< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
And when the Queene of Sheba heard of the fame of Salomon, she came to proue Salomon with hard questions at Ierusalem, with a very great traine, and camels that bare sweete odours and much golde, and precious stones: and when she came to Salomon, she communed with him of all that was in her heart.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
And Salomon declared her all her questions, and there was nothing hid from Salomon, which he declared not vnto her.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
Then the Queene of Sheba sawe the wisedome of Salomon, and the house that he had buylt,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
And the meate of his table, and the sitting of his seruants, and the order of his wayters, and their apparel, and his butlers, and their apparel, and his burnt offrings which he offred in the house of the Lord, and she was greatly astonied.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
And she saide to the King, It was a true worde which I heard in mine owne lande of thy sayings, and of thy wisedome:
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
Howbeit I beleeued not their report, vntil I came, and mine eyes had seene it: and beholde, the one halfe of thy great wisedom was not told me: for thou exceedest the fame that I heard.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Happie are thy men, and happie are these thy seruants, which stande before thee alway, and heare thy wisedome.
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Blessed be the Lord thy God, which loued thee, to set thee on his throne as King, in the steade of the Lord thy God: because thy God loueth Israel, to establish it for euer, therefore hath he made thee King ouer them, to execute iudgement and iustice.
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
Then she gaue the King sixe score talents of golde, and of sweete odours exceeding much and precious stones: neither was there such sweete odours since, as the Queene of Sheba gaue vnto King Salomon.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
And the seruants also of Huram, and the seruants of Salomon which brought golde from Ophir, brought Algummim wood and precious stones.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
And the King made of the Algummim wood staires in the house of the Lord, and in the Kings house, and harpes and violes for singers: and there was no such seene before in the lande of Iudah.
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
And King Salomon gaue to the Queene of Sheba euery pleasant thing that she asked, besides for that which she had brought vnto the King: so she returned and went to her owne countrey, both she, and her seruants.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
Also the weight of golde that came to Salomon in one yeere, was sixe hundreth three score and sixe talents of golde,
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
Besides that which chapmen and marchants brought: and all the Kings of Arabia, and the princes of the countrey brought golde and siluer to Salomon.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
And King Salomon made two hundreth targets of beaten golde, and sixe hundreth shekels of beaten golde went to one target,
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
And three hundreth shieldes of beaten golde: three hundreth shekels of golde went to one shielde, and the King put them in the house of the wood of Lebanon.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
And the King made a great throne of yuorie and ouerlaid it with pure golde.
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
And the throne had sixe steppes, with a footestoole of gold fastened to the throne, and stayes on either side on the place of the seate, and two lyons standing by the stayes.
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
And twelue lyons stoode there on the sixe steps on either side: there was not the like made in any kingdome.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
And all King Salomons drinking vessels were of golde, and all the vessels of the house of the wood of Lebanon were of pure gold: for siluer was nothing esteemed in ye dayes of Salomon.
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
For the Kings ships went to Tarshish with the seruants of Huram, euery three yeere once came the ships of Tarshish, and brought golde, and siluer, yuorie, and apes, and peacockes.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
So King Salomon excelled all the Kings of the earth in riches and wisedome.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
And all the Kings of the earth sought the presence of Salomon, to heare his wisedome that God had put in his heart.
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
And they brought euery man his present, vessels of siluer, and vessels of golde, and raiment, armour, and sweet odours, horses, and mules, from yeere to yeere.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
And Salomon had foure thousand stalles of horses, and charets, and twelue thousand horsmen, whom he bestowed in the charet cities, and with the King at Ierusalem.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
And he reigned ouer all the Kings from the Riuer euen vnto the land of the Philistims, and to the border of Egypt.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
And the King gaue siluer in Ierusalem, as stones, and gaue cedar trees as the wilde fig trees, that are aboundant in the plaine.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
And they brought vnto Salomon horses out of Egypt, and out of all landes.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
Concerning the rest of the actes of Salomon first and last, are they not written in the booke of Nathan the Prophet, and in the prophecie of Ahiiah the Shilonite, and in the visions of Ieedo the Seer against Ieroboam the sonne of Nebat?
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
And Salomon reigned in Ierusalem ouer all Israel fourtie yeeres.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Salomon slept with his fathers, and they buryed him in the citie of Dauid his father: and Rehoboam his sonne reigned in his steade.

< 2 Nyakati 9 >