< 2 Nyakati 6 >

1 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene.
Alors Salomon dit: L'Éternel a dit qu'il habiterait dans l'obscurité.
2 Nimejenga Hekalu zuri kwa ajili yako, mahali pako pa kukaa milele.”
Et moi, j'ai bâti une maison pour ta demeure, et un domicile afin que tu y habites à toujours!
3 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
Puis le roi tourna son visage, et bénit toute l'assemblée d'Israël; et toute l'assemblée d'Israël était debout.
4 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mikono yake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
Et il dit: Béni soit l'Éternel, le Dieu d'Israël, qui de sa bouche a parlé à David, mon père, et qui, de sa main, a accompli ce qu'il avait promis en disant:
5 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, wala sikumchagua mtu yeyote kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli.
Depuis le jour où j'ai fait sortir mon peuple du pays d'Égypte, je n'ai point choisi de ville entre toutes les tribus d'Israël pour y bâtir une maison, afin que mon nom y fût, et je n'ai point choisi d'homme pour être chef de mon peuple d'Israël.
6 Lakini sasa nimeuchagua Yerusalemu ili Jina langu lipate kuwamo humo, na nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
Mais j'ai choisi Jérusalem pour que mon nom y fût, et j'ai choisi David pour qu'il régnât sur mon peuple d'Israël.
7 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Or David, mon père, avait dessein de bâtir une maison au nom de l'Éternel, le Dieu d'Israël.
8 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
Mais l'Éternel dit à David, mon père: Puisque tu as eu le dessein de bâtir une maison à mon nom, tu as bien fait de former ce dessein.
9 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea Hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Seulement ce n'est pas toi qui bâtiras cette maison; mais c'est ton fils, issu de toi, qui bâtira cette maison à mon nom.
10 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
L'Éternel a donc accompli la parole qu'il avait prononcée; j'ai succédé à David, mon père, et je me suis assis sur le trône d'Israël, comme l'Éternel l'avait dit, et j'ai bâti cette maison au nom de l'Éternel, le Dieu d'Israël.
11 Nimeliweka humo Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na watu wa Israeli.”
Et j'y ai mis l'arche, où est l'alliance de l'Éternel, qu'il a traitée avec les enfants d'Israël.
12 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, naye akakunjua mikono yake.
Puis il se plaça devant l'autel de l'Éternel, en face de toute l'assemblée d'Israël, et il étendit ses mains.
13 Basi Solomoni alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano na kimo chake dhiraa tatu, naye akaliweka katikati ya ukumbi wa nje. Akapanda juu ya hilo jukwaa kisha akapiga magoti mbele ya kusanyiko lote la Israeli, akanyoosha mikono yake kwelekea mbinguni.
Car Salomon avait fait une tribune d'airain, et il l'avait mise au milieu du grand parvis; elle était longue de cinq coudées, large de cinq coudées, et haute de trois coudées; il s'y plaça, se mit à genoux, en face de toute l'assemblée d'Israël, et, étendant ses mains vers les cieux, il dit:
14 Akasema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
O Éternel, Dieu d'Israël! ni dans les cieux, ni sur la terre, il n'y a de Dieu semblable à toi, qui gardes l'alliance et la miséricorde envers tes serviteurs qui marchent de tout leur cœur devant ta face;
15 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
Toi qui as tenu à ton serviteur David, mon père, ce que tu lui avais promis; et ce que tu as prononcé de ta bouche, tu l'as accompli de ta main, comme il paraît aujourd'hui.
16 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
Maintenant donc, ô Éternel, Dieu d'Israël! tiens à ton serviteur David, mon père, ce que tu lui as promis en disant: Tu ne manqueras jamais devant moi d'un successeur assis sur le trône d'Israël; pourvu que tes fils prennent garde à leur voie, pour marcher dans ma loi, comme tu as marché devant ma face.
17 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
Et maintenant, ô Éternel, Dieu d'Israël! que ta parole, que tu as prononcée à David, ton serviteur, soit ratifiée!
18 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani na wanadamu? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
Mais serait-il vrai que Dieu habitât sur la terre avec les hommes? Voici, les cieux, même les cieux des cieux, ne peuvent te contenir, combien moins cette maison que j'ai bâtie?
19 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
Toutefois, ô Éternel, mon Dieu! aie égard à la prière de ton serviteur et à sa supplication, pour écouter le cri et la prière que ton serviteur t'adresse.
20 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
Que tes yeux soient ouverts, jour et nuit, sur cette maison, sur le lieu où tu as promis de mettre ton nom, exauçant la prière que ton serviteur te fait en ce lieu.
21 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
Exauce les supplications de ton serviteur et de ton peuple d'Israël, quand ils prieront en ce lieu; exauce-les des cieux, du lieu de ta demeure; exauce et pardonne!
22 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
Quand quelqu'un aura péché contre son prochain, et qu'on lui déférera le serment pour le faire jurer, et qu'il viendra prêter serment devant ton autel, dans cette maison;
23 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimwadhibu yule mwenye hatia kwa kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
Toi, écoute des cieux, agis et juge tes serviteurs, en donnant au méchant son salaire, et faisant retomber sa conduite sur sa tête; en justifiant le juste, et lui rendant selon sa justice.
24 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
Quand ton peuple d'Israël aura été battu par l'ennemi, pour avoir péché contre toi; s'ils retournent à toi, s'ils donnent gloire à ton nom, s'ils t'adressent dans cette maison des prières et des supplications;
25 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
Toi, exauce-les des cieux, et pardonne le péché de ton peuple d'Israël, et ramène-les dans la terre que tu as donnée à eux et à leurs pères.
26 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
Quand les cieux seront fermés, et qu'il n'y aura point de pluie, parce qu'ils auront péché contre toi; s'ils prient en ce lieu, s'ils donnent gloire à ton nom, et s'ils se détournent de leurs péchés, parce que tu les auras affligés;
27 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
Toi, exauce-les des cieux, et pardonne le péché de tes serviteurs et de ton peuple d'Israël, après que tu leur auras enseigné le bon chemin, par lequel ils doivent marcher; et envoie de la pluie sur la terre que tu as donnée en héritage à ton peuple.
28 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
Quand il y aura dans le pays la famine ou la peste, quand il y aura la rouille, la nielle, les sauterelles ou les chenilles, quand les ennemis les assiégeront dans leur pays, dans leurs portes, ou qu'il y aura une plaie, une maladie quelconque;
29 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu zake na uchungu wake, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili,
Quelque prière, quelque supplication que fasse quelque homme que ce soit de tout ton peuple d'Israël, selon qu'ils auront reconnu chacun sa plaie et sa douleur, et que chacun aura étendu ses mains vers cette maison;
30 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
Toi, exauce-les des cieux, du lieu de ta demeure, et pardonne; rends à chacun selon toutes ses voies, toi qui connais son cœur; car seul tu connais le cœur des enfants des hommes;
31 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
Afin qu'ils te craignent, pour marcher dans tes voies, tout le temps qu'ils vivront sur la terre que tu as donnée à nos pères.
32 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu na mkono wako wenye nguvu ulionyooshwa, atakapokuja kuomba kuelekea Hekalu hili,
Et l'étranger lui-même, qui ne sera pas de ton peuple d'Israël, mais qui viendra d'un pays éloigné, à cause de ton grand nom, de ta main forte, et de ton bras étendu; quand il viendra prier dans cette maison,
33 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
Toi, exauce-le des cieux, du lieu de ta demeure, et fais tout ce que cet étranger réclamera de toi; afin que tous les peuples de la terre connaissent ton nom, qu'ils te craignent comme ton peuple d'Israël, et sachent que ton nom est invoqué sur cette maison que j'ai bâtie.
34 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
Quand ton peuple sortira en guerre contre ses ennemis, par le chemin où tu l'auras envoyé; s'ils te prient, en regardant vers cette ville que tu as choisie, et vers cette maison que j'ai bâtie à ton nom,
35 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
Exauce des cieux leur prière et leur supplication, et fais-leur droit.
36 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi iliyo mbali au karibu
Quand ils auront péché contre toi (car il n'y a point d'homme qui ne pèche), et que, irrité contre eux, tu les auras livrés à leurs ennemis, et que ceux qui les auront pris les auront emmenés captifs en quelque pays, soit au loin, soit au près;
37 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya utumwa na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa na tumetenda uovu’;
Si, dans le pays où ils seront captifs, ils rentrent en eux-mêmes, et que, se repentant, ils prient dans le pays de leur captivité, en disant: Nous avons péché, nous avons commis l'iniquité, nous avons agi méchamment!
38 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
S'ils retournent à toi de tout leur cœur et de toute leur âme, dans le pays de leur captivité où on les aura emmenés captifs, et s'ils t'adressent leurs prières, en regardant vers leur pays, que tu as donné à leurs pères, vers cette ville que tu as choisie, et vers cette maison que j'ai bâtie à ton nom;
39 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako.
Exauce des cieux, du lieu de ta demeure, leurs prières et leurs supplications, et fais-leur droit; pardonne à ton peuple qui aura péché contre toi.
40 “Sasa, Mungu wangu, macho yako na yafumbuke na masikio yako yasikie maombi yaombwayo mahali hapa.
Maintenant, ô mon Dieu! que tes yeux soient ouverts et que tes oreilles soient attentives à la prière faite en ce lieu!
41 “Sasa inuka, Ee Bwana Mungu,
Et maintenant, Éternel Dieu! lève-toi, viens au lieu de ton repos, toi et l'arche de ta force. Éternel Dieu, que tes sacrificateurs soient revêtus de salut, et que tes bien-aimés se réjouissent de leur bonheur!
42 Ee Bwana Mungu, usimkatae
Éternel Dieu, ne repousse pas ton oint; souviens-toi des grâces accordées à David, ton serviteur.

< 2 Nyakati 6 >