< 2 Nyakati 4 >
1 Mfalme Solomoni akatengeneza madhabahu ya shaba yenye urefu wa dhiraa ishirini, upana wa dhiraa ishirini na kimo chake dhiraa kumi.
He made also an altar of copper, twenty cubits being its length, and twenty cubits its breadth, and ten cubits its height.
2 Akatengeneza Bahari ya kusubu, yenye umbo la mviringo, ya dhiraa kumi kutoka ukingo hadi ukingo na kimo cha dhiraa tano. Kamba ya urefu wa dhiraa thelathini ingeweza kuizunguka.
He made also the molten sea, being ten cubits from the one brim to the other, rounded all about, and it was five cubits in height: and a line of thirty cubits did encompass it round about.
3 Chini ya huo ukingo, kulikuwa na mafahali kuizunguka, yaani mafahali kumi katika kila dhiraa moja. Hayo mafahali waliyasubu katika safu mbili yakiwa ya kitu kimoja na hiyo Bahari.
And likenesses of oxen were under it, encompassing it all round about, ten in a cubit, encircling the sea round about: the oxen were in two rows [and were] cast [with it], when it was cast.
4 Bahari hiyo ilikaa juu ya mafahali kumi na wawili, mafahali watatu walielekeza nyuso zao kaskazini, watatu magharibi, watatu kusini na watatu mashariki. Bahari hiyo ilikaa juu ya hao mafahali, nazo sehemu zao za nyuma zilielekeana.
It was standing upon twelve oxen, three looking toward the north, and three looking toward the west, and three looking toward the south, and three looking toward the east; and the sea was resting above upon them, and all their hinder parts were inward.
5 Unene wake ulikuwa nyanda nne, na ukingo wake ulifanana na ukingo wa kikombe, kama ua la yungiyungi iliyochanua. Iliweza kuchukua bathi 3,000.
And its thickness was a hand's breadth, and its brim like the brim of a cup, with lily-buds; and it could hold and contain three thousand baths.
6 Kisha akatengeneza masinia kumi kwa ajili ya kuoshea vifaa, naye akayaweka matano upande wa kusini na matano upande wa kaskazini. Ndani yake ndimo walioshea vifaa vya kutumika katika sadaka za kuteketezwa, lakini ile Bahari ilikuwa ni kwa ajili ya makuhani kunawia.
He made also ten lavers; and he placed five on the right hand, and five on the left, to wash in them: what belonged to the burnt-offering they rinsed off at them; but the sea was for the priests to wash in.
7 Akatengeneza vinara vya taa kumi vya dhahabu kama ilivyoainishwa kwao na kuviweka hekaluni, vinara vitano upande wa kusini na vitano upande wa kaskazini.
And he made ten candlesticks of gold according to their prescribed manner: and he placed [them] in the temple, five on the right side, and five on the left.
8 Akatengeneza meza kumi na kuziweka hekaluni, tano upande wa kusini na tano upande wa kaskazini. Pia akatengeneza mabakuli 100 ya dhahabu ya kunyunyizia.
He made also ten tables, and he set them in the temple, five on the right side, and five on the left. And he made a hundred bowls of gold.
9 Akatengeneza ukumbi wa makuhani na ukumbi mwingine mkubwa na milango yake, naye akaifunika hiyo milango kwa shaba.
And he made the court of the priests, and the great out-court, and doors for the out-court, and their doors he overlaid with copper.
10 Akaweka ile Bahari upande wa kusini, kwenye pembe ya kusini mashariki ya nyumba.
And the sea he placed on the right side toward the east, opposite to the south.
11 Pia akatengeneza masufuria, masepetu na mabakuli ya kunyunyizia. Kwa hiyo Huramu akakamilisha kazi katika Hekalu la Mungu kama vile Mfalme Solomoni alikuwa amemwagiza, yaani:
And Churam made the pots, and the shovels, and the basins. And Churam made an end of doing the work which he made for king Solomon in the house of God:
12 zile nguzo mbili; yale mataji mawili yaliyokuwa juu ya hizo nguzo, zile nyavu mbili za kupamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli yaliyowekwa juu ya zile nguzo;
The two pillars, and the bowls, and the capitals on the top of the two pillars, and the two networks to cover the bowl-shaped capitals which were on the top of the pillars;
13 yale makomamanga 400 kwa ajili ya hizo nyavu mbili (safu mbili za makomamanga kwa kila wavu yakipamba hayo mataji mawili yenye umbo la bakuli juu ya hizo nguzo);
And the four hundred pomegranates for the two networks, two rows of pomegranates for each network, to cover the two bowl-shaped capitals which were upon the front of the pillars.
14 vishikio pamoja na masinia yake;
The bases also did he make, and the lavers made he upon the bases.
15 hiyo Bahari na hao mafahali kumi na wawili chini yake;
The one sea, and the twelve oxen under it,
16 pia hayo masufuria, masepetu, uma za nyama na vyombo vingine vyote vilivyohusiana. Vitu vyote ambavyo Huramu-Abi alimtengenezea Mfalme Solomoni kwa ajili ya Hekalu la Bwana vilikuwa vya shaba iliyosuguliwa.
And the pots also, and the shovels, and the forks, and all their instruments, did Churam-Abiv make for king Solomon for the house of the Lord, of polished copper.
17 Mfalme aliagiza wavisubu vitu hivi kwenye kalibu za udongo wa mfinyanzi katika uwanda wa Yordani kati ya Sukothi na Sereda.
In the plain of the Jordan did the king cast them, in the clay-ground between Succoth and Zeredathah.
18 Vitu hivi vyote Mfalme Solomoni alivyotengeneza vilikuwa vingi sana hivi kwamba uzito wa shaba haungekadirika.
And Solomon made all these vessels in very great abundance; for the weight of the copper was not inquired into.
19 Solomoni pia akatengeneza samani zote zilizokuwa ndani ya Hekalu la Mungu: madhabahu ya dhahabu; meza za kuweka mikate ya Wonyesho;
And Solomon made all the vessels that pertained to the house of God; and the altar of gold also, and the tables whereon the show-bread [was set];
20 vinara vya taa vya dhahabu safi pamoja na taa zake ili ziwake mbele ya sehemu takatifu ya ndani kama ilivyoelekezwa;
And the candlesticks with their lamps, to light them after the prescribed manner before the debir, of pure gold.
21 maua ya dhahabu yaliyofanyizwa, taa na makoleo (vilikuwa vya dhahabu bora kabisa);
And the flowers, and the lamps, and the tongs, were of gold, the purest of gold;
22 mikasi ya dhahabu safi, mabakuli ya kunyunyizia, masinia na vyetezo; milango ya dhahabu ya Hekalu: yaani milango ya ndani ya Patakatifu pa Patakatifu, na milango ya ukumbi mkuu.
And the knives, and the basins, and the spoons, and the censers were of pure gold; and the entrance of the house, its inner doors for the most holy place, and the doors of the house of the temple, were of gold.