< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
Da de tyve År var omme, i hvilke Salomo havde bygget på HERRENs Hus og sit Palads -
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
også de Byer, Huram afstod til Salomo, befæstede Salomo og lod Israeliterne bosætte sig i dem -
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
drog Salomo til Hamat-Zoba og indtog det.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
Han befæstede også Tadmor i Ørkenen og alle de Forrådsbyer, han byggede i Hamat;
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
ligeledes genopbyggedehan Øvre og Nedre-Bet-Horon, så de blev Fæstninger med Mure, Porte og Portslåer,
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
ligeledes Ba'alat og alle Salomos Forrådsbyer, Vognbyerne og Rytterbyerne, og alt andet, som Salomo fik Lyst til at bygge i Jerusalem, i Libanon og i hele sit Rige.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
Alt, hvad der var tilbage af Hetiterne, Amoriterne, Perizziterne, Hivviterne og Jebusiterne, og som ikke hørte til Israeliterne,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
deres Efterkommere, som var tilbage efter dem i Landet, og som Israeliterne ikke havde tilintetgjort. dem udskrev Salomo til Hoveriarbejde, som det er den Dag i Dag.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Af Israeliterne derimod gjorde Salomo ingen til Arbejdstrælle for sig, men de var Krigsfolk, Hærførere og Vognkæmpere hos ham og Førere for hans Stridsvogne og Rytteri.
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
Tallet på Kong Salomos Overfogeder var 250; de havde Tilsyn med Folkene.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Faraos Datter flyttede Salomo fra Davidsbyen ind i det Hus, han havde bygget til hende; thi han tænkte: "Jeg vil ikke have en Kvinde boende i Kong David af Israels Palads, thi bellige er de Steder, hvor HERRENs Ark kommer."
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Nu ofrede Salomo Brændofre til HERREN på HERRENs Alter, som han Havde bygget foran Forhallen,
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
idet han ofrede, som det efter Moses's Bud hørte sig til hver enkelt Dag, på Sabbaterne, Nymånedagene og Højtiderne tre Gange om Året, de usyrede Brøds Højtid, Ugernes Højtid og Løvhytternes Højtid.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
Og efter den Ordning, hans Fader David havde truffet, satte han Præsternes Skifter til deres Arbejde og Leviterne til deres Tjeneste, til at synge Lovsangen og gå Præsterne til Hånde efter hver Dags Behov, ligeledes Dørvogterne efter deres Skifter til at holde Vagt ved de enkelte Porte; thi således var den Guds Mand Davids Bud.
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
Og man fraveg ikke i mindste Måde Kongens Bud vedrørende Præsterne og Leviterne og Skatkamrene.
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
Således fuldendtes hele Salomos Værk, fra den Dag Grundvolden lagdes til HERRENs Hus, til Salomo var færdig med HERRENs Hus.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Ved den Tid drog Salomo til Ezjongeber og Elot ved Edoms Kyst;
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
og Huram sendte ham Folk med Skibe og befarne Søfolk, der sammen med Salomos Folk sejlede til Ofir, hvor de hentede 450 Talenter Guld, som de bragte Kong Salomo.

< 2 Nyakati 8 >