< 2 Wakorintho 2 >

1 Hivyo nilikusudia moyoni mwangu nisifanye ziara nyingine yenye kuwaumiza ninyi.
Mais j'ai décidé pour moi-même de ne plus venir vers vous dans la tristesse.
2 Kwa kuwa kama nikiwahuzunisha ninyi, ni nani aliyebaki wa kunifurahisha isipokuwa ninyi ambao nimewahuzunisha?
Car si je vous attriste, qui me réjouira, sinon celui que j'attriste?
3 Niliandika hivyo kama nilivyofanya, ili nikija nisihuzunishwe na wale watu ambao wangenifanya nifurahi. Nina uhakika na ninyi nyote, kwamba wote mngeshiriki furaha yangu.
Et je vous ai écrit cela même, afin que, lorsque je viendrai, je ne sois pas attristé par ceux dont je dois me réjouir, ayant confiance en vous tous pour que ma joie soit partagée par vous tous.
4 Kwa maana niliwaandikia kutokana na dhiki kubwa na kutaabika sana kwa moyo wangu tena kwa machozi mengi, shabaha yangu si ili niwasababishe mhuzunike bali kuwaonyesha kina cha upendo wangu kwenu.
Car c'est dans la détresse et l'angoisse du cœur que je vous ai écrit avec beaucoup de larmes, non pour vous affliger, mais pour vous faire connaître l'amour que j'ai si abondamment pour vous.
5 Lakini ikiwa mtu yeyote amesababisha huzuni, kwa kiasi fulani hakunihuzunisha mimi kama vile alivyowahuzunisha ninyi nyote, ili nisiwe mkali kupita kiasi.
Mais si quelqu'un a causé de la peine, ce n'est pas à moi qu'il en a causé, mais en partie à vous tous, afin que je ne vous presse pas trop.
6 Adhabu hii aliyopewa na wengi inamtosha.
Ce châtiment infligé par la multitude est suffisant pour un tel homme;
7 Basi sasa badala yake, inawapasa kumsamehe na kumfariji, ili asigubikwe na huzuni kupita kiasi.
c'est pourquoi, au contraire, vous devriez plutôt lui pardonner et le consoler, de peur qu'un tel homme ne soit englouti par sa trop grande tristesse.
8 Kwa hiyo, nawasihi, mpate kuuthibitisha tena upendo wenu kwa ajili yake.
C'est pourquoi je vous prie de confirmer votre amour pour lui.
9 Sababu ya kuwaandikia ni kuona kama mngeweza kushinda hilo jaribio na kutii katika kila jambo.
C'est en effet dans ce but que j'ai aussi écrit, afin de connaître l'épreuve de vous, pour savoir si vous êtes obéissants en toutes choses.
10 Kama ninyi mkimsamehe mtu yeyote, mimi pia nimemsamehe. Kile nilichosamehe, kama kulikuwa na kitu chochote cha kusamehe, nimekwisha kusamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
Maintenant, moi aussi, je pardonne à quiconque vous pardonnez quelque chose. Car si j'ai pardonné quelque chose, c'est pour vous que je l'ai fait en présence du Christ,
11 ili Shetani asitushinde. Kwa maana hatuachi kuzijua hila zake.
afin que Satan ne puisse pas prendre l'avantage sur nous, car nous n'ignorons pas ses desseins.
12 Basi nilipofika Troa kuhubiri Injili ya Kristo na kukuta kwamba Bwana alikuwa amenifungulia mlango,
Or, lorsque j'arrivai à Troas pour la Bonne Nouvelle du Christ, et qu'une porte me fut ouverte dans le Seigneur,
13 bado nilikuwa sina utulivu akilini mwangu kwa sababu sikumkuta ndugu yangu Tito huko. Hivyo niliagana nao nikaenda Makedonia.
je n'avais aucun soulagement pour mon esprit, parce que je n'avais pas trouvé Tite, mon frère; mais, prenant congé d'eux, je me rendis en Macédoine.
14 Lakini Mungu ashukuriwe, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Kristo. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.
Or, grâces soient rendues à Dieu qui nous conduit toujours en triomphe dans le Christ, et qui révèle par nous en tout lieu l'odeur agréable de sa connaissance.
15 Kwa maana sisi kwa Mungu ni harufu nzuri ya manukato ya Kristo miongoni mwa wale wanaookolewa na kwa wale wanaopotea.
Car nous sommes une agréable odeur de Christ pour Dieu, pour ceux qui sont sauvés et pour ceux qui périssent:
16 Kwa wale wanaopotea, sisi ni harufu ya mauti iletayo mauti; lakini kwa wale wanaookolewa, sisi ni harufu nzuri iletayo uzima. Ni nani awezaye mambo hayo?
pour les uns, une odeur de mort à la mort, pour les autres, une agréable odeur de vie à la vie. Qui est suffisant pour ces choses?
17 Tofauti na watu wengine wengi, sisi hatufanyi biashara na Neno la Mungu kwa ajili ya kupata faida. Kinyume chake, katika Kristo tunalisema Neno la Mungu kwa unyoofu, kama watu tuliotumwa kutoka kwa Mungu.
Car nous ne sommes pas comme tant d'autres, colportant la parole de Dieu. Mais comme de sincérité, comme de Dieu, devant Dieu, nous parlons en Christ.

< 2 Wakorintho 2 >