< 2 Wakorintho 5 >

1 Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios g166)
Now we know that if the earthly tent we live in is destroyed, we have a building from God, an eternal house in heaven, not made by human hands. (aiōnios g166)
2 Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
For in this tent we groan, longing to be further clothed with our heavenly dwelling,
3 kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.
because when we are clothed, we will not be found naked.
4 Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
For while we are in this tent, we groan and are burdened, not because we want to be unclothed, but further clothed, so that what is mortal may be swallowed up by life.
5 Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.
Now he who has prepared us for this very thing is God, who has also given us the Spirit as a guarantee.
6 Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana,
Therefore we have courage at all times, and we know that while we are at home in the body we are away from the Lord.
7 kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.
For we walk by faith, not by sight.
8 Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana.
Yes, we have courage and would rather be away from the body and at home with the Lord.
9 Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana.
Therefore, whether we are at home or away, we aspire to be pleasing to him.
10 Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.
For we must all appear before the judgment seat of Christ, so that each of us may receive his due for what he has done in the body, whether good or evil.
11 Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia.
Therefore, because we know what it is to fear the Lord, we persuade others. What we are is known to God, and I hope that it is known in your consciences as well.
12 Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni.
For we are not commending ourselves to you again, but we are giving you an opportunity to boast about us, so that you may be able to answer those who boast about outward appearances and not about matters of the heart.
13 Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu.
If we are out of our mind, it is for God; if we are in our right mind, it is for you.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa.
For the love of Christ compels us, because we have concluded that if one died for all, then all have died.
15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.
And he died for all so that those who live may no longer live for themselves, but for him who died for them and was raised.
16 Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo.
So from now on we regard no one according to the flesh. Even if we have known Christ according to the flesh, we no longer know him in that way.
17 Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya.
Therefore, if anyone is in Christ, he is a new creation. Old things have passed away; behold, all things have become new.
18 Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho:
And all these things are from God, who reconciled us to himself through Jesus Christ and gave us the ministry of reconciliation,
19 Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.
namely, that God was reconciling the world to himself in Christ, not counting people's trespasses against them. And he has committed to us the message of reconciliation.
20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
Therefore, we are ambassadors for Christ, as though God were making an appeal through us. We plead on Christ's behalf: “Be reconciled to God.”
21 Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.
For God made him who did not know sin to be a sin offering for us, so that in him we might become the righteousness of God.

< 2 Wakorintho 5 >