< 2 Wakorintho 5 >
1 Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios )
FOR we know that if our earthly house of this body were dissolved, we have nevertheless a building that is by Aloha; a house which is not made with hands, in the heaven, eternal. (aiōnios )
2 Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
For concerning this also we groan, and long to put on our house which is from heaven,
3 kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.
if, when that we have clothed, we may not be found naked.
4 Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
For now while we are in this house, we groan from the weight of it: yet are we not willing to cast it off, but to be clothed upon of it, that its mortality might be swallowed up in life.
5 Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.
And he who prepareth us for this is Aloha, who hath given to us the earnest-pledge of his Spirit.
6 Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana,
For therefore do we know and are persuaded, that so long as we remain in the body we are in pilgrimage from our Lord.
7 kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.
For by faith we walk, and not by sight.
8 Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana.
On this account we confide, and long to pass away from the body, and to be with our Lord.
9 Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana.
We give diligence, that whether we are pilgrims or inhabitants, we may be pleasing unto Him.
10 Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.
For we are all to stand before the tribunal of the Meshiha, that every man may be recompensed in his body (for) that which is done in it, whether of good or of evil.
11 Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia.
THEREFORE, because we know the terror of our Lord, we persuade men; and to Aloha we are manifest; but I hope that to your minds also we are manifest.
12 Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni.
For we commend not ourselves again to you, but we give you cause to be boastful of us to them who in appearance boast, but not in heart.
13 Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu.
For if we be beside ourselves, (it is) unto Aloha; and if we be right, (it is) unto you.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa.
For the love of the Meshiha constraineth us, because we judge this, That if one for every man hath died, then (was) every man dead.
15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.
And for every man he died, that they who live should not live to themselves, but to him who on their behalf died and arose.
16 Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo.
And henceforth we no man know according to the flesh; and if we have known the Meshiha according to the flesh, yet from now we know not.
17 Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya.
Whoever therefore is in the Meshiha is a new creature; the old things have passed, and every thing hath become new
18 Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho:
from Aloha, who hath reconciled us to himself in the Meshiha, and given to us the ministry of reconciliation.
19 Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.
For Aloha is in the Meshiha, who hath reconciled the world with his greatness; and he hath not reckoned unto them their sins, and hath put in us the word of reconciliation.
20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
WE are ambassadors then for the Meshiha, and as if Aloha himself besought you by us: instead of the Meshiha, therefore, we beseech, Be you reconciled unto Aloha.
21 Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.
For Him who knew not sin, on our account hath he made sin, that we might be in him the righteousness of Aloha.