< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
And the queen of Sheba hath heard of the fame of Solomon, and cometh in to try Solomon with acute sayings, to Jerusalem, with a very great company, and camels bearing spices and gold in abundance, and precious stone; and she cometh in unto Solomon, and speaketh with him all that hath been with her heart,
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
and Solomon declareth to her all her matters, and there hath not been hid a thing from Solomon that he hath not declared to her.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
And the queen of Sheba seeth the wisdom of Solomon, and the house that he hath built,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
and the food of his table, and the sitting of his servants, and the standing of his ministers, and their clothing, and his stewards, and their clothing, an his burnt-offering that he offered up in the house of Jehovah, and there hath not been any more spirit in her.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
And she saith unto the king, 'True [is] the word that I heard in my land concerning thy matters and concerning thy wisdom,
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
and I have given no credence to their words, till that I have come, and mine eyes see, and lo, there hath not been declared to me the half of the abundance of thy wisdom — thou hast added unto the report that I heard.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
'O the happiness of thy men, and the happiness of thy servants — these — who are standing before thee continually, and hearing thy wisdom.
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Let Jehovah thy God be blessed who hath delighted in thee, to put thee on His throne for king for Jehovah thy God; in the love of thy God to Israel, to establish it to the age, He hath put thee over them for king, to do judgment and righteousness.'
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
And she giveth to the king a hundred and twenty talents of gold, and spices in great abundance, and precious stone; and there hath not been any such spice as the queen of Sheba hath given to king Solomon.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
And also, servants of Huram, and servants of Solomon, who brought in gold from Ophir, have brought in algum-trees and precious stone.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
And the king maketh the algum-trees staircases for the house of Jehovah, and for the house of the king, and harps and psalteries for singers; and there have been none seen like these before in the land of Judah.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
And king Solomon hath given to the queen of Sheba all her desire that she asked, apart from that which she had brought unto the king, and she turneth and goeth to her land, she and her servants.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
And the weight of the gold that is coming to Solomon in one year is six hundred and sixty and six talents of gold,
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
apart from [what] the tourists, and the merchants, are bringing in; and all the kings of Arabia, and the governors of the land, are bringing in gold and silver to Solomon.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
And king Solomon maketh two hundred targets of alloyed gold, six hundred [shekels] of alloyed gold he causeth to go up on the one target;
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
and three hundred shields of alloyed gold, three hundred [shekels] of gold he causeth to go up on the one shield, and the king putteth them in the house of the forest of Lebanon.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
And the king maketh a great throne of ivory, and overlayeth it with pure gold;
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
and six steps [are] to the throne, and a footstool of gold, to the throne they are fastened, and hands [are] on this [side] and on that on the place of the sitting, and two lions are standing near the hands,
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
and twelve lions are standing there on the six steps on this [side], and on that: it hath not been made so for any kingdom.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
And all the drinking vessels of king Solomon [are] of gold, and all the vessels of the house of the forest of Lebanon [are] of refined gold — silver is not reckoned in the days of Solomon for anything;
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
for ships of the king are going to Tarshish, with servants of Huram: once in three years come do the ships of Tarshish bearing gold, and silver, ivory, apes, and peacocks.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
And king Solomon becometh greater than any of the kings of the earth for riches and wisdom;
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
and all the kings of the earth are seeking the presence of Solomon to hear his wisdom that God hath put in his heart,
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
and they are bringing in each his present, vessels of silver, and vessels of gold, and garments, harness, and spices, horses, and mules, a rate year by year.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
And there are to Solomon four thousand stalls for horses and chariots, and twelve thousand horsemen, and he placed them in cities of the chariot, and with the king in Jerusalem.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
And he is ruling over all the kings from the River even unto the land of the Philistines, and unto the border of Egypt.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
And the king maketh the silver in Jerusalem as stones, and the cedars he hath made as sycamores, that [are] in the low country, for abundance,
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
and they are bringing out horses from Egypt to Solomon, and from all the lands.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
And the rest of the matters of Solomon, the first and the last, are they not written beside the matters of Nathan the prophet, and beside the prophecy of Ahijah the Shilonite, and with the visions of Iddo the seer concerning Jeroboam son of Nebat?
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
And Solomon reigneth in Jerusalem over all Israel forty years,
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
and Solomon lieth with his fathers, and they bury him in the city of David his father, and reign doth Rehoboam his son in his stead.

< 2 Nyakati 9 >