< 2 Wakorintho 1 >
1 Barua hii ni kutoka kwangu mimi Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu, Kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, pamoja na watakatifu wote walioko Akaya yote:
To the Church of God which is in Corinth, and to all the saints throughout Greece. from Paul, by God’s will an apostle of Christ, and from brother Timothy.
2 Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo iwe nanyi.
Grace to you and peace from God our Father in the Lord Jesus Christ.
3 Ahimidiwe Mungu na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, Baba wa huruma na Mungu wa faraja yote.
Thanks be to the God and Father of our Lord Jesus Christ, the Father of tender mercies and the God of all comfort,
4 Yeye hutufariji katika taabu zetu, ili tuweze kuwafariji walio katika taabu yoyote kwa faraja ambayo sisi wenyewe tumepokea kutoka kwa Mungu.
who ever comforts me in all my troubles, so that I may be continually able to comfort those who are in any trouble by the comfort with which God is ever comforting me.
5 Kama vile mateso ya Kristo yanavyozidi ndani ya maisha yetu, hivyo ndivyo faraja yetu inavyofurika kwa njia ya Kristo.
For just as I have more than my share in the sufferings of the Christ, so also through the Christ I have more than my share of comfort.
6 Kama tunataabika, ni kwa ajili ya faraja na wokovu wenu; kama tukifarijiwa, ni kwa ajili ya faraja yenu, iwaleteayo saburi ya mateso yale yale yanayotupata.
If I am afflicted, it is for your comfort and salvation; and if I am receiving comfort, it is for your comfort - a comfort produced within you by your patient fortitude, under the same sufferings which I also am enduring.
7 Nalo tumaini letu kwenu ni thabiti, kwa sababu tunajua kwamba kama vile mnavyoshiriki mateso yetu, ndivyo pia mnavyoshiriki katika faraja yetu.
My hope for you is firm; for I know that as you are comrades in my sufferings, so also are you comrades in my comfort.
8 Ndugu wapendwa, hatutaki mkose kujua kuhusu zile taabu tulizopata huko Asia. Kwa maana tulilemewa na mizigo sana, kiasi cha kushindwa kuvumilia, hata tulikata tamaa ya kuishi.
Now, brothers, I want you to know about the troubles which befell me in Asia; how I was burdened altogether beyond my strength, so that I renounced all hope even of life itself.
9 Kwa kweli, mioyoni mwetu tulihisi tumekabiliwa na hukumu ya kifo, ili tusijitegemee sisi wenyewe bali tumtegemee Mungu afufuaye wafu.
Indeed, I had in myself, and still have, the sentence of death, in order that I might not rely on myself, but on God who raises the dead to life.
10 Yeye aliyetuokoa kwenye hatari kubwa ya kifo na atatuokoa tena. Kwake yeye tumeweka tumaini letu kwamba ataendelea kutuokoa.
He delivered me from such a death, and will deliver me. On him I have set my hopes that he will continue to deliver me,
11 Kama vile mlivyoungana kusaidiana nasi katika maombi, hivyo wengi watatoa shukrani kwa niaba yetu kwa ajili ya baraka za neema tulizopata kwa majibu ya maombi ya wengi.
while all of you also are helping me by your prayers; so that from many lips thanksgiving may rise on my behalf for the blessings vouchsafed to me through the intercessions of many.
12 Basi haya ndiyo majivuno yetu: Dhamiri yetu inatushuhudia kwamba tumeenenda katika ulimwengu na hasa katika uhusiano wetu na ninyi, katika utakatifu na uaminifu utokao kwa Mungu. Hatukufanya hivyo kwa hekima ya kidunia bali kwa neema ya Mungu.
For this is my proud boast, the testimony of my conscience, that it was in holiness and with pure motives before God, not in worldly wisdom, but in the grace of God, that I have conducted myself in the world, and above all in my relations with you.
13 Kwa maana hatuwaandikii mambo ambayo hamwezi kusoma au kuyaelewa. Natumaini kwamba,
For I am writing to you nothing different from what you read aloud and very well recognize, and I hope will continue to recognize to the very end,
14 kama vile mlivyotuelewa kwa sehemu, mtakuja kuelewa kwa ukamilifu ili mweze kujivuna kwa ajili yetu, kama na sisi tutakavyojivuna kwa ajili yenu katika siku ya Bwana Yesu.
as some indeed did recognize in part at last, that I am your cause of boasting, just as you will be mine on the Day of Jesus our Lord.
15 Kwa kuwa nilikuwa na uhakika wa mambo haya, nilitaka nije kwenu kwanza, ili mpate faida mara mbili.
And in this confidence I intended to visit you, before going elsewhere, that you might have a pleasure twice over.
16 Nilipanga kuwatembelea nikiwa safarini kwenda Makedonia na kurudi tena kwenu nikitoka Makedonia, ili mnisafirishe katika safari yangu ya kwenda Uyahudi.
I intended to go by you into Macedonia, and to come again to you from Macedonia, and by you to be sent forward on my way to Judea.
17 Nilipopanga jambo hili, je, nilikuwa kigeugeu? Au ninafanya mipango yangu kwa hali ya mwili, ili niseme, “Ndiyo, ndiyo” na “Siyo, siyo” wakati huo huo?
In purposing this did I display "caprice"? Or what I purpose do I purpose in a worldly way, so that it may mean either "Yes, yes," or "No, no"?
18 Hakika kama Mungu alivyo mwaminifu, maneno yetu kwenu hayajawa “Ndiyo na Siyo.”
As God is faithful, my message to you is not now "Yes," now "No."
19 Kwa kuwa Yesu Kristo, Mwana wa Mungu, ambaye tulimhubiri kwenu: Mimi, Silvano na Timotheo, hakuwa “Ndiyo” na “Siyo,” bali kwake yeye siku zote ni “Ndiyo.”
For Jesus Christ, Son of God, who was proclaimed among you by us, that is, by Silvanus and Timothy and me, was not wavering between "Yes" and "No," but in him is the everlasting "Yes."
20 Kwa maana ahadi zote za Mungu zilizo katika Kristo ni “Ndiyo.” Kwa sababu hii ni kwake yeye tunasema “Amen” kwa utukufu wa Mungu.
For however many are the promises of God, in him they are "Yes." Therefore also through him let the Amen be said by our voices to the glory of God.
21 Basi ni Mungu atufanyaye sisi pamoja nanyi kusimama imara katika Kristo. Ametutia mafuta
And he who has established me with you in the Anointed One, and has anointed me, is God.
22 kwa kututia muhuri wake na kutupa Roho wake mioyoni mwetu kuwa rehani kwa ajili ya kututhibitishia kile kijacho.
He has also set his seal upon me, and given me the pledge of his Spirit in my heart.
23 Mungu ni shahidi wangu kwamba ilikuwa ni kwa ajili ya kuwahurumia ninyi sikurudi Korintho.
But for my part I call God to witness, as my soul shall answer for it, that it was to spare you that I came not to Corinth
24 Si kwamba tunatawala imani yenu, bali twatenda kazi pamoja nanyi kwa ajili ya furaha yenu, kwa sababu ni kwa imani mwasimama imara.
(not that I am attempting to lord it over your faith, but rather to work with you for your happiness); for your faith is stedfast.