< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
Kun Saban kuningatar kuuli Salomon maineen, tuli hän Jerusalemiin koettelemaan Salomoa arvoituksilla. Hän tuli sangen suuren seurueen kanssa, mukanaan kameleja, jotka kantoivat hajuaineita, kultaa ylen paljon ja kalliita kiviä. Ja kun hän tuli Salomon luo, puhui hän tälle kaikki, mitä hänellä oli mielessänsä.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
Mutta Salomo selitti hänelle kaikki hänen kysymyksensä; Salomolle ei mikään jäänyt ongelmaksi, jota hän ei olisi hänelle selittänyt.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
Kun Saban kuningatar näki kaiken Salomon viisauden, linnan, jonka hän oli rakentanut,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
ruuat hänen pöydällänsä, kuinka hänen palvelijansa asuivat ja hänen palvelusväkensä palveli ja kuinka he olivat puetut, ja näki hänen juomanlaskijansa ja kuinka he olivat puetut, ja hänen yläsalinsa, josta hän nousi Herran temppeliin, meni hän miltei hengettömäksi.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
Sitten hän sanoi kuninkaalle: "Totta oli se puhe, jonka minä kotimaahani sinusta ja sinun viisaudestasi kuulin.
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
Minä en uskonut, mitä sanottiin, ennenkuin itse tulin ja sain omin silmin nähdä; ja katso, ei puoltakaan sinun suuresta viisaudestasi oltu minulle kerrottu. Sinä olet paljon suurempi, kuin minä olin kuullut huhuttavan.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Onnellisia ovat sinun miehesi, onnellisia nämä palvelijasi, jotka aina saavat olla sinun edessäsi ja kuulla sinun viisauttasi.
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Kiitetty olkoon Herra, sinun Jumalasi, joka sinuun on niin mielistynyt, että on asettanut sinut valtaistuimellensa olemaan kuninkaana Herran, sinun Jumalasi, kunniaksi. Sentähden, että sinun Jumalasi rakastaa Israelia ja tahtoo pitää sen pystyssä ainiaan, on hän antanut sinut heille kuninkaaksi, tekemään sitä, mikä oikeus ja vanhurskaus on."
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Ja hän antoi kuninkaalle sata kaksikymmentä talenttia kultaa, sangen paljon hajuaineita ja kalliita kiviä. Ei milloinkaan ole ollut moisia hajuaineita kuin ne, jotka Saban kuningatar antoi kuningas Salomolle.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
Huuramin palvelijat ja Salomon palvelijat, jotka toivat kultaa Oofirista, toivat myöskin santelipuuta ja kalliita kiviä.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
Ja kuningas teetti santelipuusta portaat Herran temppeliin ja kuninkaan palatsiin ja kanteleita ja harppuja laulajille. Moisia ei oltu ennen nähty Juudan maassa.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
Kuningas Salomo taas antoi Saban kuningattarelle kaikki, mitä tämä halusi ja pyysi, antoi vielä enemmän, kuin mitä tämä oli tuonut kuninkaalle. Sitten hän lähti paluumatkalle ja meni palvelijoineen omaan maahansa.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Kullan paino, mikä yhtenä vuotena tuli Salomolle, oli kuusisataa kuusikymmentä kuusi talenttia kultaa,
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
paitsi mitä kauppamiehet ja kaupustelijat toivat. Sen lisäksi kaikki Arabian kuninkaat ja maan käskynhaltijat toivat Salomolle kultaa ja hopeata.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
Ja kuningas Salomo teetti kaksisataa suurta kilpeä pakotetusta kullasta ja käytti jokaiseen kilpeen kuusisataa sekeliä pakotettua kultaa;
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
samoin kolmesataa pienempää kilpeä pakotetusta kullasta, ja käytti jokaiseen kilpeen kolmesataa sekeliä kultaa. Ja kuningas asetti ne Libanoninmetsä-taloon.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Vielä kuningas teetti suuren norsunluisen valtaistuimen ja päällysti sen puhtaalla kullalla.
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
Valtaistuimessa oli kuusi porrasta ja astinlauta, kullalla kiinnitettyinä valtaistuimeen. Istuimen kummallakin puolella oli käsinoja, ja kaksi leijonaa seisoi käsinojan vieressä.
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
Ja kaksitoista leijonaa seisoi siinä kuudella portaalla, kummallakin puolella. Senkaltaista ei ole tehty missään muussa valtakunnassa.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
Ja kaikki kuningas Salomon juoma-astiat olivat kultaa, ja kaikki Libanoninmetsä-talon astiat olivat puhdasta kultaa. Hopeata ei Salomon päivinä pidetty minkään arvoisena.
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
Kuninkaalla oli näet laivoja, jotka kulkivat Tarsiiseen Huuramin palvelijain kanssa; kerran kolmessa vuodessa Tarsiin-laivat tulivat ja toivat kultaa ja hopeata, norsunluuta, apinoita ja riikinkukkoja.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
Ja kuningas Salomo oli kaikkia maan kuninkaita suurempi rikkaudessa ja viisaudessa.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
Ja kaikki maan kuninkaat pyrkivät näkemään Salomoa kuullaksensa hänen viisauttaan, jonka Jumala oli antanut hänen sydämeensä.
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
Ja he toivat kukin lahjansa: hopea-ja kultakaluja, vaatteita, aseita, hajuaineita, hevosia ja muuleja, joka vuosi vuoden tarpeen.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
Salomolla oli neljätuhatta hevosvaljakkoa vaunuineen ja kaksitoista tuhatta ratsumiestä; ne hän sijoitti vaunukaupunkeihin ja kuninkaan luo Jerusalemiin.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
Ja hän vallitsi kaikkia kuninkaita Eufrat-virrasta aina filistealaisten maahan ja Egyptin rajaan asti.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
Ja kuningas toimitti niin, että Jerusalemissa oli hopeata kuin kiviä, ja setripuuta niin paljon kuin metsäviikunapuita Alankomaassa.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
Ja hevosia tuotiin Salomolle Egyptistä ja kaikista muista maista.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
Mitä muuta Salomosta on kerrottavaa, hänen sekä aikaisemmista että myöhemmistä vaiheistaan, se on kirjoitettuna profeetta Naatanin historiassa, siilolaisen Ahian ennustuksessa ja näkijä Jeddon näyssä Jerobeamista, Nebatin pojasta.
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
Salomo hallitsi Jerusalemissa koko Israelia neljäkymmentä vuotta.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
Sitten Salomo meni lepoon isiensä tykö, ja hänet haudattiin isänsä Daavidin kaupunkiin. Ja hänen poikansa Rehabeam tuli kuninkaaksi hänen sijaansa.

< 2 Nyakati 9 >