< 2 Nyakati 4 >

1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
Also he made a brasun auter of twenti cubitis of lengthe, and of twenti cubitis of breede, and of ten cubitis of heiythe;
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
he made also a yotun see of ten cubitis fro brynke til to brynke, round bi cumpas; it hadde fyue cubitis of heiythe; and a coorde of thritti cubitis cumpasside the cumpas therof.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
And the licnesse of oxis was vndur it, and bi ten cubitis summe grauyngis with outforth cumpassiden the brynke of the see as with tweyne ordris; sotheli the oxis weren yotun.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
And thilke see was set on twelue oxis, of whiche oxis thre bihelden to the north, and othere thre to the west, sotheli thre othere bihelden the south, and thre `that weren residue bihelden the eest, and hadden the see set aboue; but the hyndrere partis of the oxis weren with ynne vndur the see.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
Sotheli the thicknesse therof hadde the mesure of a pawm of the hond, and the brynke therof was as the brynke of a cuppe, ethir of a lilie crokid ayen, and it took thre thousynde metretis of mesure.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
Also he made ten holowe vessels, and settide fyue at the riytside, and fyue at the leftside, that thei schulden waische in tho alle thingis, whiche thei schulden offre in to brent sacrifice; sotheli the preestis weren waischun in the see.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
Sotheli he made ten goldun candilstikis bi the licknesse which he hadde comaundid to be maad, and he settide tho in the temple, fyue at the riytside and fyue at the leftsid.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
And he made also ten boordis, and settide tho in the temple, fyue at the riytside and fyue at the leftside.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
Also he made an hundrid goldun viols. `Also he made a large place of preestis, and a greet hows, and doris in the greet hows, which he hilide with bras.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
Forsothe he settide the see in the riytsyde ayens the eest at the south.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
Also Iram made cawdruns, and fleischokis, and viols, and he fillide al the werk of the kyng in the hows of God,
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
that is, twei pilers, and pomels, and heedis, and as summe nettis, that hiliden the heedis aboue the pomels;
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
also he made fourti pumgarnadis, and twei werkis lijk nettis, so that two ordris of pumgarnadis weren ioyned to ech werk like nettis, which hiliden the pomels, and heedis of the pilers.
14 vishikio pamoja na masinia yake;
He made also foundementis, and holow vessels, whiche he settide on the foundementis;
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
he made o see, and twelue oxis vndur the see,
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
and caudruns, and fleischookis, and viols. Iram, the fadir of Salomon, made to hym alle vessels in the hows of the Lord of clennest bras.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
The kyng yetide tho in the cuntrey of Jordan, in cleiy lond bitwixe Socoth and Saredata.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
Forsothe the multitude of vessels was vnnoumbrable, so that the weiyte of bras was not knowun.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
And Salomon made alle the vessels of Goddis hows, the goldun auter, `and bordis, and loouys of settyng forth on tho;
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
and candilstikis of purest gold, with her lanternes, that tho schulden schyne bifor Goddis answering place bi the custom;
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
and he made summe werkis lijk flouris, and lanternes, and goldun tongis; alle thingis weren maad of clennest gold;
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
also he made pannes for colis to brenne encense, and censeris, and viols, and morters, of pureste gold. And he grauyde doris of the ynnere temple, that is, in the hooli of hooli thingis, and the goldun doris of the temple with out forth; and so al the werk was fillid that Salomon made in the hows of the Lord.

< 2 Nyakati 4 >