< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
Or, au bout des vingt ans employés par Salomon à construire la maison du Seigneur et son propre palais,
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
Salomon fortifia les villes que lui avait cédées Houram, roi de Tyr, et les peupla d’Israélites.
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
Puis, Salomon marcha contre Hamat-Çoba et s’en rendit maître.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
Il bâtit le Tadmor du désert ainsi que toutes les villes d’approvisionnement qu’il éleva dans le pays de Hamat.
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
Il bâtit le Beth-Horôn supérieur et le Beth-Horôn inférieur, villes fortes munies de murailles, de portes et de verrous,
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
de même Baalat et toutes les autres villes d’approvisionnement de Salomon, toutes les villes de chariots, celles des cavaliers, bref, tout ce qu’il plaisait à Salomon de construire à Jérusalem, au Liban et dans tout le pays soumis à sa domination.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
Toute la population survivante des Héthéens, des Amorréens, des Phérézéens, des Hévéens et des Jébuséens, lesquels ne font point partie des enfants d’Israël,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
leurs descendants qui étaient restés après eux dans le pays et que les enfants d’Israël n’avaient pas exterminés, Salomon les obligea à payer tribut; ce qu’ils font encore aujourd’hui.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Pour les enfants d’Israël, Salomon n’en employa point comme esclaves pour ses travaux; ils étaient seulement ses hommes de guerre, ses fonctionnaires, capitaines, commandants de ses chars et de sa cavalerie.
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
Les surveillants en chef du roi Salomon étaient au nombre de deux cent cinquante, chargés de diriger le peuple.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Quant à la fille de Pharaon, Salomon lui fit quitter la Cité de David pour l’installer dans la demeure qu’il lui avait construite, "car, disait-il, je ne dois pas laisser résider une femme dans les demeures de David, roi d’Israël, devenues sacrées depuis que l’arche du Seigneur y a été transférée".
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Dès lors, Salomon offrait des holocaustes au Seigneur, sur l’autel qu’il lui avait élevé devant le portique;
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
en se conformant au rite de chaque jour, il les offrait, selon les prescriptions de Moïse, les jours du Sabbat et des néoménies et aux fêtes qui se suivent trois fois par an, à la fête des Azymes, à la fête des Semaines et à la fête des Tabernacles.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
En vertu de la réglementation de son père David, il installa les sections de prêtres dans leur service et les Lévites dans leurs charges, consistant à réciter les cantiques et à faire le service concurremment avec les prêtres, selon le rite de chaque jour; il posta aussi les portiers par escouades à chacune des portes, comme l’avait ordonné David, l’homme de Dieu.
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
On ne s’écarta en rien des prescriptions du roi David, concernant les prêtres et les Lévites, et notamment les trésors.
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
l’œuvre entière de Salomon fut accomplie à ce jour: la fondation de la maison du Seigneur jusqu’à son achèvement. La maison du Seigneur se trouva complète.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Alors Salomon se rendit à Ecion-Ghéber et à Elot, au bord de la mer dans le pays d’Edom.
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
Houram lui expédia, par ses serviteurs, des vaisseaux et des matelots experts dans la marine, qui se rendirent avec les serviteurs de Salomon à Ophir, d’où ils emportèrent quatre cent cinquante kikkar d’or, qu’ils remirent au roi Salomon.

< 2 Nyakati 8 >