< 2 Nyakati 4 >

1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
Et il fit un autel d'airain long de vingt coudées, large de vingt coudées, et haut de dix coudées.
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
Et il fit la Mer, en fonte, ayant dix coudées de l'un de ses bords à l'autre, ronde dans son contour et haute de cinq coudées, et un cordon de trente coudées l'embrassait tout à l'entour.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
Et des figures de coloquintes étaient en dessous à l'entour, l'embrassant dans sa Circonférence à raison de dix par coudée, ceignant la Mer dans sa circonférence; il y avait deux rangées de coloquintes coulées d'une même fonte avec elle.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
Elle reposait sur douze taureaux regardant, trois le septentrion, et trois l'occident, et trois le midi, et trois l'orient, et toutes leurs croupes étaient tournées en dedans, et la mer posait dessus en hauteur.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
Et son épaisseur était d'une palme, et son rebord comme le travail du rebord d'une coupe, en fleur de lis, et quant à sa capacité en baths, elle en pouvait contenir trois mille.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
Et il fit dix bassins, dont il plaça cinq à droite et cinq à gauche, pour y laver; on y rinçait la batterie de l'holocauste, et la Mer servait à l'ablution des Prêtres.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
Et il fit les candélabres d'or, selon leur façon, et les plaça dans le Temple, cinq à droite et cinq à gauche.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
Et il fit dix tables qu'il déposa dans le temple, cinq à droite et cinq à gauche; et il fit cent jattes d'or.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
Et il fit le Parvis des Prêtres, et le grand Parvis et des portes au grand Parvis, et il en revêtit d'airain les battants.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
Et il plaça la Mer au côté droit de l'édifice, à l'orient vers le midi.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
Et Huram fit les pots, les pelles et les jattes; et Huram termina le travail qu'il faisait pour le roi Salomon dans la Maison de Dieu,
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
deux colonnes et les globes et les chapiteaux sur le faîte des deux colonnes et les deux treillis recouvrant les deux globes des chapiteaux sur le faîte des colonnes,
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
et les quatre cents grenades des deux treillis, deux rangées de grenades par treillis pour couvrir les deux globes des chapiteaux aux colonnes;
14 vishikio pamoja na masinia yake;
et il fit les piédestaux et fit les bassins posant sur les piédestaux;
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
la Mer, unique, et les douze taureaux qui étaient dessous;
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
et les pots et les pelles et les fourchettes et tous les ustensiles assortis, Huram-Abiv les fit pour le roi Salomon dans le Temple de l'Éternel, en airain poli.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
C'est dans le Cercle du Jourdain que le roi les fit couler dans une terre glaise entre Succoth et Tserédatha.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Et Salomon fit tous ces ustensiles en grande quantité; car on ne s'enquit point du poids de l'airain.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
Et Salomon fit tous les meubles qui étaient dans la Maison de Dieu, savoir, l'autel d'or et les tables sur lesquelles étaient les pains de présentation,
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
et les candélabres et leurs lampes d'or pur pour brûler selon le rite devant le Sanctuaire,
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
et les fleurs et les lampes et les pinces d'or, tout d'or pur;
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
et les couteaux et les jattes et les coupes et les bouilloires d'or fin, et à la porte du Temple ses battants, intérieurs, du Lieu Très-Saint, et les battants des portes de l'édifice, du Temple, d'or.

< 2 Nyakati 4 >