< 2 Nyakati 6 >

1 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene.
Thanne Salomon seide, The Lord bihiyte, that he wolde dwelle in derknesse;
2 Nimejenga Hekalu zuri kwa ajili yako, mahali pako pa kukaa milele.”
forsothe I haue bilde an hows to his name, that he schulde dwelle there with outen ende.
3 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
And Salomon turnede his face, and blesside al the multitude of Israel; for al the cumpeny stood ententif; and he seide,
4 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mikono yake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
Blessid be the Lord God of Israel, for he fillide in werk that thing, that he spak to Dauid, my fadir, and seide,
5 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, wala sikumchagua mtu yeyote kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli.
Fro the dai in which Y ledde my puple out of the lond of Egipt, Y chees not a citee of alle the lynagis of Israel, that an hows schulde be bildid therynne to my name, nether Y chees ony other man, that he schulde be duyk on my puple Israel;
6 Lakini sasa nimeuchagua Yerusalemu ili Jina langu lipate kuwamo humo, na nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
but Y chees Jerusalem, that my name be therynne, and Y chees Dauid, to ordeyne hym on my puple Israel.
7 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
And whanne it was of the wille of Dauid, my fadir, to bilde an hows to the name of the Lord God of Israel,
8 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
the Lord seide to hym, For this was thi wille, `that thou woldist bilde an hows to my name, sotheli thou didist wel,
9 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea Hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
hauynge suche a wil, but thou schalt not bilde an hows to me; netheles the sone, that schal go out of thi leendis, he schal bilde an hows to my name.
10 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Therfor the Lord hath fillid his word, which he spak; and Y roos for Dauid, my fader, and Y sat on the trone of Israel, as the Lord spak, and Y bildide an hous to the name of the Lord God of Israel;
11 Nimeliweka humo Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na watu wa Israeli.”
and I haue put therynne the arke, in which is the couenaunt of the Lord, which he `couenauntide with the sones of Israel.
12 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, naye akakunjua mikono yake.
Therfor Salomon stood bifor the auter of the Lord euene ayens al the multitude of Israel, and stretchide forth his hondis.
13 Basi Solomoni alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano na kimo chake dhiraa tatu, naye akaliweka katikati ya ukumbi wa nje. Akapanda juu ya hilo jukwaa kisha akapiga magoti mbele ya kusanyiko lote la Israeli, akanyoosha mikono yake kwelekea mbinguni.
For Salomon hadde maad a brasun foundement, and hadde set it in the myddis of the greet hows, and it hadde fyue cubitis of lengthe, and fyue of breede, and thre cubitis of heiythe, and he stood theron; and fro that tyme he knelide ayens al the multitude of Israel, and reiside the hondis in to heuene,
14 Akasema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
and seide, Lord God of Israel, noon is lijk thee; `thou art God in heuene and in erthe, which kepist couenaunt and mercy with thi seruauntis, that goon bifor thee in al her herte;
15 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
which hast youe to Dauid thi seruaunt, my fadir, what euer thingis thou hast spoke to hym, and thow hast fillid in werk tho thingis, whiche thou bihiytist bi mouth, as also present tyme preueth.
16 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
Now therfor, Lord God of Israel, fille thou to thi seruaunt my fadir Dauid, what euer thingis thou hast spoke, seiynge, A man of thee schal not faile bifor me, that schal sitte on the trone of Israel; so netheles if thi sones kepen my weies, and goon in my lawe, as and thou hast go bifor me.
17 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
And now, Lord God of Israel, thi word be maad stidefast, which thou spakist to thi seruaunt Dauid.
18 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani na wanadamu? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
Therfor whether it is leueful, that the Lord dwelle with men on erthe? If heuene and the heuenes of heuenes `taken not thee, how myche more this hows, which Y haue bildid?
19 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
But herto oneli it is maad, that thou, my Lord God, biholde the preier of thi seruaunt, and the bisechyng of hym, and that thou here the preieris, whiche thi seruaunt schedith bifor thee;
20 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
that thou opyne thin iyen on this hows bi dayes and nyytis, on the place in which thou bihiytist, that thi name schulde be clepid,
21 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
and that thou woldist here the preier, which thi seruaunt preieth therynne. Here thou the preieris of thi seruaunt, and of thi puple Israel; who euer preieth in this place, here thou fro thi dwellyng place, that is, fro heuenes, and do thou merci.
22 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
If ony man synneth ayens his neiybore, and cometh redi to swere ayens him, and byndith hym silf with cursyng bifor the auter in this hows,
23 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimwadhibu yule mwenye hatia kwa kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
thou schalt here fro heuene, and schalt do the doom of thi seruauntis; so that thou yelde to the wickid man his weie in to his owne heed, and that thou venge the iust man, and yelde to hym after his riytfulnesse.
24 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
If thi puple Israel is ouercomen of enemyes, for thei schulen do synne ayens thee, and if thei conuertid doen penaunce, and bisechen thi name, and preien in this place,
25 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
thou schalt here fro heuene, and do thou mercy to the synne of thi puple Israel, and brynge hem ayen `in to the lond, which thou hast youe to hem, and to `the fadris of hem.
26 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
If whanne heuene is closid, reyn come not doun for the synne of thi puple, and thei bisechen thee in this place, and knowlechen to thi name, and ben turned fro her synnes, whanne thou hast turmentid hem,
27 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
here thou, Lord, fro heuene, and foryyue thou synnes to thi seruauntis, and to thi puple Israel, and teche thou hem a good weie, bi which thei schulen entre, and yyue thou reyn to the lond, which thou hast youe to thi puple to haue in possessioun.
28 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
If hungur risith in the lond, and pestilence, and rust, and wynd distriynge cornes, and a locuste, and bruke cometh, and if enemyes bisegen the yatis of the citee, aftir that the cuntreis ben distried, and al veniaunce and sikenesse oppressith;
29 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu zake na uchungu wake, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili,
if ony of thi puple Israel bisechith, and knowith his veniaunce and sikenesse, and if he spredith abrood hise hondis in this hows,
30 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
thou schalt here fro heuene, that is, fro thin hiye dwellyng place, and do thou mercy, and yelde thou to ech man aftir hise weies, whiche thou knowist, that he hath in his herte; for thou aloone knowist the hertis of the sones of men;
31 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
that thei drede thee, and go in thi weies in alle daies, in which thei lyuen on the face of erthe, which thou hast youe to oure fadris.
32 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu na mkono wako wenye nguvu ulionyooshwa, atakapokuja kuomba kuelekea Hekalu hili,
Also thou schalt here fro heuene, thi moost stidfast dwellyng place, a straunger, which is not of thi puple Israel, if he cometh fro a fer lond for thi greet name, and for thi stronge hond, and arm holdun forth, `and preye in this place;
33 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
and thou schalt do alle thingis, for which thilke pilgrym `inwardli clepith thee, that alle the puplis of erthe knowe thi name, and drede thee, as thi puple Israel doith; and that thei knowe, that thi name is clepid on this hows, which Y haue bildid to thi name.
34 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
If thi puple goith out to batel ayens hise aduersaries, bi the weie in which thou sendist hem, thei schulen worschipe thee ayens the weie in which this citee is, which thou hast chose, and the hows which Y bildide to thi name,
35 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
that thou here fro heuene her preieris and bisechyng, and do veniaunce.
36 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi iliyo mbali au karibu
Forsothe if thei synnen ayens thee, for no man is that synneth not, and if thou art wrooth to hem, and bitakist hem to enemyes; and enemyes leden hem prisoneris in to a fer lond, ether certis which lond is nyy;
37 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya utumwa na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa na tumetenda uovu’;
and if thei ben conuertid in her herte in the lond, to which thei ben led prisoneris, and thei don penaunce, and bisechen thee in the lond of her caitifte, and seien, We han synned, we han do wickidly, we diden vniustli;
38 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
and if thei turnen ayen to thee in al her herte, and in al her soule, in the lond of her caitifte, to which thei ben led, thei schulen worschipe thee ayens the weie of her lond, which thou hast youe to the fadris of hem, and of the citee which thou hast chose, and of the hows which Y bildide to thi name; that thou here fro heuene,
39 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako.
that is, fro thi stidefast dwellyng place, the preieris of hem, and that thou make dom, and foryyue to thi puple, thouy `it be synful; for thou art my God;
40 “Sasa, Mungu wangu, macho yako na yafumbuke na masikio yako yasikie maombi yaombwayo mahali hapa.
Y biseche, be thin iyen openyd, and thin eeris be ententif to the preier which is maad in this place.
41 “Sasa inuka, Ee Bwana Mungu,
Now therfor, Lord God, rise in to thi reste, thou and the arke of thi strengthe; Lord God, thi preestis be clothid with helthe, and thi hooli men be glad in goodis.
42 Ee Bwana Mungu, usimkatae
Lord God, turne thou not a weie the face of thi crist; haue thou mynde on the mercyes of Dauid thi seruaunt.

< 2 Nyakati 6 >