< 2 Nyakati 6 >
1 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene.
then to say Solomon LORD to say to/for to dwell in/on/with cloud
2 Nimejenga Hekalu zuri kwa ajili yako, mahali pako pa kukaa milele.”
and I to build house: home elevation to/for you and foundation to/for to dwell you forever: enduring
3 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
and to turn: turn [the] king [obj] face his and to bless [obj] all assembly Israel and all assembly Israel to stand: stand
4 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mikono yake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
and to say to bless LORD God Israel which to speak: promise in/on/with lip his with David father my and in/on/with hand: power his to fill to/for to say
5 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, wala sikumchagua mtu yeyote kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli.
from [the] day which to come out: send [obj] people my from land: country/planet Egypt not to choose in/on/with city from all tribe Israel to/for to build house: home to/for to be name my there and not to choose in/on/with man to/for to be leader upon people my Israel
6 Lakini sasa nimeuchagua Yerusalemu ili Jina langu lipate kuwamo humo, na nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
and to choose in/on/with Jerusalem to/for to be name my there and to choose in/on/with David to/for to be upon people my Israel
7 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
and to be with heart David father my to/for to build house: home to/for name LORD God Israel
8 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
and to say LORD to(wards) David father my because which to be with heart your to/for to build house: home to/for name my be pleasing for to be with heart your
9 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea Hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
except you(m. s.) not to build [the] house: home for son: child your [the] to come out: produce from loin your he/she/it to build [the] house: home to/for name my
10 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
and to arise: establish LORD [obj] word: promised his which to speak: promise and to arise: establish underneath: instead David father my and to dwell upon throne Israel like/as as which to speak: promise LORD and to build [the] house: home to/for name LORD God Israel
11 Nimeliweka humo Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na watu wa Israeli.”
and to set: make there [obj] [the] ark which there covenant LORD which to cut: make(covenant) with son: descendant/people Israel
12 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, naye akakunjua mikono yake.
and to stand: stand to/for face: before altar LORD before all assembly Israel and to spread palm his
13 Basi Solomoni alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano na kimo chake dhiraa tatu, naye akaliweka katikati ya ukumbi wa nje. Akapanda juu ya hilo jukwaa kisha akapiga magoti mbele ya kusanyiko lote la Israeli, akanyoosha mikono yake kwelekea mbinguni.
for to make Solomon basin bronze and to give: put him in/on/with midst [the] enclosure five cubit length his and five cubit width his and cubit three height his and to stand: stand upon him and to bless upon knee his before all assembly Israel and to spread palm his [the] heaven [to]
14 Akasema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
and to say LORD God Israel nothing like you God in/on/with heaven and in/on/with land: country/planet to keep: obey [the] covenant and [the] kindness to/for servant/slave your [the] to go: walk to/for face: before your in/on/with all heart their
15 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
which to keep: obey to/for servant/slave your David father my [obj] which to speak: promise to/for him and to speak: speak in/on/with lip your and in/on/with hand: power your to fill like/as day: today [the] this
16 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
and now LORD God Israel to keep: guard to/for servant/slave your David father my [obj] which to speak: promise to/for him to/for to say not to cut: lack to/for you man from to/for face: before my to dwell upon throne Israel except if to keep: careful son: descendant/people your [obj] way: conduct their to/for to go: walk in/on/with instruction my like/as as which to go: walk to/for face: before my
17 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
and now LORD God Israel be faithful word your which to speak: speak to/for servant/slave your to/for David
18 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani na wanadamu? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
for truly to dwell God with [the] man upon [the] land: country/planet behold heaven and heaven [the] heaven not to sustain you also for [the] house: home [the] this which to build
19 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
and to turn to(wards) prayer servant/slave your and to(wards) supplication his LORD God my to/for to hear: hear to(wards) [the] cry and to(wards) [the] prayer which servant/slave your to pray to/for face: before your
20 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
to/for to be eye your to open to(wards) [the] house: home [the] this by day and night to(wards) [the] place which to say to/for to set: make name your there to/for to hear: hear to(wards) [the] prayer which to pray servant/slave your to(wards) [the] place [the] this
21 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
and to hear: hear to(wards) supplication servant/slave your and people your Israel which to pray to(wards) [the] place [the] this and you(m. s.) to hear: hear from place to dwell you from [the] heaven and to hear: hear and to forgive
22 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
if to sin man: anyone to/for neighbor his and to lift: raise in/on/with him oath to/for oath his and to come (in): come to swear to/for face: before altar your in/on/with house: home [the] this
23 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimwadhibu yule mwenye hatia kwa kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
and you(m. s.) to hear: hear from [the] heaven and to make: do and to judge [obj] servant/slave your to/for to return: pay to/for wicked to/for to give: give way: conduct his in/on/with head his and to/for to justify righteous to/for to give: give to/for him like/as righteousness his
24 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
and if to strike people your Israel to/for face: before enemy for to sin to/for you and to return: repent and to give thanks [obj] name your and to pray and be gracious to/for face: before your in/on/with house: home [the] this
25 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
and you(m. s.) to hear: hear from [the] heaven and to forgive to/for sin people your Israel and to return: return them to(wards) [the] land: soil which to give: give to/for them and to/for father their
26 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
in/on/with to restrain [the] heaven and not to be rain for to sin to/for you and to pray to(wards) [the] place [the] this and to give thanks [obj] name your from sin their to return: repent [emph?] for to afflict them
27 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
and you(m. s.) to hear: hear [the] heaven and to forgive to/for sin servant/slave your and people your Israel for to show them to(wards) [the] way: conduct [the] pleasant which to go: walk in/on/with her and to give: give rain upon land: country/planet your which to give: give to/for people your to/for inheritance
28 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
famine for to be in/on/with land: country/planet pestilence for to be blight and mildew locust and locust for to be for to confine to/for him enemy his in/on/with land: country/planet gate his all plague and all sickness
29 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu zake na uchungu wake, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili,
all prayer all supplication which to be to/for all [the] man and to/for all people your Israel which to know man: anyone plague his and pain his and to spread palm his to(wards) [the] house: home [the] this
30 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
and you(m. s.) to hear: hear from [the] heaven foundation to dwell you and to forgive and to give: give to/for man like/as all way: conduct his which to know [obj] heart his for you(m. s.) to/for alone you to know [obj] heart son: child [the] man
31 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
because to fear you to/for to go: walk in/on/with way: conduct your all [the] day which they(masc.) alive upon face: surface [the] land: soil which to give: give to/for father our
32 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu na mkono wako wenye nguvu ulionyooshwa, atakapokuja kuomba kuelekea Hekalu hili,
and also to(wards) [the] foreign which not from people your Israel he/she/it and to come (in): come from land: country/planet distant because name your [the] great: large and hand: power your [the] strong and arm your [the] to stretch and to come (in): come and to pray to(wards) [the] house: home [the] this
33 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
and you(m. s.) to hear: hear from [the] heaven from foundation to dwell you and to make: do like/as all which to call: call to to(wards) you [the] foreign because to know all people [the] land: country/planet [obj] name your and to/for to fear: revere [obj] you like/as people your Israel and to/for to know for name your to call: call by upon [the] house: home [the] this which to build
34 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
for to come out: come people your to/for battle upon enemy his in/on/with way: direction which to send: depart them and to pray to(wards) you way: direction [the] city [the] this which to choose in/on/with her and [the] house: home which to build to/for name your
35 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
and to hear: hear from [the] heaven [obj] prayer their and [obj] supplication their and to make: do justice their
36 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi iliyo mbali au karibu
for to sin to/for you for nothing man which not to sin and be angry in/on/with them and to give: give them to/for face: before enemy and to take captive them to take captive them to(wards) land: country/planet distant or near
37 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya utumwa na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa na tumetenda uovu’;
and to return: recall to(wards) heart their in/on/with land: country/planet which to take captive there and to return: repent and be gracious to(wards) you in/on/with land: country/planet captivity their to/for to say to sin to pervert and be wicked
38 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
and to return: repent to(wards) you in/on/with all heart their and in/on/with all soul their in/on/with land: country/planet captivity their which to take captive [obj] them and to pray way: direction land: country/planet their which to give: give to/for father their and [the] city which to choose and to/for house: home which to build to/for name your
39 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako.
and to hear: hear from [the] heaven from foundation to dwell you [obj] prayer their and [obj] supplication their and to make: do justice their and to forgive to/for people your which to sin to/for you
40 “Sasa, Mungu wangu, macho yako na yafumbuke na masikio yako yasikie maombi yaombwayo mahali hapa.
now God my to be please eye your to open and ear your attentive to/for prayer [the] place [the] this
41 “Sasa inuka, Ee Bwana Mungu,
and now to arise: rise [emph?] LORD God to/for rest your you(m. s.) and ark strength your priest your LORD God to clothe deliverance: salvation and pious your to rejoice in/on/with good
42 Ee Bwana Mungu, usimkatae
LORD God not to return: turn back face anointed your to remember [emph?] to/for kindness David servant/slave your