< 2 Wakorintho 2 >
1 Hivyo nilikusudia moyoni mwangu nisifanye ziara nyingine yenye kuwaumiza ninyi.
And I decided this to myself, not to come again to you in sorrow,
2 Kwa kuwa kama nikiwahuzunisha ninyi, ni nani aliyebaki wa kunifurahisha isipokuwa ninyi ambao nimewahuzunisha?
for if I make you sorry, then who is he who is making me glad, except he who is made sorry by me?
3 Niliandika hivyo kama nilivyofanya, ili nikija nisihuzunishwe na wale watu ambao wangenifanya nifurahi. Nina uhakika na ninyi nyote, kwamba wote mngeshiriki furaha yangu.
And I wrote to you this same thing, that having come, I may not have sorrow from them of whom it was necessary [for] me to have joy, having confidence in you all, that my joy is of you all,
4 Kwa maana niliwaandikia kutokana na dhiki kubwa na kutaabika sana kwa moyo wangu tena kwa machozi mengi, shabaha yangu si ili niwasababishe mhuzunike bali kuwaonyesha kina cha upendo wangu kwenu.
for out of much tribulation and pressure of heart I wrote to you through many tears, not that you might be made sorry, but that you might know the love that I have more abundantly toward you.
5 Lakini ikiwa mtu yeyote amesababisha huzuni, kwa kiasi fulani hakunihuzunisha mimi kama vile alivyowahuzunisha ninyi nyote, ili nisiwe mkali kupita kiasi.
And if anyone has caused sorrow, he has not caused sorrow to me, but in part, that I may not burden you all;
6 Adhabu hii aliyopewa na wengi inamtosha.
sufficient to such a one is this punishment, that [is] by the greater part,
7 Basi sasa badala yake, inawapasa kumsamehe na kumfariji, ili asigubikwe na huzuni kupita kiasi.
so that, on the contrary, [it is] rather for you to forgive and to comfort, lest by over abundant sorrow such a one may be swallowed up;
8 Kwa hiyo, nawasihi, mpate kuuthibitisha tena upendo wenu kwa ajili yake.
for this reason, I call on you to confirm love to him,
9 Sababu ya kuwaandikia ni kuona kama mngeweza kushinda hilo jaribio na kutii katika kila jambo.
for this also I wrote, that I might know your proof, whether you are obedient in regard to all things.
10 Kama ninyi mkimsamehe mtu yeyote, mimi pia nimemsamehe. Kile nilichosamehe, kama kulikuwa na kitu chochote cha kusamehe, nimekwisha kusamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
And to whom you forgive anything—I also; for I also, if I have forgiven anything, to whom I have forgiven [it], because of you—in the person of Christ—[I forgive it, ]
11 ili Shetani asitushinde. Kwa maana hatuachi kuzijua hila zake.
that we may not be over-reached by Satan, for we are not ignorant of his schemes.
12 Basi nilipofika Troa kuhubiri Injili ya Kristo na kukuta kwamba Bwana alikuwa amenifungulia mlango,
And having come to Troas for the good news of the Christ, and a door having been opened to me in the LORD,
13 bado nilikuwa sina utulivu akilini mwangu kwa sababu sikumkuta ndugu yangu Tito huko. Hivyo niliagana nao nikaenda Makedonia.
I have not had rest to my spirit, on my not finding my brother Titus, but having taken leave of them, I went forth to Macedonia;
14 Lakini Mungu ashukuriwe, yeye ambaye siku zote hutufanya tuandamane kwa ushindi tukiwa ndani ya Kristo. Naye kupitia kwetu hueneza kila mahali harufu nzuri ya kumjua yeye.
and to God [is] thanks, who at all times is leading us in triumph in the Christ, and the fragrance of His knowledge He is revealing through us in every place;
15 Kwa maana sisi kwa Mungu ni harufu nzuri ya manukato ya Kristo miongoni mwa wale wanaookolewa na kwa wale wanaopotea.
we are a refreshing fragrance to God because of Christ, in those being saved, and in those being lost;
16 Kwa wale wanaopotea, sisi ni harufu ya mauti iletayo mauti; lakini kwa wale wanaookolewa, sisi ni harufu nzuri iletayo uzima. Ni nani awezaye mambo hayo?
to one, indeed, a fragrance of death to death, and to the other, a fragrance of life to life; and who is sufficient for these things?
17 Tofauti na watu wengine wengi, sisi hatufanyi biashara na Neno la Mungu kwa ajili ya kupata faida. Kinyume chake, katika Kristo tunalisema Neno la Mungu kwa unyoofu, kama watu tuliotumwa kutoka kwa Mungu.
For we are not as the many, adulterating the word of God, but as of sincerity—but as of God; in the presence of God, in Christ we speak.