< 2 Nyakati 6 >

1 Ndipo Solomoni akasema, “Bwana alisema kwamba ataishi katika giza nene.
Then Solomon spoke, Jehovah has said that he would dwell in the thick darkness.
2 Nimejenga Hekalu zuri kwa ajili yako, mahali pako pa kukaa milele.”
But I have built for thee a house of habitation, and a place for thee to dwell in forever.
3 Kusanyiko lote la Israeli lilipokuwa limesimama hapo, mfalme akageuka na kuwabariki.
And the king turned his face, and blessed all the assembly of Israel. And all the assembly of Israel stood.
4 Kisha akasema: “Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, ambaye kwa mikono yake mwenyewe ametimiza lile alilomwahidi Daudi baba yangu kwa kinywa chake mwenyewe. Kwa kuwa alisema,
And he said, Blessed be Jehovah, the God of Israel, who spoke with his mouth to David my father, and has with his hands fulfilled it, saying,
5 ‘Tangu siku niliyowatoa watu wangu kutoka Misri, sikuchagua mji katika kabila lolote la Israeli ili Hekalu lijengwe humo ili Jina langu lipate kuwamo humo, wala sikumchagua mtu yeyote kuwa kiongozi wa watu wangu Israeli.
Since the day that I brought forth my people out of the land of Egypt, I chose no city out of all the tribes of Israel to build a house in that my name might be there. Neither did I choose any man to be ruler over my people Israel.
6 Lakini sasa nimeuchagua Yerusalemu ili Jina langu lipate kuwamo humo, na nimemchagua Daudi kuwatawala watu wangu Israeli.’
But I have chosen Jerusalem that my name might be there. And have chosen David to be over my people Israel.
7 “Ilikuwa moyoni mwa Daudi baba yangu kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
Now it was in the heart of David my father to build a house for the name of Jehovah, the God of Israel.
8 Lakini Bwana akamwambia Daudi baba yangu, ‘Kwa sababu ilikuwa moyoni mwako kujenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu, ulifanya vyema kuwa na jambo hili moyoni mwako.
But Jehovah said to David my father, Whereas it was in thy heart to build a house for my name, thou did well that it was in thy heart.
9 Hata hivyo, sio wewe utakayenijengea Hekalu, bali mwanao, ambaye ni nyama yako na damu yako mwenyewe, yeye ndiye atakayejenga Hekalu kwa ajili ya Jina langu.’
Nevertheless thou shall not build the house, but thy son who shall come forth out of thy loins, he shall build the house for my name.
10 “Bwana ametimiza ahadi aliyoiweka: Nimeingia mahali pa Daudi baba yangu na sasa ninakikalia kiti cha ufalme cha Israeli, kama vile Bwana alivyoahidi, nami nimejenga Hekalu kwa ajili ya Jina la Bwana, Mungu wa Israeli.
And Jehovah has performed his word that he spoke. For I have risen up in the place of David my father, and sit on the throne of Israel, as Jehovah promised, and have built the house for the name of Jehovah, the God of Israel.
11 Nimeliweka humo Sanduku la Agano, ambamo ndani yake kuna lile Agano la Bwana alilofanya na watu wa Israeli.”
And there I have set the ark in which is the covenant of Jehovah, which he made with the sons of Israel.
12 Kisha Solomoni akasimama mbele ya madhabahu ya Bwana machoni pa kusanyiko lote la Israeli, naye akakunjua mikono yake.
And he stood before the altar of Jehovah in the presence of all the assembly of Israel, and spread forth his hands.
13 Basi Solomoni alikuwa ametengeneza jukwaa la shaba, urefu wake dhiraa tano, na upana wake dhiraa tano na kimo chake dhiraa tatu, naye akaliweka katikati ya ukumbi wa nje. Akapanda juu ya hilo jukwaa kisha akapiga magoti mbele ya kusanyiko lote la Israeli, akanyoosha mikono yake kwelekea mbinguni.
For Solomon had made a brazen scaffold, five cubits long, and five cubits broad, and three cubits high, and had set it in the midst of the court. And upon it he stood, and knelt down upon his knees before all the assembly of Israel, and spread forth his hands toward heaven.
14 Akasema: “Ee Bwana, Mungu wa Israeli, hakuna Mungu kama wewe juu mbinguni wala chini duniani, wewe unayetunza Agano lako la upendo na watumishi wanaodumu katika njia yako kwa moyo wote.
And he said, O Jehovah, the God of Israel, there is no God like thee, in heaven, or on earth, who keep covenant and loving kindness with thy servants, who walk before thee with all their heart,
15 Umetimiza ahadi yako kwa mtumishi wako Daudi baba yangu, kwa kinywa chako uliahidi na kwa mkono wako umetimiza, kama ilivyo leo.
who have kept with thy servant David my father that which thou promised him. Yea, thou spoke with thy mouth, and have fulfilled it with thy hand, as it is this day.
16 “Sasa Bwana, Mungu wa Israeli, mtimizie mtumishi wako Daudi baba yangu ahadi zako ulizomwahidi uliposema, ‘Kamwe hutakosa kuwa na mtu atakayeketi mbele zangu kwenye kiti cha ufalme cha Israeli, kama wanao wakiangalia yote wayafanyayo kuenenda mbele zangu kama vile ulivyofanya.’
Now therefore, O Jehovah, the God of Israel, keep with thy servant David my father that which thou have promised him, saying, There shall not fail thee a man in my sight to sit on the throne of Israel, if only thy sons take heed to their way, to walk in my law as thou have walked before me.
17 Sasa, Ee Bwana, Mungu wa Israeli, acha neno lako lile ulilomwahidi mtumishi wako Daudi baba yangu litimie.
Now therefore, O Jehovah, the God of Israel, let thy word be verified, which thou spoke to thy servant David.
18 “Lakini kweli, je, Mungu atafanya makao duniani na wanadamu? Mbingu, hata mbingu zilizo juu sana, haziwezi kukutosha wewe. Sembuse Hekalu hili nililojenga!
But will God in very deed dwell with men on the earth? Behold, heaven and the heaven of heavens cannot contain thee. How much less this house which I have built!
19 Hata hivyo sikiliza dua ya mtumishi wako na maombi yake kwa huruma, Ee Bwana Mungu wangu. Sikia kilio na dua ambayo mtumishi wako anaomba mbele zako siku hii ya leo.
Yet have thou respect to the prayer of thy servant, and to his supplication, O Jehovah my God, to hearken to the cry and to the prayer which thy servant prays before thee,
20 Macho yako na yafumbuke kuelekea Hekalu hili usiku na mchana, mahali hapa ambapo ulisema, ‘Jina langu litakuwako humo,’ ili kwamba upate kusikia maombi ambayo mtumishi wako ataomba kuelekea mahali hapa.
that thine eyes may be open toward this house day and night, even toward the place of which thou have said that thou would put thy name there, to hearken to the prayer which thy servant shall pray toward this place.
21 Usikie maombi ya mtumishi wako na ya watu wako Israeli wakati wanapoomba kuelekea mahali hapa. Sikia kutoka mbinguni, mahali pa makao yako na usikiapo, samehe.
And hearken thou to the supplications of thy servant, and of thy people Israel, when they shall pray toward this place. Yea, hear thou from thy dwelling-place, even from heaven, and when thou hear forgive.
22 “Mtu anapomkosea jirani yake na akatakiwa kuapa, akija na kuapa mbele ya madhabahu yako ndani ya Hekalu hili,
If a man sins against his neighbor, and an oath be laid upon him to cause him to swear, and he comes and swears before thine altar in this house,
23 basi, sikia kutoka mbinguni na ukatende. Hukumu kati ya watumishi wako, ukimwadhibu yule mwenye hatia kwa kuleta juu ya kichwa chake yale aliyoyatenda. Umtangazie mwenye haki kwamba hana hatia, hivyo ukathibitishe kuwa haki kwake.
then hear thou from heaven, and do, and judge thy servants, requiting the wicked, to bring his way upon his own head, and justifying the righteous, to give him according to his righteousness.
24 “Wakati watu wako Israeli watakapokuwa wameshindwa na adui kwa sababu ya dhambi walizofanya dhidi yako, watakapokugeukia na kulikiri jina lako, wakiomba na kufanya dua kwako katika Hekalu hili,
And if thy people Israel be smitten down before the enemy because they have sinned against thee, and shall turn again and confess thy name, and pray and make supplication before thee in this house,
25 basi usikie kutoka mbinguni, ukasamehe dhambi ya watu wako Israeli na kuwarudisha katika nchi uliyowapa baba zao.
then hear thou from heaven, and forgive the sin of thy people Israel, and bring them again to the land which thou gave to them and to their fathers.
26 “Wakati mbingu zitakapokuwa zimefungwa kusiwe na mvua kwa sababu watu wako wametenda dhambi dhidi yako, watakapoomba kuelekea mahali hapa na kulikiri jina lako nao wakageuka kutoka dhambi zao kwa sababu umewaadhibu,
When the heavens are shut up, and there is no rain, because they have sinned against thee, if they pray toward this place, and confess thy name, and turn from their sin when thou do afflict them,
27 basi usikie kutoka mbinguni na usamehe dhambi ya watumishi wako, watu wako Israeli. Wafundishe njia sahihi ya kuishi na ukanyeshe mvua juu ya nchi uliyowapa watu wako kuwa urithi.
then hear thou in heaven, and forgive the sin of thy servants, and of thy people Israel, when thou teach them the good way wherein they should walk, and send rain upon thy land, which thou have given to thy people for an inheritance.
28 “Wakati njaa au tauni vikija juu ya nchi, au koga au kawa, nzige au panzi, au wakati adui atakapowazingira katika mji wao wowote, maafa ya namna yoyote au ugonjwa wowote unaoweza kuwajia,
If there be in the land famine, if there be pestilence, if there be blight or mildew, locust or caterpillar, if their enemies besiege them in the land of their cities, whatever plague or whatever sickness there be,
29 wakati dua au maombi yatakapofanywa na mmojawapo wa watu wako Israeli, kila mmoja akitambua taabu zake na uchungu wake, naye akainyoosha mikono yake kuelekea Hekalu hili,
whatever prayer and supplication be made by any man, or by all thy people Israel, who shall know every man his own plague and his own sorrow, and shall spread forth his hands toward this house,
30 basi usikie kutoka mbinguni, katika makao yako. Usamehe na utende, umpe kila mtu kulingana na matendo yake, kwa kuwa unaujua moyo wake (kwa kuwa ni wewe peke yako ujuaye mioyo ya watu wote),
then hear thou from heaven thy dwelling-place and forgive, and render to every man according to all his ways, whose heart thou know, (for thou, even thou only, know the hearts of the sons of men),
31 ili wakuogope kwa wakati wote watakaoishi katika nchi uliyowapa baba zetu.
that they may fear thee, to walk in thy ways so long as they live in the land which thou gave to our fathers.
32 “Kwa habari ya mgeni ambaye si miongoni mwa watu wako Israeli, lakini amekuja kutoka nchi ya mbali kwa sababu ya jina lako kuu na mkono wako wenye nguvu ulionyooshwa, atakapokuja kuomba kuelekea Hekalu hili,
Moreover concerning the foreigner, who is not of thy people Israel, when he shall come from a far country for thy great name's sake, and thy mighty hand, and thine outstretched arm, when they shall come and pray toward this house,
33 basi na usikie kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, ukafanye lolote ambalo mgeni huyo anakuomba, ili mataifa yote ya dunia wapate kujua jina lako na wakuogope kama wafanyavyo watu wako Israeli nao wapate pia kujua kwamba nyumba hii niliyoijenga imeitwa kwa Jina lako.
then hear thou from heaven, even from thy dwelling-place, and do according to all that the foreigner calls to thee for, that all the peoples of the earth may know thy name, and fear thee, as do thy people Israel, and that they may know that this house which I have built is called by thy name.
34 “Wakati watu wako watakapokwenda vitani dhidi ya adui zao, popote utakapowapeleka, wakati watakapoomba kwa Bwana kuelekea mji ambao umeuchagua, na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
If thy people go out to battle against their enemies, by whatever way thou shall send them, and they pray to thee toward this city which thou have chosen, and the house which I have built for thy name,
35 basi usikie dua na maombi yao kutoka mbinguni, ukawatetee haki yao.
then hear thou from heaven their prayer and their supplication, and maintain their cause.
36 “Watakapotenda dhambi dhidi yako, kwa kuwa hakuna mtu yeyote ambaye hatendi dhambi, nawe ukachukizwa nao na kuwakabidhi kwa adui, ambaye atawachukua utumwani katika nchi iliyo mbali au karibu
If they sin against thee (for there is no man that sins not), and thou be angry with them, and deliver them to the enemy, so that they carry them away captive to a land far off or near,
37 na kama watabadilika mioyo yao katika nchi wanakoshikiliwa mateka, nao wakatubu na kukulilia katika nchi ya utumwa na kusema, ‘Tumetenda dhambi, tumefanya makosa na tumetenda uovu’;
yet if they shall rethink themselves in the land where they are carried captive, and turn again, and make supplication to thee in the land of their captivity, saying, We have sinned, we have done perversely, and have dealt wickedly,
38 kama wakikugeukia kwa moyo wao wote na nafsi zao katika nchi ya adui zao ambao waliwachukua mateka, wakakuomba kuelekea nchi uliyowapa baba zao, kuelekea mji uliouchagua na Hekalu nililolijenga kwa ajili ya Jina lako,
if they return to thee with all their heart and with all their soul in the land of their captivity where they have carried them captive, and pray toward their land, which thou gave to their fathers, and the city which thou have chosen, and toward the house which I have built for thy name,
39 basi kutoka mbinguni, mahali pa makao yako, usikie dua yao na maombi yao na kuitetea haki yao. Uwasamehe watu wako, waliotenda dhambi dhidi yako.
then hear thou from heaven, even from thy dwelling-place, their prayer and their supplications, and maintain their case, and forgive thy people who have sinned against thee.
40 “Sasa, Mungu wangu, macho yako na yafumbuke na masikio yako yasikie maombi yaombwayo mahali hapa.
Now, O my God, let, I beseech thee, thine eyes be open, and let thine ears be attendant to the prayer that is made in this place.
41 “Sasa inuka, Ee Bwana Mungu,
Now therefore arise, O Jehovah God, into thy resting-place, thou, and the ark of thy strength. Let thy priests, O Jehovah God, be clothed with salvation, and let thy sanctified rejoice in goodness.
42 Ee Bwana Mungu, usimkatae
O Jehovah God, do not turn away the face of thine anointed. Remember thy loving kindnesses to David thy servant.

< 2 Nyakati 6 >