< 2 Nyakati 7 >

1 Baada ya Solomoni kumaliza kuomba, moto ukashuka kutoka mbinguni na kuteketeza sadaka ya kuteketezwa na dhabihu, nao utukufu wa Bwana ukalijaza Hekalu.
When Solomon finished praying, fire came down from the sky and burned all the offerings and sacrifices [that were on the altar], and the glorious radiance of Yahweh filled the temple.
2 Makuhani hawakuweza kuingia ndani ya Hekalu la Bwana kwa sababu utukufu wa Bwana ulilijaza.
The radiance [was extremely bright], with the result that the priests could not enter the temple of Yahweh.
3 Waisraeli wote walipoona moto ukishuka na utukufu wa Bwana ukiwa juu ya Hekalu, wakapiga magoti sakafuni wakasujudu nyuso zao mpaka chini, nao wakamwabudu na kumshukuru Bwana wakisema, “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.”
When all the Israeli people [who were there] saw the fire coming down and the glory of Yahweh above the temple, they prostrated themselves with their faces touching the ground. They worshiped and thanked Yahweh, singing, “Yahweh is always good to us; he faithfully loves us forever.”
4 Ndipo mfalme na watu wote wakatoa dhabihu mbele za Bwana Mungu.
Then the king and all the people who were there dedicated the temple to Yahweh by offering more sacrifices to him. King Solomon gave 22,000 cattle and 120,000 sheep and goats to be sacrificed.
5 Naye Mfalme Solomoni akatoa dhabihu ya ngʼombe 22,000 pamoja na kondoo na mbuzi 120,000. Hivyo ndivyo mfalme na watu wote walivyoweka wakfu Hekalu la Mungu.
6 Makuhani wakasimama kwenye nafasi zao, vivyo hivyo Walawi wakiwa na vyombo vya uimbaji vya Bwana ambavyo Mfalme Daudi alikuwa ametengeneza kwa ajili ya kumsifu Bwana, navyo vilitumika wakati aliposhukuru, akisema, “Upendo wake wadumu milele.” Mkabala na Walawi, makuhani walipiga tarumbeta zao, nao Waisraeli wote walikuwa wamesimama.
The priests stood in their positions, and the other descendants of Levi stood in their positions holding the musical instruments [to praise] Yahweh, instruments that King David had caused to be made for praising Yahweh and thanking him. [They sang], “He faithfully loves us forever.” Facing the other descendants of Levi the priests stood, blowing their trumpets, while all the Israeli people were standing [and listening].
7 Solomoni akaweka wakfu sehemu ya katikati ya ua uliokuwa mbele ya Hekalu la Bwana na hapo akatoa sadaka za kuteketezwa na mafuta ya sadaka za amani, kwa sababu madhabahu ya shaba aliyokuwa ametengeneza haikutosha kuweka sadaka hizo zote za kuteketezwa, sadaka za nafaka na za mafuta.
Solomon dedicated the middle part of the courtyard in front of the temple. Then he gave offerings to be completely burned there along with the fat of the animals to be sacrificed to maintain fellowship with Yahweh. The priests burned them there in the courtyard because in addition to those things there were offerings of grain, with the result that there was not enough space on the bronze altar to burn all those sacrifices.
8 Hivyo Solomoni akaiadhimisha sikukuu wakati ule kwa muda wa siku saba, na Israeli wote pamoja naye. Walikuwa kusanyiko kubwa sana, watu kutoka Lebo-Hamathi hadi Kijito cha Misri.
Solomon [and the other people] celebrated the Festival of Living in Temporary Shelters for seven days. There was a huge group of people who celebrated with him. Some of them came from [as far away as] Lebo-Hamath [in the far north] and the border of Egypt [in the far south].
9 Katika siku ya nane walifanya kusanyiko, kwa kuwa walikuwa wanaadhimisha kuwekwa wakfu kwa madhabahu kwa muda wa siku saba na sikukuu kwa muda wa siku nyingine saba zaidi.
On the eighth/next day they gathered again [to worship Yahweh]. They had celebrated the dedication of the altar for seven days and the Festival of Living in Temporary Shelters for seven days.
10 Katika siku ya ishirini na tatu ya mwezi wa saba Solomoni akawaaga watu waende nyumbani mwao, wakishangilia na kufurahi mioyoni mwao, kwa wema mwingi Bwana Mungu aliomtendea Daudi na Solomoni na kwa ajili ya watu wake Israeli.
Then on the next day Solomon sent them to their homes. They were very joyful because of all the good things that Yahweh had done for David and Solomon and for all his Israeli people.
11 Solomoni alipomaliza kujenga Hekalu la Bwana na jumba la kifalme, naye akiwa amefanikiwa kutenda yale yote aliyokuwa nayo moyoni mwake kufanya katika Hekalu la Bwana na katika jumba lake mwenyewe la kifalme,
Solomon’s [workers] finished building the temple and Solomon’s palace. And Solomon finished doing everything else that he had planned to do.
12 Bwana akamtokea Solomoni usiku na kumwambia: “Nimesikia maombi yako nami nimechagua mahali hapa kwa ajili yangu mwenyewe kuwa Hekalu kwa ajili ya dhabihu.
Then Yahweh appeared to him one night [in a dream] and said to him, “I have heard your prayer, and I have chosen this temple to be the place where my people will offer sacrifices to me.
13 “Wakati nitakapofunga mbingu ili isiwepo mvua, au nikiamuru nzige kula mazao ya nchi au nikituma tauni miongoni mwa watu wangu,
“When I prevent any rain from falling, or when I command locusts to eat all the crops, or when I send a plague among my people,
14 kama watu wangu, wanaoitwa kwa Jina langu, watajinyenyekesha na kuomba na kuutafuta uso wangu na kuacha njia zao mbaya, basi nitasikia toka mbinguni na kuwasamehe dhambi yao na nitaiponya nchi yao.
if the people who belong to me humble themselves and pray, and request me to help them, and if they turn away from their sinful behavior, then I will hear from heaven. I will forgive them for having sinned and I will cause them to prosper again.
15 Sasa macho yangu yatafumbuka na masikio yangu yatasikiliza kwa makini maombi yaombwayo mahali hapa.
I [SYN] will see them and I [SYN] will hear them when they pray to me in this place.
16 Kwa maana sasa nimechagua na kutakasa Hekalu hili ili kwamba Jina langu lipate kuwa huko milele. Macho yangu na moyo wangu utakuwepo huko daima.
I have chosen and have (set apart/dedicated) this temple in order that people may worship [MTY] me there forever. I will always watch over [MTY] it and protect [IDM] it.
17 “Kwa habari yako wewe, kama ukienenda mbele zangu kama Daudi baba yako alivyoenenda na kufanya yote nikuamuruyo, nawe ukizishika amri zangu na sheria zangu,
“And as for you, if you obey me as David your father did, and if you do all that I command you to do, and obey all my laws and decrees,
18 Nitakiimarisha kiti chako cha enzi kama nilivyoagana na Daudi baba yako niliposema, ‘Hutakosa kamwe mtu wa kutawala juu ya Israeli.’
I will make sure that your descendants will always be kings, which is what I promised to David your father, saying, ‘Some of your descendants will always be the kings of Israel.’
19 “Lakini kama ukigeuka na kuyaacha maagizo na amri nilizowapa na kwenda kuitumikia miungu mingine na kuiabudu,
“But if you Israelis turn away from me and disobey the decrees and commands that I have given to you, and you start to worship other gods,
20 ndipo nitakapoingʼoa Israeli kutoka nchi yangu niliyowapa, nami nitalikataa Hekalu hili nililolitakasa kwa ajili ya Jina langu. Nitalifanya kitu cha kudharauliwa na kitu cha kudhihakiwa miongoni mwa watu wote.
I will cause you to be expelled from this land that I have given to you, and I will abandon this temple that I have set apart to be the place where people should worship me. I will cause it to be despised and ridiculed by people of all nations.
21 Ingawa Hekalu hili linavutia sana sasa, wote watakaolipita watashangaa na kusema, ‘Kwa nini Bwana amefanya kitu kama hiki katika nchi hii na kwa Hekalu hili?’
Although this temple is now greatly respected, when that happens, all the people who pass by will be appalled, and they will say, ‘Why has Yahweh done terrible things like this to this country and to this temple?’
22 Watu watajibu, ‘Ni kwa sababu wamemwacha Bwana, Mungu wa baba zao, aliyewatoa Misri, nao wamekumbatia miungu mingine, wakaiabudu na kuitumikia, ndiyo sababu ameyaleta maafa haya yote juu yao.’”
And others will reply, ‘It happened because they rejected Yahweh, the God to whom their ancestors belonged, the one who brought their ancestors out of Egypt, and they have been worshiping other gods and trying to please them. And that is why Yahweh has caused them to experience all these disasters.’”

< 2 Nyakati 7 >