< 2 Nyakati 5 >

1 Hivyo Solomoni alipomaliza kazi ya Hekalu la Bwana, akaviingiza ndani vile vitu ambavyo Daudi baba yake alikuwa ameviweka wakfu: yaani, fedha, dhahabu na samani; kisha akaviweka katika hazina za Hekalu la Mungu.
Saa blev alt Arbejdet færdigt, som Salomo lod gøre til Herrens Hus; og Salomo førte det ind, som David, hans Fader, havde helliget, og Sølvet og Guldet og alle Redskaberne lagde han i Guds Hus's Skatkammer.
2 Kisha Solomoni akawaita huko Yerusalemu wazee wa Israeli, viongozi wote wa makabila na wakuu wa jamaa za Waisraeli, ili walilete Sanduku la Agano la Bwana kutoka Sayuni, Mji wa Daudi.
Da samlede Salomo til Jerusalem de Ældste i Israel og alle Stammernes Øverster, Fyrster for Fædrenehusene iblandt Israels Børn, for at føre Herrens Pagts Ark op fra Davids Stad, det er Zion.
3 Nao wanaume wote wa Israeli wakakusanyika kwa mfalme wakati wa sikukuu mwezi wa saba.
Og alle Israels Mænd samledes til Kongen paa Højtiden, det er, i den syvende Maaned.
4 Wazee wote wa Israeli walipofika, Walawi wakajitwika Sanduku la Agano,
Og alle Israels Ældste kom, og Leviterne bare Arken.
5 nao wakalipandisha Sanduku na Hema la Kukutania pamoja na vyombo vyote vitakatifu vilivyokuwa ndani yake. Makuhani, waliokuwa Walawi, walivibeba vitu hivyo,
Og de førte Arken op tillige med Forsamlingens Paulun og alle de hellige Redskaber, som vare i Paulunet; Præsterne, Leviterne, førte dem op.
6 naye Mfalme Solomoni na kusanyiko lote la Israeli waliokusanyika kumzunguka walikuwa mbele ya hilo Sanduku, nao wakatoa dhabihu nyingi za kondoo na ngʼombe ambao idadi yao haikuwezekana kuandikwa au kuhesabiwa.
Men Kong Salomo og al Israels Menighed, de, som vare samlede om ham foran Arken, ofrede smaat Kvæg og stort Kvæg, som ikke kunde tælles eller regnes for Mangfoldighed.
7 Makuhani wakalileta Sanduku la Agano la Bwana hadi mahali pake ndani ya sehemu takatifu ndani ya Hekalu, yaani Patakatifu pa Patakatifu, na kuliweka chini ya mabawa ya makerubi.
Saa førte Præsterne Herrens Pagts Ark til dens Sted, ind i Koret udi Huset i det Allerhelligste, hen under Kerubernes Vinger.
8 Makerubi yalitandaza mabawa yao juu ya mahali pa Sanduku la Agano na kufunika Sanduku na mipiko yake ya kubebea.
Og Keruberne udbredte Vingerne over Arkens Sted, og Keruberne dækkede over Arken og over dens Stænger oventil.
9 Mipiko hiyo ilikuwa mirefu sana kiasi kwamba ncha zake zilizojitokeza kutoka kwenye Sanduku, nazo zilionekana ukiwa mbele ya Patakatifu pa Patakatifu, lakini sio nje ya Mahali Patakatifu. Hiyo mipiko ipo hata leo.
Og man drog Stængerne langt ud, saa at man saa Knapperne paa Arkens Stænger lige for Koret, men udentil saa man dem ikke; og den blev der indtil denne Dag.
10 Ndani ya Sanduku hapakuwepo kitu kingine chochote isipokuwa zile mbao mbili ambazo Mose alikuwa ameziweka ndani yake huko Horebu, mahali ambapo Bwana alifanya Agano na Waisraeli baada ya kutoka Misri.
Der var intet i Arken uden de to Tavler, som Mose lagde deri ved Horeb, der Herren gjorde Pagt med Israels Børn, der de droge ud af Ægypten.
11 Basi makuhani wakaondoka hapo Mahali Patakatifu. Makuhani wote waliokuwa huko walikuwa wamejiweka wakfu, bila kujali migawanyo yao.
Og det skete, der Præsterne gik ud af det Hellige (thi alle Præster, som fandtes, havde helliget sig, saa at de ikke holdt sig efter Skifterne;
12 Walawi wote waliokuwa waimbaji, yaani, Asafu, Hemani, Yeduthuni, wana wa ndugu zao, walisimama upande wa mashariki wa madhabahu, wakiwa wamevaa kitani safi huku wakipiga matoazi, vinubi na zeze. Walikuwa pamoja na makuhani 120 wakipiga tarumbeta.
og Leviterne, Sangerne, alle sam men, baade Asaf, Heman og Jeduthun og deres Børn og deres Brødre, iførte kosteligt Linklæde, med Cymbler og med Psaltre og Harper, stode Østen ved Alteret og hos dem hundrede og tyve Præster, som blæste i Basunerne);
13 Wapiga tarumbeta na waimbaji wakaungana katika sauti linganifu, ikawa kama vile ni sauti moja, wakimsifu na kumshukuru Bwana, nao alipoinua sauti zao pamoja na tarumbeta na matoazi na vyombo vingine vya uimbaji, wakamsifu Bwana wakisema: “Yeye ni mwema; upendo wake unadumu milele.” Ndipo Hekalu la Bwana likajazwa na wingu,
ja det skete, der de som een Mand blæste i Basuner og sang for enstemmigt at lade sig høre med Lov og Tak til Herren, og der de opløftede Røsten med Basuner og med Cymbler og med andre Sanginstrumenter, og der de lovede Herren, at han er god, og hans Miskundhed er evindelig: Da blev Huset i Herrens Hus fyldt med en Sky.
14 nao makuhani hawakuweza kufanya huduma yao kwa sababu ya lile wingu, kwa kuwa utukufu wa Bwana ulijaza Hekalu la Mungu.
Og Præsterne kunde ikke staa og gøre Tjeneste for Skyen; thi Herrens Herlighed fyldte Guds Hus.

< 2 Nyakati 5 >