< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
Or, vingt ans s’étant accomplis après que Salomon eut bâti la maison du Seigneur et sa propre maison,
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
Il bâtit les villes qu’Hiram lui avait données, et y fit habiter les enfants d’Israël.
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
Il s’en alla aussi à Emath-Suba, et s’en empara.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
Et il bâtit Palmyre dans le désert, et les autres villes très fortifiées, il les bâtit en Emath.
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
Il construisit aussi Béthoron la haute, et Béthoron la basse, villes murées, ayant des portes, des verrous et des serrures;
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
Et de plus Balaath. toutes les villes très fortes qui étaient à Salomon, toutes les villes des quadriges, et les villes de la cavalerie: tout ce que Salomon voulut et décida, il le bâtit, dans Jérusalem, et sur le Liban, et dans tout le pays de sa domination.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
Quant à tout le peuple qui était resté des Héthéens, des Amorrhéens, des Phérézéens, des Hévéens et des Jébuséens, qui n’étaient point de la race d’Israël,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
Mais des enfants et des descendants de ceux que les enfants d’Israël n’avaient point tués, Salomon les rendit dépendants et tributaires jusqu’à ce jour.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Pour les enfants d’Israël, il ne les employa pas à travailler aux ouvrages du roi; car c’étaient des hommes de guerre, les premiers chefs et les commandants de ses quadriges et de sa cavalerie.
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
Or tous les princes de l’armée du roi Salomon étaient au nombre de deux cent cinquante, qui instruisaient le peuple.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Quant à la fille de Pharaon, il la transporta de la cité de David dans la maison qu’il lui avait bâtie; car le roi dit: Ma femme n’habitera pas dans la maison de David, roi d’Israël, parce quelle a été sanctifiée, du moment que l’arche du Seigneur y est entrée.
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Alors Salomon offrit des holocaustes au Seigneur sur l’autel du Seigneur, qu’il avait construit devant le portique,
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
Pour qu’on y offrît chaque jour des sacrifices, selon le commandement de Moïse, aux jours du sabbat, aux calendes, et aux jours de fête, trois fois par an, c’est-à-dire à la solennité des azymes, à la solennité des semaines et à la solennité des tabernacles.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
Et il établit, selon les prescriptions de David, son père, les devoirs des prêtres dans leur ministère, les Lévites dans leur ordre, pour chanter des louanges et servir devant les prêtres, suivant le rite de chaque jour, et les portiers, d’après la distribution qui en avait été faite pour chaque porte; ainsi, en effet, l’avait ordonné David, l’homme de Dieu.
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
Touchant les commandements du roi, ni les prêtres ni les Lévites n’omirent rien de tout ce qu’il avait ordonné, et par rapport à la garde des trésors,
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
Salomon eut toutes les dépenses préparées depuis le jour qu’il jeta les fondements de la maison jusqu’au jour où il l’acheva.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Alors Salomon alla à Asiongaber et à Aïlath, sur le bord de la mer Rouge, qui est dans la terre d’Edom.
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
Or Hiram lui envoya, par l’entremise de ses serviteurs, des vaisseaux et des matelots connaissant la mer, et ils allèrent avec les serviteurs de Salomon à Ophir, et ils emportèrent de là quatre cent cinquante talents d’or, et ils les portèrent au roi Salomon.

< 2 Nyakati 8 >