< 2 Nyakati 5 >

1 Hivyo Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani, fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Mungu.
Da hele Arbejdet, som Salomo lod udføre ved HERRENS Hus, var færdigt, bragte Salomo sin Fader Davids Helliggaver, Sølvet og Guldet, derind og lagde alle Tingene i Skatkamrene i Guds Hus.
2 Kisha Solomoni akawaita huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Derpaa kaldte Salomo Israels Ældste og alle Stammernes Overhoveder, Israeliternes Fædrenehuses Øverster, sammen i Jerusalem for at føre HERRENS Pagts Ark op fra Davidsbyen, det er Zion.
3 Nao wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme wakati wa sikukuu mwezi wa saba.
Saa samledes alle Israels Mænd hos Kongen paa Højtiden i Etanim Maaned, det er den syvende Maaned.
4 Wazee wote wa Israeli walipofika, Walawi wakajitwika Sanduku la Agano,
Og alle Israels Ældste kom, og Leviterne har Arken.
5 nao wakalipandisha Sanduku na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani, waliokuwa Walawi, walivibeba vitu hivyo,
Og de bragte Arken op tillige med Aabenbaringsteltet og alle de hellige Ting, der var i Teltet; Præsterne og Leviterne bragte dem op:
6 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
Og Kong Salomo tillige med hele Israels Menighed, som havde givet Møde hos ham foran Arken, ofrede Smaakvæg og Hornkvæg, saa meget, at det ikke var til at tælle eller overse.
7 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
Saa førte Præsterne HERRENS Pagts Ark ind paa dens Plads i Templets Inderhal, det Allerhelligste, og stillede den under Kerubernes Vinger;
8 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kufunika Sanduku na mipiko yake ya kubebea.
og Keruberne udbredte deres Vinger over Pladsen, hvor Arken stod, og saaledes dannede Keruberne et Dække over Arken og dens Bærestænger.
9 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilizojitokeza kutoka kwenye Sanduku, nazo zilionekana ukiwa mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
Stængerne var saa lange, at Enderne af dem kunde ses fra det Hellige foran Inderhallen, men de kunde ikke ses længere ude; og de er der den Dag i Dag.
10 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
Der var ikke andet i Arken end de to Tavler, Moses havde lagt ned i den paa Horeb, Tavlerne med den Pagt, HERREN havde sluttet med Israeliterne, da de drog bort fra Ægypten.
11 Basi makuhani wakaondoka hapo Mahali Patakatifu. Makuhani wote waliokuwa huko walikuwa wamejiweka wakfu, bila kujali migawanyo yao.
Da Præsterne derpaa gik ud af Helligdommen — alle de Præster, der var til Stede, havde nemlig helliget sig uden Hensyn til Skifterne;
12 Walawi wote waliokuwa waimbaji, yaani, Asafu, Hemani, Yeduthuni, wana wa ndugu zao, walisimama upande wa mashariki wa madhabahu, wakiwa wamevaa kitani safi huku wakipiga matoazi, vinubi na zeze. Walikuwa pamoja na makuhani 120 wakipiga tarumbeta.
og alle de levitiske Sangere, Asaf, Heman og Jedutun tillige med deres Sønner og Brødre stod østen for Alteret i Klæder af fint Linned med Cymbler, Harper og Citre, og sammen med dem stod 120 Præster, der blæste i Trompeter —
13 Wapiga tarumbeta na waimbaji wakaungana katika sauti linganifu, ikawa kama vile ni sauti moja, wakimsifu na kumshukuru Bwana, nao alipoinua sauti zao pamoja na tarumbeta na matoazi na vyombo vingine vya uimbaji, wakamsifu Bwana wakisema: “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.” Ndipo Hekalu la Bwana likajazwa na wingu,
i samme Øjeblik som Trompetblæserne og Sangerne paa een Gang stemte i for at love og prise HERREN og lod Trompeterne, Cymblerne og Musikinstrumenterne klinge og lovede HERREN med Ordene »thi han er god, og hans Miskundhed varer evindelig!« — fyldte Skyen HERRENS Hus,
14 nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu la Mungu.
saa at Præsterne af Skyen hindredes i at staa og udføre deres Tjeneste, thi HERRENS Herlighed fyldte Guds Hus.

< 2 Nyakati 5 >