< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
And when the queen of Sheba heard of the fame of Solomon, she came to prove Solomon with hard questions at Jerusalem, with a very great company, and camels that bore spices, and gold in abundance, and precious stones: and when she had come to Solomon, she communed with him of all that was in her heart.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
And Solomon told her all her questions: and there was nothing hid from Solomon which he told her not.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
And when the queen of Sheba had seen the wisdom of Solomon, and the house that he had built,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
And the provisions of his table, and the sitting of his servants, and the attendance of his ministers, and their apparel; his cup-bearers also, and their apparel; and his ascent by which he went up into the house of the LORD; there was no more spirit in her.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
And she said to the king, [It was] a true report which I heard in my own land of thy acts, and of thy wisdom:
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
Yet, I believed not their words, until I came, and my eyes had seen [it]: and behold, the one half of the greatness of thy wisdom was not told to me: [for] thou exceedest the fame that I heard.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Happy [are] thy men, and happy [are] these thy servants, who stand continually before thee, and hear thy wisdom.
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Blessed be the LORD thy God, who delighted in thee to set thee on his throne, [to be] king for the LORD thy God: because thy God loved Israel, to establish them for ever, therefore he made thee king over them, to do judgment and justice.
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
And she gave the king a hundred and twenty talents of gold, and of spices great abundance, and precious stones: neither was there any such spice as the queen of Sheba gave to king Solomon.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
And the servants also of Huram, and the servants of Solomon, who brought gold from Ophir, brought algum trees and precious stones.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
And the king made [of] the algum trees terraces to the house of the LORD, and to the king's palace, and harps and psalteries for singers: and there were none such seen before in the land of Judah.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
And king Solomon gave to the queen of Sheba all her desire, whatever she asked, besides [that] which she had brought to the king. So she turned, and went away to her own land, she and her servants.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Now the weight of gold that came to Solomon in one year was six hundred and sixty and six talents of gold;
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
Besides [that which] chapmen and merchants brought. And all the kings of Arabia and governors of the country brought gold and silver to Solomon.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
And king Solomon made two hundred targets [of] beaten gold: six hundred [shekels] of beaten gold went to one target.
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
And three hundred shields [made he of] beaten gold: three hundred [shekels] of gold went to one shield. And the king put them in the house of the forest of Lebanon.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
Moreover, the king made a great throne of ivory, and overlaid it with pure gold.
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
And [there were] six steps to the throne, with a footstool of gold, [which were] fastened to the throne, and stays on each side of the sitting-place, and two lions standing by the stays:
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
And twelve lions stood there on the one side and on the other upon the six steps. There was not the like made in any kingdom.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
And all the drinking vessels of king Solomon [were of] gold, and all the vessels of the house of the forest of Lebanon [were of] pure gold: none [were of] silver; it was [not] any thing accounted of in the days of Solomon.
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
For the king's ships went to Tarshish with the servants of Huram: once every three years came the ships of Tarshish bringing gold, and silver, ivory, and apes, and peacocks.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
And king Solomon surpassed all the kings of the earth in riches and wisdom.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
And all the kings of the earth sought the presence of Solomon, to hear his wisdom, that God had put in his heart.
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
And they brought every man his present, vessels of silver, and vessels of gold, and raiment, harness, and spices, horses, and mules, a rate year by year.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
And Solomon had four thousand stalls for horses and chariots, and twelve thousand horsemen; whom he bestowed in the chariot cities, and with the king at Jerusalem.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
And he reigned over all the kings from the river even to the land of the Philistines, and to the border of Egypt.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
And the king made silver in Jerusalem as stones, and cedar trees he made as the sycamore trees that [are] in the low plains in abundance.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
And they brought to Solomon horses from Egypt, and from all lands.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
Now the rest of the acts of Solomon, first and last, [are] they not written in the book of Nathan the prophet, and in the prophecy of Ahijah the Shilonite, and in the visions of Iddo the seer against Jeroboam the son of Nebat?
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
And Solomon reigned in Jerusalem over all Israel forty years.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Solomon slept with his fathers, and he was buried in the city of David his father: and Rehoboam his son reigned in his stead.

< 2 Nyakati 9 >