< 2 Wakorintho 13 >
1 Hii ndiyo mara ya tatu mimi kuja kwenu. “Shtaka lolote lazima lithibitishwe na mashahidi wawili au watatu.”
This will be my third visit to you. Out of the mouth of two or three witnesses shall every word be confirmed.
2 Nimekwisha kuwaonya nilipokuwa pamoja nanyi mara ya pili. Sasa narudia wakati sipo, kwamba nikija tena sitawahurumia wale waliokuwa wametenda dhambi hapo awali na wengine wote,
I have said formerly, and I now forewarn you as when I was present the second time, so now when I am absent the second time, so now when I am absent, saying to those who had sinned before, and to all the rest, "If I come again, I will not spare,"
3 kwa kuwa mnadai uthibitisho kwamba Kristo anazungumza kwa kunitumia mimi. Yeye si dhaifu katika kushughulika nanyi, bali ana nguvu kati yenu.
Since you want a proof of Christ who is speaking in me, he who is not feeble toward you, but powerful among you.
4 Kwa kuwa alisulubiwa katika udhaifu, lakini anaishi kwa nguvu za Mungu. Vivyo hivyo, sisi tu dhaifu kupitia kwake, lakini katika kuwashughulikia ninyi tutaishi pamoja naye kwa nguvu za Mungu.
For though he was crucified through weakness, yet he now lives through the power of God. I also am weak, sharing in his weakness, but I shall live with him by the power of God.
5 Jichunguzeni wenyewe mwone kama mnaishi katika imani. Jipimeni wenyewe. Je, hamtambui ya kuwa Yesu Kristo yumo ndani yenu? Kama sivyo, basi, mmeshindwa kufikia kipimo hicho!
Examine yourselves to see if you are in the faith; put your own selves to the proof. Or do you not know, your own selves, that Jesus Christ is in you, unless indeed you fail to abide the proof?
6 Natumaini mtaona kuwa sisi hatukushindwa.
But I hope you will find that I abide the proof.
7 Lakini tunamwomba Mungu msije mkatenda kosa lolote, si ili sisi tuonekane kuwa tumeshinda hilo jaribio, bali ili ninyi mtende lililo haki, hata kama tutaonekana kuwa tumeshindwa.
And my prayer to God is that you may do no evil; not in order that I may appear approved, but that you may do what is noble, though I should seem unable to abide the proof.
8 Kwa maana hatuwezi kufanya lolote kinyume na kweli, bali kuithibitisha kweli tu.
For I have no power against the truth, but only in defense of the truth.
9 Tunafurahi wakati wowote sisi tunapokuwa dhaifu, lakini ninyi mkawa na nguvu. Nayo maombi yetu ni kwamba mpate kuwa wakamilifu.
For I am always glad whenever I am weak, but you are strong. For this also I am praying, for your perfect reformation.
10 Hii ndiyo sababu nawaandikia mambo haya wakati sipo, ili nikija nisiwe mkali katika kutumia mamlaka yangu, mamlaka Bwana aliyonipa ya kuwajenga ninyi wala si ya kuwabomoa.
For this reason I am writing thus while absent, so that when I come, I may not have to deal sharply, according to the authority which the Lord gave me for building up, and not for pulling down.
11 Hatimaye, ndugu zangu, kwaherini. Kuweni wakamilifu, mkafarijike, kuweni wa nia moja, kaeni kwa amani. Naye Mungu wa upendo na amani atakuwa pamoja nanyi.
Finally, brothers, farewell. Aim at perfection, take courage, be of one mind, live in peace; so shall the God of love and peace be with you.
12 Salimianeni ninyi kwa ninyi kwa busu takatifu.
Salute one another with a holy kiss.
13 Watakatifu wote wanawasalimu.
All the saints salute you.
14 Neema ya Bwana Yesu Kristo, na upendo wa Mungu, na ushirika wa Roho Mtakatifu ukae nanyi nyote. Amen.
The grace of our Lord Jesus Christ, and the love of God, and the fellowship of the Holy Spirit be with you all.