< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
Le roi Salomon avait mis vingt ans à construire ces deux édifices: le temple du Seigneur et son propre palais.
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
Et il rebâtit les villes qu'Hiram lui avait données, et il y établit des fils d'Israël.
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
Puis, il se rendit à Bésoba, qu'il entoura de remparts.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
Et il bâtit Thœdnior (Palmyre) dans le désert, ainsi que toutes les places fortes du pays d'Emath.
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
Et il fit de Béthoron-la-Haute et de Béthoron-la-Basse deux forteresses, avec murailles, portes et verrous.
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
Et il bâtit Balaath, ainsi que toutes les places fortes qui lui appartenaient, toutes les villes des chars, les villes des cavaliers, enfin tout ce qu'il lui plut de bâtir tant à Jérusalem que dans le Liban, et dans tout son royaume.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
Tout ce qui restait de l'Hettéen, de l'Amorrhéen, de l'Evéen, du Jébuséen; tout ce qui n'était point d'Israël,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
Mais qui descendait de ceux que les fils d'Israël n'avaient point exterminés, et qui étaient restés avec eux en la terre promise, furent obligés de payer à Salomon un tribut qu'ils paient encore de nos jours.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Et Salomon ne permit point qu'il y eût en son royaume de serviteurs nés des fils d'Israël; car ceux-ci étaient des guerriers, des chefs, des vaillants, qui commandaient les chars et les cavaliers.
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
Il y en avait à la tête des intendants du roi Salomon; on en comptait deux cent cinquante dirigeant les travaux du peuple.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Et Salomon conduisit la fille du Pharaon de la ville de David, au palais qu'il avait bâti pour elle, car il avait dit: Ma femme ne doit pas demeurer en la ville de David, roi d'Israël, parce qu'une ville où est entrée l'arche du Seigneur est sainte.
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Alors, Salomon offrit des holocaustes au Seigneur sur l'autel qu'il avait élevé au Seigneur devant le temple,
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
Selon la règle de chaque jour; il les offrit conformément aux commandements de Moïse sur les sabbats, les lunes et les fêtes des trois époques de l'année: fête des azymes, fête des semaines, fête des tabernacles.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
Ensuite, conformément à l'ordre établi par David, son père, il régla les fonctions des prêtres et celles des lévites, qui devaient servir et chanter journellement devant les prêtres; il désigna aussi les portiers; car, ainsi l'avait prescrit David, homme de Dieu.
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
Et on ne s'écarta point des commandements du roi, concernant les prêtres et les lévites, en aucune chose, notamment en ce qui regardait les trésors.
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
Tous les travaux avaient été préparés à partir du jour où Salomon avait jeté les fondations du temple, jusqu'à celui où la construction fut achevée.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Alors, Salomon alla à Asiongaber et à Ailath, en la terre d'Idumée, près du rivage de la mer.
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
Là, Hiram lui envoya des vaisseaux et des serviteurs habitués à la mer; ceux-ci naviguèrent, avec les serviteurs de Salomon, jusqu'à Ophir; ils rapportèrent de là trois cent cinquante talents d'or, et ils revinrent auprès du roi Salomon.

< 2 Nyakati 8 >