< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Ko je kraljica iz Sabe slišala o Salomonovi slavi, je prišla v Jeruzalem, da Salomona preizkusi s težkimi vprašanji, z zelo veliko skupino in kamelami, ki so nosile dišave, zlata v obilju in dragocene kamne. Ko je prišla k Salomonu, se je z njim posvetovala o vsem, kar je bilo na njenem srcu.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
Salomon ji je odgovoril [na] vsa njena vprašanja. Ničesar ni bilo skrito pred Salomonom, česar ji ne bi povedal.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
Ko je kraljica iz Sabe videla Salomonovo modrost in hišo, ki jo je zgradil,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
hrano njegove mize, sedenje njegovih služabnikov, položaj njegovih služabnikov in njihovo obleko; tudi njegove dvorne točaje in njihovo obleko in njegov vzpon, s katerim je odšel gor v Gospodovo hišo, tam ni bilo več duha v njej.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
Kralju je rekla: » To je bilo resnično poročilo, ki sem ga slišala v svoji lastni deželi o tvojih dejanjih in o tvoji modrosti.
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
Vendar nisem verjela njihovim besedam, dokler nisem prišla in so moje oči to videle. Glej, ni mi bilo povedano niti o eni polovici veličine tvoje modrosti, kajti presegaš slavo, ki sem jo slišala.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Srečni so tvoji možje in srečni so ti tvoji služabniki, ki nenehno stojijo pred teboj in poslušajo tvojo modrost.
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Blagoslovljen bodi Gospod, tvoj Bog, ki se je razveseljeval v tebi, da te postavi na svoj prestol, da bi bil kralj za Gospoda, tvojega Boga. Ker je tvoj Bog ljubil Izrael, da jih utrdi na veke, te je zato postavil [za] kralja nad njimi, da izvajaš sodbo in pravico.«
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Kralju je izročila sto dvajset talentov zlata, veliko obilje dišav in dragocene kamne. Niti ni bilo tam nobenih takšnih dišav, kot jih je kraljica iz Sabe izročila kralju Salomonu.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
Hurámovi služabniki in Salomonovi služabniki, ki so pripeljali zlato iz Ofírja, so pripeljali tudi sandalovino in dragocene kamne.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
Kralj je iz sandalovine naredil terase h Gospodovi hiši in h kraljevi palači in harfe ter plunke za pevce. Ničesar takšnega ni bilo prej videti v Judovi deželi.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
Kralj Salomon je kraljici iz Sabe izročil vse njene želje, karkoli je prosila, poleg tega, kar je prinesla h kralju. Tako se je obrnila in odšla proč k svoji lastni deželi, ona in njeni služabniki.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Torej teža zlata, ki je prišla k Salomonu v enem letu, je bila šeststo šestinšestdeset talentov zlata,
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
poleg tega, kar so prinašali krošnjarji in trgovci. Vsi kralji Arabije in voditelji dežele so Salomonu prinašali zlato in srebro.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
Kralj Salomon je naredil dvesto okroglih ščitov iz kovanega zlata. Šeststo šeklov iz kovanega zlata je šlo k enemu okroglemu ščitu.
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
Tristo ščitov je naredil iz kovanega zlata. Tristo šeklov zlata je šlo za en ščit. Kralj jih je postavil v hiši libanonskega gozda.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Poleg tega je kralj naredil velik prestol iz slonovine in ga prevlekel s čistim zlatom.
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
K prestolu je bilo šest stopnic, s pručko iz zlata, ki so bile pritrjene k prestolu in opori [za roke] na vsaki strani prostora za sedenje in dva leva, stoječa pri oporah [za roke].
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
Dvanajst levov je stalo tam na eni strani in na drugi, na šestih stopnicah. Ničesar podobnega ni bilo narejenega v nobenem kraljestvu.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
Vse posode za pitje kralja Salomona so bile iz zlata in vse posode hiše libanonskega gozda so bile iz čistega zlata. Nobena ni bila iz srebra, le-to ni bilo nič cenjeno v Salomonovih dneh.
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Kajti kraljeve ladje so odplule v Taršíš s Hurámovimi služabniki. Enkrat na vsaka tri leta so prišle ladje iz Taršíša, ki so pripeljale zlato, srebro, slonovino, opice in pave.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
Kralj Salomon je presegal vse zemeljske kralje v bogastvih in modrosti.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Vsi kralji zemlje so iskali Salomonovo prisotnost, da slišijo njegovo modrost, ki jo je Bog položil v njegovo srce.
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
Prinašali so mu vsak človek svoje darilo, posode iz srebra, posode iz zlata, oblačila, vprege, dišave, konje in mule, mero leto za letom.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
Salomon je imel štiri tisoč boksov za konje in bojne vozove in dvanajst tisoč konjenikov, ki jih je namestil v mestih za bojne vozove in s kraljem v Jeruzalemu.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
Kraljeval je nad vsemi kralji od reke celo do dežele Filistejcev in do meje Egipta.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
Kralj je naredil srebra v Jeruzalemu kakor kamnov in cedrovih dreves je naredil [toliko] kakor egiptovskih smokev, ki jih je na nizkih ravnicah v obilju.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
K Salomonu so vodili konje iz Egipta in iz vseh dežel.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
Torej preostala izmed Salomonovih dejanj, prva in zadnja, mar niso zapisana v knjigi preroka Natána in v prerokovanju Šilčana Ahíja in v videnjih vidca Idója zoper Nebátovega sina Jerobeáma?
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
Salomon je v Jeruzalemu nad Izraelom kraljeval štirideset let.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Salomon je zaspal s svojimi očeti in je bil pokopan v mestu svojega očeta Davida in namesto njega je zakraljeval njegov sin Rehabám.

< 2 Nyakati 9 >