< 2 Wakorintho 5 >

1 Kwa maana twajua kama hema yetu ya dunia tunayoishi ikiharibiwa, tunalo jengo kutoka kwa Mungu, nyumba iliyo ya milele kule mbinguni, isiyojengwa kwa mikono ya wanadamu. (aiōnios g166)
FOR we know that if our earthly house of this tabernacle should be taken down, we have a building from God, a house not made with hands, eternal in the heavens. (aiōnios g166)
2 Katika hema hii twalia kwa uchungu, tukitamani kuvikwa makao yetu ya mbinguni,
For in this we groan, earnestly desiring to be clothed with our mansion which is from heaven;
3 kwa kuwa tukiisha kuvikwa hatutaonekana tena kuwa uchi.
that so invested, we may not be found naked.
4 Kwa kuwa tukiwa bado katika hema hii twalia kwa uchungu na kulemewa, kwa sababu hatutaki kuvuliwa bali kuvikwa makao yetu ya mbinguni ili kwamba kile kipatikanacho na mauti kimezwe na uzima.
For we which are in this tabernacle, groan, being burdened; wherein we desire not to be unclothed, but clothed upon, that what is mortal may be swallowed up of life.
5 Basi Mungu ndiye alitufanya kwa ajili ya jambo lilo hilo naye ametupa Roho Mtakatifu kuwa amana, akituhakikishia ahadi ya kile kijacho.
But he that hath wrought us for this very thing is God, who also hath given us the earnest of the spirit.
6 Kwa hiyo siku zote tunalo tumaini, hata ingawa tunajua kwamba wakati tukiwa katika mwili huu, tuko mbali na Bwana,
Therefore we have always confidence, and know that whilst we are indwelling in the body, we are absent from the Lord:
7 kwa maana twaenenda kwa imani wala si kwa kuona.
(for we walk by faith, not by sight.)
8 Naam, tunalo tumaini na ingekuwa bora zaidi kuuacha mwili huu na kwenda kukaa na Bwana.
We are confident indeed, and with pleasure expect to go out from the body, and to dwell within with the Lord:
9 Kwa hiyo, kama tuko katika mwili huu au tuko mbali nao, lengo letu ni kumpendeza Bwana.
wherefore also our ambition is, that whether dwelling in the body, or out of the body, we may be acceptable to him.
10 Kwa kuwa sisi sote tutasimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apate kulipwa kwa ajili ya yale ambayo yametendwa katika mwili wake, yakiwa mema au mabaya.
For we must all appear before the judgment-seat of Christ, that each may receive the things done in the body according to what he hath done, whether it be good, or whether it be evil.
11 Basi, kwa kuwa tunajua kumcha Bwana, tunajitahidi kuwavuta wengine. Lakini Mungu anatufahamu dhahiri, nami natumaini kwamba tu dhahiri katika dhamiri zenu pia.
Knowing therefore the terror of the Lord, we persuade men; but we have been made manifest to God, and I hope also have been made manifest in your consciences.
12 Sio kwamba tunajaribu kujistahilisha kwenu tena, lakini tunataka kuwapa nafasi ili mwone fahari juu yetu mweze kuwajibu hao wanaoona fahari juu ya mambo yanayoonekana badala ya mambo yaliyo moyoni.
For we commend not ourselves again unto you, but give you occasion of glorying on our behalf, that ye may have an answer for those who glory in countenance, and not in heart.
13 Kama tumerukwa na akili, ni kwa ajili ya Mungu; kama tuna akili timamu, ni kwa ajili yenu.
For if we are transported out of ourselves, it is for God; or if we are sober-minded, it is for your sake.
14 Kwa kuwa upendo wa Kristo unatutia nguvu, kwa sababu tunasadiki kuwa mmoja alikufa kwa ajili ya wote, kwa hiyo wote walikufa.
For the love of Christ constraineth us, because we judge thus, that if one died for all, then were all dead:
15 Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, ili kwamba wote wanaoishi wasiishi tena kwa ajili ya nafsi zao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa na kufufuliwa tena kwa ajili yao.
and he died for all, that they who live should not henceforth live unto themselves, but unto him that died for them, and rose again.
16 Hivyo tangu sasa hatumwangalii mtu yeyote kwa mtazamo wa kibinadamu. Ingawa wakati fulani tulimwangalia Kristo kwa namna ya kibinadamu, hatumwangalii tena hivyo.
Wherefore from the present moment know we no man after the flesh: yea though we have also known Christ after the flesh, yet so henceforth know we him no more.
17 Kwa hiyo kama mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama, yamekuwa mapya.
Wherefore if any person be in Christ, he is a new creation: the old things are passed away; behold, all things are become new.
18 Haya yote yanatokana na Mungu, ambaye ametupatanisha sisi na nafsi yake kwa njia ya Yesu Kristo na kutupata sisi huduma ya upatanisho:
But all things are of God, who hath reconciled us to himself by Jesus Christ, and hath given to us the ministry of reconciliation;
19 Kwamba Mungu alikuwa ndani ya Kristo akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake mwenyewe, akiwa hawahesabii watu dhambi zao. Naye ametukabidhi sisi ujumbe huu wa upatanisho.
namely, that God was in Christ, reconciling the world unto himself, not imputing to them their offences: and hath committed to us the word of reconciliation.
20 Kwa hiyo sisi ni mabalozi wa Kristo, kana kwamba Mungu anawasihi kupitia kwa vinywa vyetu. Nasi twawaomba sana ninyi kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
Therefore we are ambassadors for Christ, as though God exhorted you by us; we entreat you for Christ’s sake, be ye reconciled to God.
21 Kwa maana Mungu alimfanya yeye asiyekuwa na dhambi kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kufanywa haki ya Mungu kwake yeye.
For he hath made him, who knew no sin, to be a sin offering for us, that we might become the righteousness of God in him.

< 2 Wakorintho 5 >