< 2 Nyakati 4 >

1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
And he makes an altar of bronze: twenty cubits its length, and twenty cubits its breadth, and ten cubits its height.
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
And he makes the molten sea; ten by the cubit, from its edge to its edge, round in encompassment, and its height [is] five by the cubit, and a line of thirty by the cubit surrounds it around.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
And the likeness of oxen [is] under it, encompassing it all around, ten to the cubit, surrounding the sea around; two rows of oxen are cast in its being cast.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
It is standing on twelve oxen, three facing the north, and three facing the west, and three facing the south, and three facing the east, and the sea [is] on them above, and all their back parts [are] within.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
And its thickness [is] a handbreadth, and its lip as the work of the lip of a cup flowered with lilies; holding [within]—it contains three thousand baths.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
And he makes ten lavers, and puts five on the right, and five on the left, to wash with them; they purge the work of the burnt-offering with them; and the sea [is] for priests to wash with.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
And he makes the ten lampstands of gold, according to their ordinance, and places [them] in the temple, five on the right, and five on the left.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
And he makes ten tables, and places [them] in the temple, five on the right, and five on the left; and he makes one hundred bowls of gold.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
And he makes the court of the priests, and the great court, and doors for the court, and he has overlaid their doors with bronze.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
And he has placed the sea on the right shoulder eastward, from toward the south.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
And Huram makes the pots, and the shovels, and the bowls, and Huram finishes to make the work that he made for King Solomon in the house of God;
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
two pillars, and the bowls, and the crowns on the heads of the two pillars, and the two networks to cover the two bowls of the crowns that [are] on the heads of the pillars;
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
and the four hundred pomegranates for the two networks, two rows of pomegranates for the one network, to cover the two bowls of the crowns that [are] on the front of the pillars.
14 vishikio pamoja na masinia yake;
And he has made the bases; and he has made the lavers on the bases;
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
the one sea, and the twelve oxen under it,
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
and the pots, and the shovels, and the forks, and all their vessels, his father Huram has made for King Solomon, for the house of YHWH, of bronze purified.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
The king has cast them in the circuit of the Jordan, in the thick soil of the ground, between Succoth and Zeredathah.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
And Solomon makes all these vessels in great abundance, that the weight of the bronze has not been searched out.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
And Solomon makes all the vessels that [are for] the house of God, and the altar of gold, and the tables, and on them [is] Bread of the Presentation;
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
and the lampstands, and their lamps, for their burning according to the ordinance, before the oracle, of gold refined;
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
and the flowers, and the lamps, and the tongs of gold—it [is] the perfection of gold;
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
and the snuffers, and the bowls, and the spoons, and the censers, of gold refined, and the opening of the house, its innermost doors to the Holy of Holies, and the doors of the house to the temple, of gold.

< 2 Nyakati 4 >