< 2 Nyakati 5 >

1 Hivyo Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani, fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Mungu.
Ke Tokosra Solomon el aksafyela orekma nukewa ke Tempul, el filiya ma nukewa ma David, papa tumal, el tuh kisakunla nu sin LEUM GOD (silver, gold, ac ma pac saya) tuh in oan in nien filma in Tempul.
2 Kisha Solomoni akawaita huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Na Tokosra Solomon el pangon mwet kol nukewa lun sruf ac sou lulap lun Israel tuh elos in tukeni nu Jerusalem, tuh elos in us Tuptup in Wuleang lun LEUM GOD liki Zion, Siti sel David, nu in Tempul.
3 Nao wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme wakati wa sikukuu mwezi wa saba.
Elos nukewa fahsreni ke pacl in Kufwen lwen Aktuktuk.
4 Wazee wote wa Israeli walipofika, Walawi wakajitwika Sanduku la Agano,
Ke pacl se mwet kol nukewa fahsreni, na mwet Levi elos srukak Tuptup in Wuleang,
5 nao wakalipandisha Sanduku na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani, waliokuwa Walawi, walivibeba vitu hivyo,
ac us nu ke Tempul. Mwet tol ac mwet Levi elos oayapa moklela Lohm Nuknuk Mutal sin LEUM GOD ac ma nukewa kac, nu ke Tempul uh.
6 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
Tokosra Solomon ac mwet Israel nukewa elos toeni sisken na Tuptup in Wuleang, ac elos kisakin sheep ac cow na pukanten su kofla in oaoala.
7 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
Na mwet tol elos us Tuptup in Wuleang lun LEUM GOD nu in Tempul, ac likiya in Acn Mutal Na Mutal, ye cherub luo.
8 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kufunika Sanduku na mipiko yake ya kubebea.
Posohksok lalos asrosrla ac afinya Tuptup sac oayapa sak usyen Tuptup sac.
9 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilizojitokeza kutoka kwenye Sanduku, nazo zilionekana ukiwa mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
Pukun sak inge ku in liyeyuk mwet se fin tu suwohs nu kac ke mutun Acn Mutal Na Mutal, tuh tia ku in liyeyuk ke kutena acn saya. (Sak inge srakna oasr we nwe misenge.)
10 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
Wangin kutena ma in Tuptup in Wuleang sac sayen eot sim luo ma Moses el tuh filiya loac Fineol Sinai, ke LEUM GOD El tuh orala wuleang yurin mwet Israel ke elos tuku liki acn Egypt.
11 Basi makuhani wakaondoka hapo Mahali Patakatifu. Makuhani wote waliokuwa huko walikuwa wamejiweka wakfu, bila kujali migawanyo yao.
Ke mwet tol elos illa liki acn mutal uh (mwet tol nukewa su oasr in acn sac elos tuh akmutalyalos sifacna, mansis u se su lalos,
12 Walawi wote waliokuwa waimbaji, yaani, Asafu, Hemani, Yeduthuni, wana wa ndugu zao, walisimama upande wa mashariki wa madhabahu, wakiwa wamevaa kitani safi huku wakipiga matoazi, vinubi na zeze. Walikuwa pamoja na makuhani 120 wakipiga tarumbeta.
ac mwet on nukewa lun mwet Levi — Asaph, Heman, Jeduthun, ac wen natulos ac sou lalos — los nukewa nukum nuknuk linen. Mwet Levi elos tu apkuran nu ke layen kutulap in loang sac, wi cymbal ac harp natulos, ac oayapa wi mwet tol siofok longoul su uk mwe ukuk.)
13 Wapiga tarumbeta na waimbaji wakaungana katika sauti linganifu, ikawa kama vile ni sauti moja, wakimsifu na kumshukuru Bwana, nao alipoinua sauti zao pamoja na tarumbeta na matoazi na vyombo vingine vya uimbaji, wakamsifu Bwana wakisema: “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.” Ndipo Hekalu la Bwana likajazwa na wingu,
Mwet on elos tukeni ke pusra sifanna in kaksakin ac sang kulo nu sin LEUM GOD. Ac ke pusren on uh ngisyak, wi pusren mwe ukuk ac cymbal ac kutu pac kain in mwe on, elos on ac fahk: “Kaksakin LEUM GOD mweyen El wo, Ac lungse lal oan ma pahtpat,” na lohm sac, lohm sin LEUM GOD, sessesla ke sie pukunyeng.
14 nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu la Mungu.
Ouinge mwet tol elos koflana tafwela alu lalos ke sripen pukunyeng sac, tuh wolana lun LEUM GOD nwakla in lohm sac.

< 2 Nyakati 5 >