< 2 Wakorintho 10 >
1 Basi, mimi Paulo ninawasihi kwa unyenyekevu na upole wa Kristo, mimi niliye “mwoga” ninapokuwa pamoja nanyi ana kwa ana, lakini mwenye ujasiri nikiwa mbali nanyi!
Сам же аз Павел молю вы кротостию и тихостию Христовою, иже в лице убо смирен в вас, не сый же у вас дерзаю в вас.
2 Nawaomba nitakapokuja kwenu nisiwe na ujasiri dhidi ya watu fulani, kama ninavyotazamia kwa wale wanaodhani kwamba tunaishi kwa kufuata namna ya ulimwengu huu.
Молю же, да не присущ дерзаю надеянием, имже помышляю смети на некия непщующыя нас яко по плоти ходящих.
3 Ingawa tunaishi duniani, hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo.
Во плоти бо ходяще, не по плоти воинствуем:
4 Silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome,
оружия бо воинства нашего не плотская, но сильна Богом на разорение твердем: помышления низлагающе,
5 tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu, na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo,
и всяко возношение взимающееся на разум Божий, и пленяюще всяк разум в послушание Христово,
6 tena tukiwa tayari kuadhibu kila tendo la kutotii, kutii kwenu kutakapokamilika.
и в готовости имуще отмстити всяко преслушание, егда исполнится ваше послушание.
7 Angalieni yale yaliyo machoni penu. Kama mtu yeyote anaamini kuwa yeye ni mali ya Kristo, basi kumbuka kuwa kama ulivyo wa Kristo, vivyo hivyo na sisi ndivyo tulivyo.
Иже ли пред лицем, зрите? Аще кто надеется себе Христова быти, да помышляет паки от себе, зане, якоже он Христов, такожде и мы Христовы.
8 Basi hata kama nikijisifu zaidi kidogo kuhusu mamlaka tuliyo nayo, ambayo Bwana alitupa ili kuwajenga wala si kuwabomoa, mimi sitaionea haya.
Аще бо и лишше что похвалюся о власти нашей, юже даде нам Господь в создание, а не на разорение ваше, не постыжуся.
9 Sitaki nionekane kama ninayejaribu kuwatisha kwa nyaraka zangu.
Но да не явлюся, яко страшя вас посланьми.
10 Kwa maana wanasema, “Nyaraka zake ni nzito na zenye nguvu, lakini ana kwa ana ni dhaifu na kuzungumza kwake ni kwa kudharauliwa.”
Яко послания убо, рече, тяжка и крепка, а пришествие тела немощно, и слово уничиженно:
11 Watu kama hao wajue ya kuwa, yale tusemayo kwa barua tukiwa hatupo pamoja nanyi, ndivyo tulivyo na ndivyo tutakavyofanya tutakapokuwa pamoja nanyi.
сие да помышляет таковый, яко яцы же есмы словом посланий, отстояще, таковии и ту суще есмы делом.
12 Hatuthubutu kujiweka kwenye kundi moja au kujilinganisha na hao wanaojitukuza wenyewe kuwa wao ni wa maana sana. Wanapojipima na kujilinganisha wenyewe kwa wenyewe, wanaonyesha ya kuwa hawana busara.
Не смеем бо судити, или прикладовати себе иным хвалящым себе самех: но сами в себе себе измеряюще, и прилагающе себе самим себе, не разумевают.
13 Lakini sisi hatujajivuna kupita kiasi, bali majivuno yetu yatakuwa katika mipaka ile Mungu aliyotuwekea, mipaka ambayo inawafikia hata ninyi.
Мы же не в безмерная похвалимся, но по мере правила, егоже раздели нам Бог меру, достизати даже и до вас.
14 Kwa maana hatukuwa tunavuka mipaka katika kujisifu kwetu, kama vile ambavyo ingekuwa kama hatukuwa tumekuja kwenu. Kwa maana sisi ndio tuliokuwa wa kwanza kuja kwenu na Injili ya Kristo.
Не яко бо не досяжуще до вас, паче простираем себе, даже бо и до вас достигохом благовестием Христовым:
15 Wala hatuvuki mipaka kwa kujisifu kwetu kwa ajili ya kazi iliyofanywa na watu wengine. Tumaini letu ni kwamba imani yenu inavyozidi kukua, eneo letu la utendaji miongoni mwenu litapanuka zaidi,
не в безмерная хвалящеся в чуждих трудех, упование же имуще, растущей вере вашей, в вас величатися по правилу нашему изобильно,
16 ili tuweze kuhubiri Injili sehemu zilizo mbali na maeneo yenu. Kwa maana hatutaki kujisifu kwa ajili ya kazi ambayo imekwisha kufanyika tayari katika eneo la mtu mwingine.
во еже и в дальших вас странах благовестити, не чужим правилом в готовых похвалитися.
17 Lakini, “Yeye ajisifuye na ajisifu katika Bwana.”
Хваляйся же, о Господе да хвалится:
18 Kwa maana si yeye ajisifuye mwenyewe akubaliwaye, bali yeye ambaye Bwana humsifu.
не хваляй бо себе сей искусен, но егоже Бог восхваляет.