< 2 Wakorintho 4 >

1 Kwa hiyo, kwa kuwa tuna huduma hii kwa rehema za Mungu, hatukati tamaa.
Wherefore, having this ministry, as we have received mercy, we do not falter;
2 Tumekataa mambo ya siri na ya aibu, wala hatufuati njia za udanganyifu, tukichanganya Neno la Mungu na uongo. Kinyume cha hayo, tunadhihirisha kweli waziwazi na kujitambulisha wenyewe kwenye dhamiri ya kila mtu mbele za Mungu.
but have commanded away the hidden things of shame, not walking in craftiness, nor handling the word of God deceitfully; but by the manifestation of the truth, commending ourselves to every man's conscience in the sight of God.
3 Hata nayo Injili yetu kama imetiwa utaji, ni kwa wale tu wanaopotea.
If then, indeed, our gospel be vailed, it is vailed among the destroyed;
4 Kwa habari yao, mungu wa dunia hii amepofusha akili za wasioamini, ili wasione nuru ya Injili ya utukufu wa Kristo, aliye sura ya Mungu. (aiōn g165)
among whom the god of this world has blinded the minds of the unbelieving, lest the light of the gospel of the glory of Christ, who is the image of God, might shine into them. (aiōn g165)
5 Kwa maana hatujihubiri sisi wenyewe ila tunamhubiri Yesu Kristo kuwa ni Bwana na sisi ni watumishi wenu kwa ajili ya Yesu.
Now, we do not preach ourselves, but Christ Jesus the Lord; and ourselves your servants, for Jesus' sake.
6 Kwa kuwa Mungu, yeye aliyesema, “Nuru na ingʼae gizani,” ameifanya nuru yake ingʼae mioyoni mwetu ili kutupatia nuru ya maarifa ya utukufu wa Mungu katika uso wa Kristo.
For God, who commanded light to shine out of darkness, has shined into our hearts, to give the light of the knowledge of the glory of God in the face of Jesus Christ.
7 Lakini tunayo hazina hii katika vyombo vya udongo, ili ijulikane wazi kwamba uwezo huu wa ajabu unatoka kwa Mungu wala si kwetu.
But we have this treasure in earthen vessels, that the excellency of the power might be of God, and not of us.
8 Twataabika kila upande lakini hatuangamizwi; twaona wasiwasi lakini hatukati tamaa;
We are pressed on every side, but not straitened; perplexed, but not in despair;
9 twateswa lakini hatuachwi; twatupwa chini lakini hatupondwi.
persecuted, but not utterly forsaken; cast down, but not destroyed.
10 Siku zote twachukua katika mwili kufa kwake Yesu ili kwamba uzima wa Yesu uweze kudhihirika katika miili yetu.
At all times carrying about in the body, the putting to death of Jesus, that the life also of Jesus may be manifested in our body.
11 Kwa maana sisi tulio hai siku zote tumetolewa tufe kwa ajili ya Yesu, ili kwamba uzima wake upate kudhihirishwa katika mwili wetu upatikanao na mauti.
For we who live are always exposed to death for the sake of Jesus, that the life also of Jesus may be manifested in our mortal flesh.
12 Hivyo basi, mauti inatenda kazi ndani yetu, bali uzima unatenda kazi ndani yenu.
So that death works in us, but life in you.
13 Imeandikwa, “Niliamini, kwa hiyo nimesema.” Kwa roho yule yule wa imani pia tuliamini na hivyo tunasema,
Yet, having the same spirit of faith, according to what is written, "I believed, therefore I have spoken"; we, also, believe, and therefore speak;
14 kwa sababu tunajua kwamba yeye aliyemfufua Bwana Yesu kutoka kwa wafu, atatufufua sisi pia pamoja na Yesu na kutuleta sisi pamoja nanyi mbele zake.
knowing that he who raised up the Lord Jesus, will raise us up, also, by Jesus, and will present us with you.
15 Haya yote ni kwa faida yenu, ili kwamba neema ile inavyowafikia watu wengi zaidi na zaidi, ipate kusababisha shukrani nyingi kwa utukufu wa Mungu.
For all these things are for your sakes; that the favor which has abounded to many, may, through the thanksgiving of the greater number, redound to the glory of God.
16 Kwa hiyo, hatukati tamaa. Ingawa utu wetu wa nje unachakaa, utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.
Wherefore, we do not faint; but, though, indeed, out outward man is impaired, yet the inward man is renewed, day by day.
17 Kwa maana dhiki yetu nyepesi iliyo ya kitambo inatutayarisha kwa ajili ya utukufu wa milele unaozidi kuwa mwingi kupita kiasi, (aiōnios g166)
For our momentary light afflictions work out for us an eternal weight of glory, great beyond expression; (aiōnios g166)
18 kwa sababu hatuangalii yale yanayoweza kuonekana bali yale yasiyoweza kuonekana. Kwa maana yale yanayoweza kuonekana ni ya kitambo tu, bali yale yasiyoweza kuonekana ni ya milele. (aiōnios g166)
while we are aiming, not at things seen, but at things unseen: for the things seen are temporal, but the things unseen are eternal. (aiōnios g166)

< 2 Wakorintho 4 >