< 2 Nyakati 5 >

1 Hivyo Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani, fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Mungu.
Salomon donc apporta tout ce qu’avait voué David, son père, l’argent, l’or et tous les vases, et il les mit dans les trésors de la maison de Dieu.
2 Kisha Solomoni akawaita huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Après quoi, il assembla les anciens d’Israël, tous les princes des tribus et les chefs des familles des enfants d’Israël à Jérusalem, pour amener l’arche de l’alliance du Seigneur de la cité de David, qui est Sion.
3 Nao wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme wakati wa sikukuu mwezi wa saba.
C’est pourquoi tous les hommes d’Israël vinrent auprès du roi au jour solennel du septième mois.
4 Wazee wote wa Israeli walipofika, Walawi wakajitwika Sanduku la Agano,
Et lorsque tous les anciens d’Israël furent venus, les Lévites enlevèrent l’arche,
5 nao wakalipandisha Sanduku na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani, waliokuwa Walawi, walivibeba vitu hivyo,
Et l’apportèrent avec tous les ornements du tabernacle. Mais les vases du sanctuaire, qui étaient dans le tabernacle, ce furent les prêtres qui les portèrent avec les Lévites.
6 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
Or le roi Salomon, tout le peuple d’Israël, et tous ceux qui s’assemblèrent devant l’arche, immolaient des béliers et des bœufs sans nombre: tant était grande, en effet, la multitude des victimes.
7 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
Les prêtres portèrent donc l’arche de l’alliance du Seigneur en son lieu, c’est-à-dire, dans l’oracle du temple, dans le Saint des saints, sous les ailes des chérubins;
8 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kufunika Sanduku na mipiko yake ya kubebea.
En sorte que les chérubins étendaient leurs ailes sur le lieu dans lequel l’arche avait été mise, et la couvraient elle-même avec ses leviers.
9 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilizojitokeza kutoka kwenye Sanduku, nazo zilionekana ukiwa mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
Quant aux leviers avec lesquels on portait l’arche, parce qu’ils étaient un peu plus longs, leurs têtes paraissaient devant le sanctuaire; mais si quelqu’un était un peu en dehors, il ne pouvait pas les voir. Ainsi l’arche a été là jusqu’au présent jour.
10 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
Il n’y avait rien dans l’arche, si ce n’est les deux tables que Moïse y mit à Horeb, quand le Seigneur donna sa loi aux enfants d’Israël sortant d’Égypte.
11 Basi makuhani wakaondoka hapo Mahali Patakatifu. Makuhani wote waliokuwa huko walikuwa wamejiweka wakfu, bila kujali migawanyo yao.
Or les prêtres étaient sortis du sanctuaire (car tous les prêtres qui purent se trouver là furent sanctifiés; et en ce temps-là les classes et l’ordre des ministères n’avaient pas été encore distribués entre eux),
12 Walawi wote waliokuwa waimbaji, yaani, Asafu, Hemani, Yeduthuni, wana wa ndugu zao, walisimama upande wa mashariki wa madhabahu, wakiwa wamevaa kitani safi huku wakipiga matoazi, vinubi na zeze. Walikuwa pamoja na makuhani 120 wakipiga tarumbeta.
Tant les Lévites que les chantres, c’est-à-dire ceux qui étaient sous Asaph, sous Héman, sous Idithun, leurs fils et leurs frères, revêtus de fin lin, faisaient retentir des cymbales, des psaltérions et des harpes, se tenant au côté oriental de l’autel; et avec eux cent vingt prêtres sonnaient des trompettes.
13 Wapiga tarumbeta na waimbaji wakaungana katika sauti linganifu, ikawa kama vile ni sauti moja, wakimsifu na kumshukuru Bwana, nao alipoinua sauti zao pamoja na tarumbeta na matoazi na vyombo vingine vya uimbaji, wakamsifu Bwana wakisema: “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.” Ndipo Hekalu la Bwana likajazwa na wingu,
Ainsi tous ensemble chantant avec des trompettes, des voix, des cymbales, des orgues et d’autres instruments de divers genres, et élevant la voix dans les airs, un bruit s’entendait au loin, en sorte que, lorsqu’ils eurent commencé à louer le Seigneur, et à dire: Rendez gloire au Seigneur, parce qu’il est bon, parce que sa miséricorde est éternelle, la maison de Dieu fut remplie d’une nuée;
14 nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu la Mungu.
En sorte que les prêtres ne pouvaient s’y tenir, ni remplir leur ministère à cause de la nuée; car la gloire du Seigneur avait rempli la maison de Dieu.

< 2 Nyakati 5 >