< 2 Nyakati 1 >

1 Solomoni mwana wa Daudi alijiimarisha kwenye milango yote! Katika ufalme wake, kwa kuwa Bwana Mungu wake alikuwa pamoja naye, naye akamfanya mkuu mno.
and to strengthen: strengthen Solomon son: child David upon royalty his and LORD God his with him and to magnify him to/for above [to]
2 Ndipo Solomoni akasema na Israeli wote, majemadari wa maelfu na majemadari wa mamia, waamuzi na viongozi wote katika Israeli, pamoja na wakuu wa jamaa.
and to say Solomon to/for all Israel to/for ruler [the] thousand and [the] hundred and to/for to judge and to/for all leader to/for all Israel head [the] father
3 Naye Solomoni na kusanyiko lote wakakwea mpaka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kwa kuwa huko ndiko Hema la Kukutania la Mungu lilipokuwa, ambalo Mose mtumishi wa Bwana alikuwa amelitengeneza huko jangwani.
and to go: went Solomon and all [the] assembly with him to/for high place which in/on/with Gibeon for there to be tent meeting [the] God which to make Moses servant/slave LORD in/on/with wilderness
4 Basi Daudi alikuwa amelipandisha Sanduku la Mungu kutoka Kiriath-Yearimu mpaka mahali alipokuwa amepatengeneza kwa ajili yake, kwa sababu alikuwa amesimamisha hema kwa ajili ya hilo Sanduku huko Yerusalemu.
truly ark [the] God to ascend: establish David from Kiriath-jearim Kiriath-jearim in/on/with to establish: prepare to/for him David for to stretch to/for him tent in/on/with Jerusalem
5 Lakini yale madhabahu ya shaba ambayo Bezaleli mwana wa Uri, mwana wa Huri, alikuwa ametengeneza yalikuwa huko Gibeoni mbele ya Maskani ya Bwana Mungu, hivyo Solomoni na kusanyiko lote walimtafuta Mungu huko.
and altar [the] bronze which to make Bezalel son: child Uri son: child Hur to set: make to/for face: before tabernacle LORD and to seek him Solomon and [the] assembly
6 Solomoni akapanda huko yalikokuwa madhabahu ya shaba mbele za Bwana katika Hema la Kukutania, na kutoa dhabihu 1,000 za sadaka za kuteketezwa juu yake.
and to ascend: rise Solomon there upon altar [the] bronze to/for face: before LORD which to/for tent meeting and to ascend: offer up upon him burnt offering thousand
7 Usiku ule Mungu akamtokea Solomoni na kumwambia, “Omba lolote utakalo nikupe.”
in/on/with night [the] he/she/it to see: see God to/for Solomon and to say to/for him to ask what? to give: give to/for you
8 Solomoni akamjibu Mungu, “Umemwonyesha baba yangu Daudi fadhili nyingi, nawe umeniweka niwe mfalme mahali pake.
and to say Solomon to/for God you(m. s.) to make: do with David father my kindness great: large and to reign me underneath: instead him
9 Sasa, Bwana Mungu, ahadi yako kwa baba yangu Daudi na ithibitike, kwa kuwa umenifanya mimi mfalme juu ya watu ambao ni wengi kama mavumbi ya nchi.
now LORD God be faithful word your with David father my for you(m. s.) to reign me upon people many like/as dust [the] land: soil
10 Nakuomba unipe mimi hekima na maarifa, ili niweze kuongoza watu hawa, kwa kuwa ni nani awezaye kutawala hawa watu wako walio wengi hivi?”
now wisdom and knowledge to give: give to/for me and to come out: come to/for face: before [the] people [the] this and to come (in): come for who? to judge [obj] people your [the] this [the] great: large
11 Mungu akamwambia Solomoni, “Kwa kuwa jambo hili ndilo shauku ya moyo wako na hukuomba mali, utajiri au heshima, wala kifo kwa ajili ya adui zako, nawe kwa kuwa hukuomba maisha marefu, bali umeomba hekima na maarifa ili kuongoza watu wangu ambao nimekufanya uwe mfalme juu yao,
and to say God to/for Solomon because which to be this with heart your and not to ask riches wealth and glory and [obj] soul: life to hate you and also day many not to ask and to ask to/for you wisdom and knowledge which to judge [obj] people my which to reign you upon him
12 kwa hiyo utapewa hekima na maarifa. Tena nitakupa pia mali, utajiri na heshima, ambavyo hakuna mfalme yeyote aliyekuwepo kabla yako amewahi kuwa navyo, na hakuna yeyote baada yako atakayekuwa navyo.”
[the] wisdom and [the] knowledge to give: give to/for you and riches and wealth and glory to give: give to/for you which not to be so to/for king which to/for face: before your and after you not to be so
13 Ndipo Solomoni akaenda mpaka Yerusalemu kutoka mahali pa juu pa kuabudia huko Gibeoni, kutoka mbele ya Hema la Kukutania. Naye akatawala Israeli.
and to come (in): come Solomon to/for high place which in/on/with Gibeon Jerusalem from to/for face: before tent meeting and to reign upon Israel
14 Solomoni akakusanya magari ya vita na farasi. Alikuwa na magari 1,400 na farasi 12,000, ambayo aliyaweka katika miji ya magari na mengine akawa nayo huko Yerusalemu.
and to gather Solomon chariot and horseman and to be to/for him thousand and four hundred chariot and two ten thousand horseman and to rest them in/on/with city [the] chariot and with [the] king in/on/with Jerusalem
15 Mfalme akafanya fedha na dhahabu kuwa vitu vya kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
and to give: make [the] king [obj] [the] silver: money and [obj] [the] gold in/on/with Jerusalem like/as stone and [obj] [the] cedar to give: make like/as sycamore which in/on/with Shephelah to/for abundance
16 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka Kue. Wafanyabiashara wa mfalme waliwanunua kutoka Kue.
and exit [the] horse which to/for Solomon from Egypt and from Kue to trade [the] king from Kue to take: buy in/on/with price
17 Waliagiza magari kutoka Misri kwa bei ya shekeli 600 za fedha, na farasi kwa shekeli 150. Pia waliwauza nje kwa wafalme wote wa Wahiti na wa Waaramu.
and to ascend: establish and to come out: send from Egypt chariot in/on/with six hundred silver: money and horse in/on/with fifty and hundred and so to/for all king [the] Hittite and king Syria in/on/with hand: by their to come out: send

< 2 Nyakati 1 >