< 2 Nyakati 4 >

1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
Uzunluqi yigirme gez, kengliki yigirme gez, égizliki on gez kélidighan bir mis qurban’gah yasatti.
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
U mistin «déngiz» yasatti; uning shekli dügilek bolup, u girwikidin bu girwikigiche on gez kéletti; égizliki besh gez, aylanmisi ottuz gez idi.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
«Déngiz»ning sirtqi asta qismi buqining shekli bilen chörüldürüp bézelgen bolup, buqilar herbir gezge ondin, ikki qatar qilinip, mis «déngiz» bilen teng quyup chiqilghanidi.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
Mis «déngiz»ni on ikki mis buqa kötürüp turatti; uning üchi shimalgha, üchi gherbke, üchi jenubqa, üchi sherqqe qarap turatti. «déngiz» buqining dümbisige yatquzulghan bolup, buqilarning quyruqi ichi terepte idi.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
Mis déngizning qélinliqi bir alqan bolup, chörisi chinining girwikidek niluper sheklide qilin’ghan, uninggha üch ming bat su patatti.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
U yene on «yuyush dési» yasitip, beshini mis déngizning ong teripige, beshini sol teripige qoyghuzdi; köydürme qurbanliqlargha ishlitidighan buyum-eswablirining hemmisi shu daslarda yuyulatti; «déngiz» bolsa kahinlarning yuyunushi üchün ishlitiletti.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
U yene belgilen’gen shekilde on altun chiraghdan yasitip muqeddes jayning ichige ornatti; uning beshini ong terepke, beshini sol terepke qoydurdi.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
Yene on shire yasitip muqeddes jayning ichige qoyghuzdi; uning beshini ong terepke, beshini sol terepke qoyghuzdi. U yene yüz dane altun chine yasatti.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
U yene «kahinlar hoylisi», chong hoyla we chong hoylining derwazilirini yasatti we derwazilarning hemmisini mis bilen qaplatti.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
U mis «déngiz»ni ibadetxanining ong teripige, yeni sherqiy jenub teripige qoyghuzdi.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
Huram yene qazan, kürek we qacha-quchilarni etküzdi. Huram shu teriqide Sulayman padishah üchün Xudaning öyining barliq qurulush xizmitini püttürdi,
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
Yeni ikki tüwrük, ikki tüwrükning üstidiki apqursiman ikki bash we bu ikki bashni yépip turidighan ikki torni yasitip püttürdi.
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
Shu ikki tor üstige qaychilashturulghan töt yüz anarni yasatti; bir torda ikki qatar anar bolup, tüwrük üstidiki apqursiman ikki bashni yépip turatti.
14 vishikio pamoja na masinia yake;
U on das tegliki we das teglikige qoyulidighan on «yuyush dési»ni,
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
«mis déngiz» we uning astidiki on ikki mis buqini yasatquzdi.
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
Qazan, kürek, wilka-ilmekler, we munasiwetlik barliq eswablarni Huram-Abi Perwerdigarning öyini dep Sulayman padishahqa parqiraydighan mista yasitip berdi.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
Padishah bularni Iordan tüzlenglikide, Sukkot bilen Zeredatah otturisida, [shu yerdiki] séghiz layda qélip yasap, quydurup chiqti.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Sulayman yasatquzghan bu eswablarning sani intayin köp idi; ketken misning éghirliqini ölchep bolmaytti.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
Sulayman yene Xudaning öyi ichidiki barliq eswablarni yasatti — yeni altun xushbuygahni, «teqdim nan» qoyulidighan shirelerni
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
we sap altunda qilin’ghan chiraghdanlar bilen chiraghlirini yasatquzdi; bu chiraghlar belgilime boyiche ichki «kalamxana» aldida yandurush üchün boldi.
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
U yene chiraghdanning gülliri, chiragh we pilik qaychilirining hemmisini altundin qildurdi (ular sap aldundin idi).
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
U yene péchaqlar, tawaqlar, piyale-qacha we küldanlarning hemmisini sap altundin qildurdi. U öyning ishiklirini, yeni ichidiki eng muqeddes jaygha kiridighan ichki qatlima ishikler we öyning «muqeddes jay»ining tashqiriqi ishiklirini altundin qildurdi.

< 2 Nyakati 4 >