< 2 Nyakati 8 >

1 Miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Solomoni alilijenga Hekalu la Bwana na jumba lake mwenyewe la kifalme,
A kad je prošlo dvadeset godina, za koliko je vremena Salomon podigao Jahvin Dom i svoj dvor,
2 Solomoni akajenga tena vijiji vile ambavyo Hiramu alikuwa amempa, naye akawapa Waisraeli waishi humo.
posagradio je Salomon gradove, koje je dao Salomonu Hiram, i naselio ondje Izraelove sinove.
3 Kisha Solomoni akaenda Hamath-Soba na kuuteka.
Potom otiđe Salomon na Sopski Hamat i osvoji ga.
4 Pia akajenga mji wa Tadmori katika jangwa na miji yote ya kuhifadhia vitu katika Hamathi.
Sagradi Tadmor u pustinji i svakojaka mjesta za skladišta u Hamatu.
5 Akajenga tena Beth-Horoni ya Juu na Beth-Horoni ya Chini, miji yenye ngome, kuta, malango na makomeo.
Sagradi i Gornji Bet Horon i Donji Bet Horon, tvrde gradove sa zidovima, vratima i prijevornicama;
6 Solomoni pia akajenga Baalathi na miji yake yote ya kuhifadhia vitu, na miji kwa ajili ya magari yake na kwa ajili ya farasi wake, chochote alichotaka kujenga katika Yerusalemu, katika Lebanoni na katika nchi yote aliyotawala.
i Baalat, i sve gradove u kojima je imao skladišta, sve gradove za bojna kola i gradove za konjanike i što je god Salomon zaželio da gradi u Jeruzalemu i na Libanonu i po svoj zemlji svojega kraljevstva.
7 Watu wote waliosalia kutoka kwa Wahiti, Waamori, Waperizi, Wahivi na Wayebusi (haya mataifa hayakuwa Waisraeli),
Svim preostalim Hetitima, Amorejcima, Perižanima, Hivijcima i Jebusejcima, koji nisu bili Izraelci,
8 yaani, wazao wao waliobakia katika nchi, ambao Waisraeli hawakuwa wamewaangamiza: hawa Solomoni akawalazimisha kuwa watumwa katika shokoa, kama ilivyo hadi leo.
sinovima njihovim koji ostadoše iza njih u zemlji i koje Izraelci nisu zatrli - Salomon nametnu tlaku do današnjega dana.
9 Lakini Solomoni hakuwafanya Waisraeli watumwa kwa ajili ya kazi yake, bali walikuwa wapiganaji, majemadari, maafisa wake, majemadari wa magari yake ya vita na waendesha magari ya vita.
Sinove Izraelove nije Salomon pretvarao u robove za posao, nego su bili vojnici, zapovjednici njegovih štitonoša i zapovjednici bojnih kola i konjice.
10 Pia walikuwa maafisa wakuu wa Mfalme Solomoni, yaani, maafisa wakaguzi 250 waliosimamia watu.
Bili su poglavari nad upravnicima, kojih je kralj Salomon imao dvjesta i pedeset, i upravljali su narodom.
11 Solomoni akampandisha mke wake binti Farao kutoka Mji wa Daudi na kumleta jumba la kifalme alilokuwa amemjengea, kwa kuwa alisema, “Mke wangu hataishi katika jumba la kifalme la Daudi mfalme wa Israeli, kwa sababu mahali ambapo Sanduku la Bwana limefika ni patakatifu.”
Salomon preseli i faraonovu kćer iz Davidova grada u kuću koju joj bijaše sagradio, jer je mislio: “Neće moja žena živjeti u dvoru izraelskoga kralja Davida, jer je svet otkako je u nj došao Kovčeg Jahvin.”
12 Mfalme Solomoni akamtolea Bwana dhabihu za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana ambayo alikuwa ameijenga mbele ya ukumbi,
Tada Salomon poče prinositi paljenice Jahvi na Jahvinu žrtveniku što ga bijaše sagradio pred trijemom,
13 kulingana na mahitaji ya kila siku kwa ajili ya sadaka zilizoamriwa na Mose kwa ajili ya Sabato, Mwezi Mwandamo na sikukuu nyingine tatu za mwaka, yaani, Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu, Sikukuu ya Majuma na Sikukuu ya Vibanda.
i to koliko je trebalo iz dana u dan da prinese po Mojsijevoj zapovijedi, u subote, i na mlađake, i na blagdane tri puta u godini, na Blagdan beskvasnih kruhova, i na Blagdan sedmica, i na Blagdan sjenica.
14 Kwa kushika maagizo ya Daudi baba yake, aliweka migawanyo ya makuhani kwa ajili ya kazi zao, nao Walawi kuongoza kusifu na kusaidia makuhani kufuatana na mahitaji ya kila siku. Pia akaweka mabawabu katika migawanyo kwa ajili ya malango mbalimbali, kwa sababu hili ndilo Daudi mtu wa Mungu alilokuwa ameagiza.
Postavio je, po uredbi oca Davida, svećeničke redove po njihovoj službi i levitske po njihovim dužnostima da pjevaju hvale i da služe pred svećenicima, koliko treba iz dana u dan, i vratare po njihovim redovima na svakim vratima, jer je takva bila zapovijed Božjega čovjeka Davida.
15 Nao hawakuziacha amri za mfalme alizoamuru makuhani au Walawi katika jambo lolote, ikiwa ni pamoja na zile za hazina.
Nisu odstupili od kraljeve zapovijedi za svećenike i levite ni u čemu, ni za riznice.
16 Kazi yote ya Mfalme Solomoni ilifanyika kuanzia siku msingi wa Hekalu la Bwana ulipowekwa mpaka kukamilika kwake. Kwa hiyo Hekalu la Bwana likamalizika kujengwa.
Tako se svršio sav Salomonov posao od dana kad je bio zasnovan Dom Jahvin pa dokle ga god nije dovršio. Tako bijaše dovršen Dom Jahvin.
17 Ndipo Solomoni akaenda Esion-Geberi na Elathi katika pwani ya Edomu.
Tada je Salomon otišao u Esjon-Geber i u Elat na morskoj obali u zemlji edomskoj.
18 Naye Hiramu alimpelekea meli zilizoongozwa na maafisa wake mwenyewe, watu waliokuwa na ujuzi wa baharini. Hawa watu pamoja na wale wa Solomoni wakasafiri kwa bahari mpaka Ofiri, wakaleta kutoka huko talanta 450 za dhahabu, ambazo walimkabidhi Mfalme Solomoni.
A Hiram mu je poslao po slugama lađe i mornare vične moru te su otišli sa Salomonovim slugama u Ofir; uzeše odande četiri stotine i pedeset talenata zlata i donesoše ih kralju Salomonu.

< 2 Nyakati 8 >