< 2 Nyakati 36 >

1 Watu wa nchi wakamchukua Yehoahazi mwana wa Yosia na kumfanya mfalme mahali pa baba yake huko Yerusalemu.
Kalpasanna, dagiti tattao iti daga ket innalada ni Joahaz a putot a lalaki ni Josias, ket insaadda isuna nga ari a kasukat ni amana idiay Jerusalem.
2 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala, akatawala huko Yerusalemu kwa miezi mitatu.
Agtawen ni Joahaz iti 23 idi mangrugi isuna nga agari, ket nagari isuna iti tallo a bulan idiay Jerusalem.
3 Mfalme wa Misri akamwondoa madarakani huko Yerusalemu na akatoza Yuda kodi ya talanta 100 za fedha na talanta moja ya dhahabu.
Inikkat isuna ti ari ti Egipto idiay Jerusalem, ket pinagbayadna ti daga iti 4, 000 a kilo ti pirak ken uppat a kilo ti balitok.
4 Mfalme wa Misri akamweka Eliakimu, nduguye Yehoahazi, kuwa mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu na kubadili jina la Eliakimu kuwa Yehoyakimu. Lakini Neko akamchukua Yehoahazi, Nduguye Eliakimu akampeleka Misri.
Insaad ti ari ti Egipto ni Eliakim, a kabsat ni Joahaz a kas ari ti Juda ken Jerusalem, ken sinukatanna ti naganna iti Jehoiakim. Kalpasanna inyapanna ti kabsat ni Eliakim a ni Joahaz idiay Egipto.
5 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Akafanya maovu machoni pa Bwana Mungu wake.
Agtawen ni Jehoyakim iti 25 idi nangrugi nga agari, ket nagari isuna iti 11 a tawen idiay Jerusalem. Inaramidna ti dakes iti imatang ni Yahweh a Diosna.
6 Nebukadneza mfalme wa Babeli akamshambulia na kumfunga kwa pingu za shaba akampeleka Babeli.
Kalpasanna, rinaut isuna ni Nebucadnesar nga ari iti Babilonia ket inkawarda isuna ket inyapanda idiay Babilonia.
7 Nebukadneza akachukua pia vyombo kutoka Hekalu la Bwana na kuviweka katika hekalu lake huko Babeli.
Nangala pay ni Nebucadnesar kadagiti sumagmamano a banbanag iti balay ni Yahweh ket inyapanna idiay Babilonia ket inkabilna dagitoy iti palasiona idiay Babilonia.
8 Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu, machukizo aliyoyafanya na yote yaliyoonekana dhidi yake, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
Maipanggep kadagiti dadduma a pakasaritaan maipanggep kenni Jehoyakim, dagiti makarimon a banbanag nga inaramidna, ken dagiti naduktalan a maibusor kenkuana, kitaenyo, naisurat dagitoy iti Libro dagiti Ar-ari iti Juda ken Israel. Kalpasanna, ti putot a lalaki ni Jehoyakim ti simmukat kenkuana nga ari.
9 Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu na siku kumi. Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana.
Walo ti tawen ni Jehoyakim idi nangrugi isuna nga agari; nagari isuna iti tallo a bulan ket sangapulo nga aldaw idiay Jerusalem. Dakes iti imatang ni Yahweh ti inaramidna.
10 Mnamo majira ya vuli, Mfalme Nebukadneza akatuma watu, nao wakamleta Babeli, pamoja na vyombo vya thamani kutoka Hekalu la Bwana. Naye akamfanya Sedekia, ndugu yake Yehoyakimu kuwa mfalme wa Yuda na Yerusalemu.
Iti panagrugi ti tawen, nangibaon ni ari Nebucadnesar kadagiti lallaki a napan nangala kenkuana ket inyapanda iti Babilonia, agraman dagiti napapateg a banbanag manipud iti balay ni Yahweh, ket insaadna ni Zedekias a kabagian ni Jehoyakim a kas ari ti Juda ken Jerusalem.
11 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu kwa miaka kumi na mmoja.
Agtawen ni Zedekias iti 21 idi nangrugi a nagari isuna; nagari isuna iti 11 a tawen idiay Jerusalem.
12 Alifanya maovu machoni pa Bwana Mungu wake, wala hakujinyenyekeza mbele ya nabii Yeremia, ambaye alinena neno la Bwana.
Dakes iti imatang ni Yahweh a Diosna ti naramidna. Saan isuna a nagpakumbaba iti sangoanan ni Jeremias a profeta a nangisao iti nagtaud iti ngiwat ni Yahweh.
13 Pia alimwasi Mfalme Nebukadneza, ambaye alikuwa amemwapisha kwa jina la Mungu. Akashupaza shingo na akafanya moyo wake kuwa mgumu wala hakutaka kumgeukia Bwana, Mungu wa Israeli.
Nagrebelde met ni Zedekias kenni Ari Nebucadesar a nangpasapata kenkuana nga agbalin isuna a napudno kenkuana babaen iti Dios. Ngem pinatangken ni Zedekias ti ulona ken pinatangkenna ti pusona a maibusor kenni Yahweh, a Dios ti Israel.
14 Zaidi ya hayo viongozi wote wa makuhani pamoja na watu wakazidi kukosa uaminifu zaidi na zaidi, wakafanya machukizo yote kama walivyofanya mataifa wakinajisi Hekalu la Bwana alilokuwa amelitakasa huko Yerusalemu.
Maysa pay, nagsukir iti kasta unay dagiti amin a papanguloen dagiti papadi ken dagiti tattao, tinuladda dagiti makarimon a banbanag nga ar-aramiden dagiti sabali a tattao. Tinulawanda ti balay ni Yahweh nga impaayna a para kenkuana idiay Jerusalem.
15 Bwana, Mungu wa baba zao, akawapelekea neno kupitia wajumbe wake tena na tena, kwa sababu alikuwa anawahurumia watu wake pamoja na mahali pa maskani yake.
Namin adu a nangipatulod ti mensahe kadakuada ni Yahweh a Dios dagiti kapuonanda babaen kadagiti mensaherona ti Dios, gapu ta maasian isuna kadagiti tattaona ken iti lugar a pagnanaedanna.
16 Lakini waliwadhihaki wajumbe wa Bwana wakayadharau maneno yake na kuwacheka manabii wake mpaka ghadhabu ya Bwana ikawa kubwa dhidi ya watu wake na hakukuwa na namna ya kuituliza.
Ngem inuy-uyawda dagiti mensaherona, linalaisda dagiti sasaona, ken kinatkatawaanda dagiti profetana agingga a simged manen ti pungtot ni Yahweh kadagiti tattaona, agingga nga awan iti makalapped iti daytoy.
17 Mungu akamwinua dhidi yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao wa kiume kwa upanga ndani ya mahali patakatifu, ambaye hakumbakiza kijana mwanaume wala kijana mwanamke, wazee wala vikongwe. Mungu akawatia wote mikononi mwa Nebukadneza.
Inyeg ngarud ti Dios kadakuada ti ari iti Caldeo a nangpapatay kadagiti agtutubo a lallaki babaen iti kampilan idiay santuario, ken saanna a kinaasian dagiti agtutubo a lallaki wenno berhen a babbalasang, dagiti lallakay wenno ubanan. Inyawat amin ida ti Dios iti imana.
18 Akavichukua kwenda Babeli vyombo vyote kutoka Hekalu la Mungu, vikubwa na vidogo, hazina za Hekalu la Bwana pamoja na hazina za mfalme na za maafisa wake.
Dagiti amin nga alikamen iti balay ti Dios, dadakkel man wenno babassit, dagiti gameng iti balay ni Yahweh, ken dagiti gameng ti ari ken dagiti opisialna-inyapanna amin dagitoy idiay Babilonia.
19 Wakalichoma Hekalu la Mungu na kuzibomoa kuta za Yerusalemu, wakachoma moto majumba yote ya kifalme na kuharibu kila kitu chake cha thamani.
Pinuoranda ti balay ti Dios, rinebbada ti pader ti Jerusalem, pinuoranda dagiti amin a palasio iti daytoy, ken dinadaelda dagiti amin a napipintas a banbanag iti daytoy.
20 Wale watu walionusurika kuuawa kwa upanga wakachukuliwa kwenda uhamishoni Babeli. Nao wakawa watumishi wake na wa wanawe mpaka wakati wa utawala wa ufalme wa Uajemi ulifika.
Inyapan ti ari idiay Babilonia dagiti nakalisi iti kampilan. Nagbalinda nga adipenna ken adipen dagiti putotna a lallaki agingga iti panagturay ti pagarian iti Persia.
21 Nchi ikaendelea kufurahia pumziko lake la Sabato, wakati wote wa kufanywa kwake ukiwa ilipumzika mpaka ile miaka sabini ilipotimia katika kutimiza neno la Bwana lililonenwa na Yeremia.
Napasamak daytoy tapno matungpal ti sao ni Yahweh babaen kenni Jeremias, agingga a rumbeng nga aginana ti daga iti tunggal Aldaw a Panaginana. Nangilin ti Aldaw a Panaginana kabayatan a napanawan daytoy agingga iti 70 a tawen.
22 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Koreshi mfalme wa Uajemi, ili kulitimiza neno la Bwana lililosemwa na nabii Yeremia, Bwana aliusukuma moyo wa Koreshi mfalme wa Uajemi kutangaza katika himaya yake yote kwa maandishi:
Ita, iti umuna a tawen ni Ciro nga ari iti Persia, tapno mapasamak ti sao ni Yahweh babaen kenni Jeremias, tinignay ni Yahweh ti espirito ni Ciro nga ari ti Persia isu a nangaramid iti maysa a pangngeddeng iti entero a pagarianna, ket insuratna pay daytoy. Kinunana,
23 “Hili ndilo asemalo Koreshi mfalme wa Uajemi: “‘Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote duniani, na ameniagiza kumjengea Hekalu huko Yerusalemu katika Yuda. Yeyote wa watu wake miongoni mwenu, Mungu wake na awe pamoja naye, wacha huyo mtu na apande.’”
“Kastoy ti kuna ni Ciro nga ari ti Persia: Ni Yahweh a Dios sadilangit, ket inyawatna amin kaniak dagiti amin a pagarian iti daga. Binilinnak a mangipasdekak iti balay a para kenkuana idiay Jerusalem, nga adda idiay Juda. Siasinoman kadakayo a maibilang kadagiti tattaona, ni koma Yahweh a Diosyo ti adda kadakayo. Mapalubusan isuna a sumang-at iti daga.”

< 2 Nyakati 36 >