< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
Et au bout de 20 ans, lorsque Salomon eut bâti la maison de l’Éternel et sa propre maison,
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
il arriva que Salomon bâtit aussi les villes que Hiram avait données à Salomon, et y fit habiter les fils d’Israël.
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
Et Salomon alla en Hamath-Tsoba, et l’assujettit.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
Et il bâtit Tadmor dans le désert, et toutes les villes à entrepôts qu’il bâtit en Hamath.
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
Et il bâtit Beth-Horon la haute, et Beth-Horon la basse, villes fortes, avec des murailles, des portes et des barres,
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
et Baalath, et toutes les villes à entrepôts qu’avait Salomon, et toutes les villes pour les chars, et les villes pour la cavalerie, et tout ce que Salomon désira de bâtir à Jérusalem, et au Liban, et dans tout le pays de sa domination.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
– Tout le peuple qui restait des Héthiens, et des Amoréens, et des Phéréziens, et des Héviens, et des Jébusiens, qui n’étaient pas d’Israël,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
– leurs fils qui étaient restés après eux dans le pays [et] que les fils d’Israël n’avaient pas détruits, Salomon les assujettit aux levées, jusqu’à ce jour.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Mais des fils d’Israël, Salomon n’en fit pas des esclaves pour ses travaux; car ils étaient hommes de guerre, et chefs de ses capitaines, et chefs de ses chars et de sa cavalerie.
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
Et c’est ici [le nombre] des chefs des intendants qu’avait le roi Salomon: 250, qui avaient autorité sur le peuple.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Et Salomon fit monter la fille du Pharaon, de la ville de David, dans la maison qu’il avait bâtie pour elle; car il dit: Ma femme n’habitera pas dans la maison de David, roi d’Israël, car les lieux où est entrée l’arche de l’Éternel sont saints.
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Alors Salomon offrit des holocaustes à l’Éternel, sur l’autel de l’Éternel, qu’il avait bâti devant le portique,
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
offrant chaque jour ce qu’il fallait, selon le commandement de Moïse, pour les sabbats, et pour les nouvelles lunes, et pour les jours solennels, trois fois par an, à la fête des pains sans levain, et à la fête des semaines, et à la fête des tabernacles.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
Et il établit, suivant l’ordonnance de David, son père, les classes des sacrificateurs dans leur service, et les lévites dans leurs charges, pour louer et pour faire le service devant les sacrificateurs, selon l’œuvre de chaque jour, et les portiers dans leurs divisions, à chaque porte; car tel avait été le commandement de David, homme de Dieu.
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
Et on ne s’écarta point du commandement du roi pour les sacrificateurs et les lévites, en aucune chose, ni à l’égard des trésors.
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
Ainsi toute l’œuvre de Salomon fut préparée, jusqu’au jour où la maison de l’Éternel fut fondée, et jusqu’à ce qu’elle fut terminée. La maison de l’Éternel fut achevée.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Alors Salomon s’en alla à Étsion-Guéber et à Éloth, sur le bord de la mer, dans le pays d’Édom.
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
Et Hiram lui envoya, par la main de ses serviteurs, des navires et des serviteurs connaissant la mer; et ils allèrent avec les serviteurs de Salomon à Ophir, et y prirent 450 talents d’or, et les apportèrent au roi Salomon.

< 2 Nyakati 8 >