< 2 Nyakati 9 >

1 Malkia wa Sheba aliposikia habari za umaarufu wa Solomoni, huyo malkia akaja Yerusalemu kumjaribu kwa maswali magumu. Alifika akiwa na msafara mkubwa sana, pamoja na ngamia waliobeba vikolezi, kiasi kikubwa cha dhahabu na vito vya thamani, alikuja kwa Solomoni na kuzungumza naye kuhusu yote ambayo alikuwa nayo moyoni mwake.
And the queen of Sheba heard of the fame of Solomon, and came to Jerusalem to prove Solomon with enigmas; with a very great train, and camels that bore spices and gold in great abundance, and precious stones; and she came to Solomon, and spoke with him of all that was in her heart.
2 Solomoni akamjibu maswali yake yote, wala hakukuwa na jambo lolote lililokuwa gumu kwake asiweze kumwelezea.
And Solomon explained to her all she spoke of, and there was not a thing hidden from Solomon that he did not explain to her.
3 Malkia wa Sheba alipoona hekima yote ya Solomoni na jumba la kifalme alilokuwa amejenga,
And when the queen of Sheba saw the wisdom of Solomon, and the house that he had built,
4 chakula kilichokuwa mezani pake, jinsi maafisa wake walivyokaa, wahudumu katika majoho yao, wanyweshaji wake na sadaka za kuteketezwa alizotoa katika Hekalu la Bwana alipatwa na mshangao.
and the food of his table, and the deportment of his servants, and the order of service of his attendants and their apparel, and his cupbearers and their apparel, and his ascent by which he went up to the house of Jehovah, there was no more spirit in her.
5 Akamwambia mfalme, “Taarifa niliyosikia kwenye nchi yangu mwenyewe kuhusu mafanikio na hekima yako ni kweli.
And she said to the king, It was a true report that I heard in mine own land of thine affairs and of thy wisdom;
6 Lakini sikuamini yaliyosemwa hadi nilipokuja na kuona kwa macho yangu mwenyewe. Naam, sikuambiwa hata nusu yake; katika hekima na mali umezidi sana kuliko ile taarifa niliyoisikia.
but I gave no credit to their words, until I came and mine eyes had seen; and behold, the half of the greatness of thy wisdom was not told me: thou exceedest the report that I heard.
7 Heri watu wako! Heri hawa maafisa wako wasimamao mbele yako daima na kusikia hekima yako!
Happy are thy men, and happy are these thy servants, who stand continually before thee and hear thy wisdom!
8 Ahimidiwe Bwana Mungu wako, ambaye amependezwa sana nawe, na akakuweka juu ya kiti chake cha ufalme utawale kwa niaba ya Bwana Mungu wako. Kwa sababu ya upendo wa Mungu wako kwa Israeli na shauku yake ya kuwadhibitisha milele, amekufanya wewe mfalme juu yao, ili kudumisha haki na uadilifu.”
Blessed be Jehovah thy God, who delighted in thee, to set thee on his throne, to be king to Jehovah thy God! Because thy God loved Israel, to establish them for ever, therefore did he make thee king over them, to do judgment and justice.
9 Naye akampa mfalme talanta 120 za dhahabu, kiasi kikubwa cha vikolezi na vito vya thamani. Haikuwahi kamwe kuletwa vikolezi vizuri kama vile Malkia wa Sheba alivyompa Mfalme Solomoni.
And she gave the king a hundred and twenty talents of gold, and spices in very great abundance, and precious stones; neither was there any such spice as that which the queen of Sheba gave to king Solomon.
10 (Watumishi wa Hiramu na wa Solomoni wakaleta dhahabu kutoka Ofiri, tena wakaleta shehena kubwa ya miti ya msandali na vito vya thamani.
(And the servants also of Huram, and the servants of Solomon, who brought gold from Ophir, brought sandal-wood and precious stones.
11 Mfalme akatumia hiyo miti ya msandali kuwa ngazi kwa ajili ya Hekalu la Bwana na kwa jumba la kifalme, pia kwa kutengeneza vinubi na zeze kwa ajili ya waimbaji. Kiasi hicho kingi cha msandali hakijawahi kuingizwa Yuda tangu siku ile.)
And the king made of the sandal-wood stairs for the house of Jehovah, and for the king's house, and harps and lutes for the singers. And there were none such seen before in the land of Judah.)
12 Mfalme Solomoni akampa Malkia wa Sheba kila kitu alichotamani na kukiomba, zaidi ya vile alivyokuwa amemletea mfalme. Kisha malkia akaondoka na kurudi katika nchi yake, yeye na watumishi wake.
And king Solomon gave to the queen of Sheba all her desire, whatever she asked, besides what she had brought to the king. And she turned and went to her own land, she and her servants.
13 Uzito wa dhahabu ambayo Solomoni alipokea kwa mwaka ulikuwa talanta 666,
And the weight of gold that came to Solomon in one year was six hundred and sixty-six talents of gold,
14 mbali na mapato yaliyoletwa na wafanyabiashara na wachuuzi. Wafalme wote wa Arabuni na watawala wa nchi wakamletea Solomoni dhahabu na fedha.
besides [what] dealers and merchants brought, and [what] all the kings of Arabia and the governors of the country brought of gold and silver to Solomon.
15 Mfalme Solomoni akatengeneza ngao kubwa 200 kwa dhahabu iliyofuliwa. Kila ngao ilikuwa na dhahabu yenye uzito wa shekeli 600
And king Solomon made two hundred targets of beaten gold, — he applied six hundred [shekels] of beaten gold to one target;
16 Akatengeneza pia ngao ndogo 300 za dhahabu iliyofuliwa, kila ngao ikiwa na uzito wa mane tatu za dhahabu. Mfalme akaziweka katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni.
and three hundred shields of beaten gold, — he applied three hundred [shekels] of gold to one shield; and the king put them in the house of the forest of Lebanon.
17 Kisha mfalme akatengeneza kiti kikubwa cha kifalme kwa kutumia pembe za ndovu na kukifunika kwa dhahabu safi.
And the king made a great throne of ivory, and overlaid it with pure gold;
18 Kiti hicho kilikuwa na ngazi sita na mahali pa kuwekea miguu vyote vya dhahabu. Pande zote za kiti kulikuwa na mahali pa kuegemeza mikono, na simba wawili wakisimama kando ya hiyo mikono.
and the throne had six steps, with a footstool of gold fastened to the throne; and there were arms on each side at the place of the seat, and two lions stood beside the arms;
19 Simba kumi na wawili walisimama kwenye ngazi sita, mmoja katika kila upande wa kila ngazi. Hakuna kitu kama hicho kilichokuwa kimefanyika kwenye ufalme mwingine wowote.
and twelve lions stood there on the one side and on the other upon the six steps: there was not the like made in any kingdom.
20 Vikombe vyote vya Mfalme Solomoni vya kunywea vilikuwa vya dhahabu na vyombo vyote vya nyumbani katika Jumba la Kifalme la Msitu wa Lebanoni vilikuwa vya dhahabu safi. Hakukuwa na kitu kilichotengenezwa kwa fedha, kwa sababu fedha ilionekana ya thamani ndogo wakati wa Solomoni.
And all king Solomon's drinking vessels were of gold, and all the vessels of the house of the forest of Lebanon were of precious gold: silver was not of the least account in the days of Solomon.
21 Mfalme alikuwa na meli nyingi za biashara baharini zilizoendeshwa na watu wa Hiramu. Kwa mara moja kila miaka mitatu zilirudi, zikiwa zimebeba dhahabu, fedha, pembe za ndovu na nyani wakubwa na wadogo.
For the king's ships went to Tarshish with the servants of Huram: once in three years came the ships of Tarshish, bringing gold and silver, ivory, and apes, and peacocks.
22 Mfalme Solomoni alikuwa mkuu zaidi kwa utajiri na hekima kuliko wafalme wote wa dunia.
And king Solomon was greater than all the kings of the earth in riches and wisdom.
23 Wafalme wote wa dunia wakatafuta kukutana na Solomoni ili kusikia hekima ambayo Mungu alikuwa ameiweka katika moyo wake.
And all the kings of the earth sought the presence of Solomon, to hear his wisdom, which God had put in his heart.
24 Mwaka baada ya mwaka, kila mmoja ambaye alikuja, alileta zawadi, vyombo vya fedha na dhahabu, majoho, silaha na vikolezi, farasi na nyumbu.
And they brought every man his present, vessels of silver and vessels of gold, and clothing, armour, and spices, horses and mules, a rate year by year.
25 Solomoni alikuwa na mabanda 4,000 kwa ajili ya farasi na magari ya vita, farasi 12,000 ambao aliwaweka katika miji ya magari ya vita na katika Yerusalemu pamoja naye.
And Solomon had four thousand stalls for horses and chariots, and twelve thousand horsemen; and he placed them in the chariot-cities, and with the king at Jerusalem.
26 Solomoni akatawala juu ya wafalme wote kuanzia Mto Frati mpaka kwenye nchi ya Wafilisti na kuendelea hadi mpaka wa Misri.
And he ruled over all the kings from the river as far as the land of the Philistines, and up to the border of Egypt.
27 Mfalme akafanya fedha kuwa kitu cha kawaida kama mawe huko Yerusalemu, mierezi akaifanya kuwa mingi kama mikuyu vilimani.
And the king made silver in Jerusalem as stones, and cedars made he as the sycamores that are in the lowland for abundance.
28 Farasi wa Solomoni waliletwa kutoka Misri na kutoka nchi nyingine zote.
And they brought to Solomon horses out of Egypt, and out of all lands.
29 Kwa habari za matukio mengine ya utawala wa Solomoni, kuanzia mwanzo hadi mwisho, je, hayakuandikwa katika kumbukumbu za nabii Nathani, katika unabii wa Ahiya Mshiloni na katika maono ya Ido mwonaji kuhusu Yeroboamu mwana wa Nebati?
And the rest of the acts of Solomon first and last, are they not written in the words of Nathan the prophet, and in the prophecy of Ahijah the Shilonite, and in the visions of Iddo the seer concerning Jeroboam the son of Nebat?
30 Solomoni alitawala Israeli yote miaka arobaini, akiwa Yerusalemu.
And Solomon reigned in Jerusalem over all Israel forty years.
31 Kisha Solomoni akalala pamoja na baba zake, naye akazikwa katika mji wa Daudi baba yake. Naye Rehoboamu mwanawe akawa mfalme baada yake.
And Solomon slept with his fathers, and they buried him in the city of David his father; and Rehoboam his son reigned in his stead.

< 2 Nyakati 9 >