, even though we once regarded Christ in this way. But now we do not judge anyone in this way any longer.
17 Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya.
Therefore, if anyone is in Christ, he is a new creation. The old things have passed away. See, they have become new.
18 Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho:
All these things are from God. He reconciled us to himself through Christ, and has given us the ministry of reconciliation.
19 Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.
That is, in Christ God is reconciling the world to himself, not counting their trespasses against them. He is entrusting to us the message of reconciliation.
20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
So we are appointed as representatives of Christ, as though God were making his appeal through us. We plead with you, for the sake of Christ: “Be reconciled to God!”
21 Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.
He made Christ become the sacrifice for our sin. He is the one who never sinned. He did this so that we might become the righteousness of God in him.

< 2 Wakorintho 5 >