< 2 Nyakati 4 >

1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
Il fit aussi un autel d’airain de vingt coudées de longueur, de vingt coudées de largeur, et de dix coudées de hauteur:
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
Et la mer d’airain, jetée en fonte, de dix coudées d’un bord jusqu’à l’autre, était toute ronde: elle avait cinq coudées de hauteur, et un cordon de trente coudées entourait sa circonférence.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
De plus, une représentation de bœufs était au-dessous de la mer, et certaines ciselures au dehors entouraient comme en deux rangs la partie la plus large de la mer dans un espace de dix coudées. Or ces bœufs avaient été jetés en fonte.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
Et la mer elle-même était posée sur douze bœufs, dont trois regardaient l’aquilon, et trois autres l’occident; or trois autres, le midi, et les autres, l’orient, tous ayant la mer posée sur eux: or la partie de derrière des bœufs était en dedans sous la mer.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
L’épaisseur de la mer avait la mesure d’un palme, et son bord était fait comme le bord d’une coupe, ou d’un lis épanoui: et elle contenait trois mille métrètes.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
Mais il fit aussi dix conques, et il en mit cinq à droite et cinq à gauche, pour qu’on y lavât tout ce qui devait être offert en holocauste; mais c’est dans la mer que les prêtres se lavaient.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
Il fit en outre dix chandeliers d’or, selon la forme d’après laquelle il avait ordonné de les faire; et il les mit dans le temple, cinq à droite et cinq à gauche;
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
Et de plus dix tables; et il les mit dans le temple, cinq à droite et cinq à gauche, ainsi que cent fioles d’or.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
Il fit encore le parvis des prêtres, et la grande basilique, et à la basilique des portes qu’il couvrit d’airain.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
Quant à la mer, il la mit du côté droit contre l’orient, vers le midi.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
Hiram fit aussi les chaudières, les grandes fourchettes et les fioles, et il acheva tout l’ouvrage du roi dans la maison de Dieu;
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
C’est-à-dire les deux colonnes, les architraves, les chapiteaux, et les espèces de réseaux qui couvraient les chapiteaux par-dessus les architraves.
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
Il fit encore les quatre cents grenades et les deux réseaux, de manière que deux rangs de grenades étaient attachés ensemble à chacun des réseaux qui couvraient les architraves et les chapiteaux des colonnes.
14 vishikio pamoja na masinia yake;
Il fit aussi les bases d’airain, et les conques qu’il superposa aux bases;
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
La mer unique, et aussi les douze bœufs sous la mer,
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
Et les chaudières, et les grandes fourchettes, et les fioles. Hiram, son père, fit à Salomon tous les vases pour la maison du Seigneur, d’un airain très pur.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
C’est dans la contrée du Jourdain que le roi les jeta en fonte, dans la terre argileuse, entre Sochoth et Sarédatha.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Or la multitude de ces vases était innombrable; en sorte qu’on ignorait le poids de l’airain.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
Ainsi Salomon fit tous les vases de la maison de Dieu, ainsi que l’autel d’or, les tables, et sur elles les pains de proposition.
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
Il fit encore d’un or très pur les chandeliers avec leurs lampes, pour luire devant l’oracle, selon le rite;
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
Ainsi que certains fleurons, les lampes et les pincettes d’or: toutes ces choses furent faites d’un or très pur.
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
Il fit aussi les cassolettes, les encensoirs, les fioles et les petits mortiers, d’un or très pur. Et il cisela les portes du temple intérieur, c’est-à-dire du Saint des saints; et les portes du temple à l’extérieur étaient d’or. Et ainsi fut achevé tout l’ouvrage que fit Salomon pour la maison du Seigneur.

< 2 Nyakati 4 >