< 2 Nyakati 35 >

1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
Forsothe Josie made pask to the Lord in Jerusalem, that was offrid in the fourtenthe dai of the firste monethe;
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
and he ordeynede prestis in her offices; and he comaundide hem for to mynystre in the hows of the Lord.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
And he spak to the dekenes, at whos techyng al Israel was halewid to the Lord, Sette ye the arke in the seyntuarie of the temple, which Salomon, kyng of Israel, the sone of Dauid, bildide; for ye schulen no more bere it. But now serue `youre Lord God and his puple Israel,
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
and make you redi bi youre housis and meynees in the departyngis of ech bi hym silf, as Dauid, king of Israel, comaundide, and Salomon, his sone, discryuede;
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
and serue ye in the seyntuarie bi the meynees and cumpenyes of dekenes,
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
and be ye halewid, and offre ye pask; also `make redi youre britheren, that thei moun `do bi the wordis, whiche the Lord spak in the hond of Moyses.
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
Ferthermore Josie yaf to al the puple, that was foundun there in the solempnytee of pask, lambren, and kidis of the flockis, and of residue scheep `he yaf thritti thousynde, and of oxis thre thousynde; these thingis of al the catel of the kyng.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
And hise duykis offriden tho thingis whiche thei avowiden bi fre wille, as wel to the puple as to prestis and dekenes. Forsothe Elchie, and Zacharie, and Jehiel, princes of the hows of the Lord, yauen to preestis, to make pask in comyn, two thousynde and sixe hundrid scheep, and thre hundrid oxis.
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
Forsothe Chononye, and Semei, and Nathanael and hise britheren, also Asabie, Jahiel, and Josabaz, princis of dekenes, yauen to othere dekenes, to make pask, fyue thousynde of scheep, and fyue hundrid oxis.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
And the seruyce was maad redi; and preestis stoden in her office, and dekenes in cumpenyes, bi comaundement of the kyng; and pask was offrid.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
And preestis spreynten her hondis with blood, and dekenes drowen of the skynnes of sacrifices, and departiden tho sacrificis,
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
for to yyue bi the housis and meyneis of alle men; and that tho schulden be offrid to the Lord, as it is writun in the book of Moises; and of oxis thei diden in lijk maner.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
And thei rostiden pask on the fier, bi that that is writun in the lawe. Sotheli thei sethiden pesible sacrifices in pannes, and cawdruns, and pottis, and in haste thei deliden to al the puple;
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
but thei maden redi aftirward to hem silf, and to prestis; for preestis weren occupied `til to nyyt in the offryng of brent sacrifices and of ynnere fatnessis. Wherfor dekenes maden redi to hem silf and to preestis, the sones of Aaron, `the laste.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
Forsothe syngeris, the sones of Asaph, stoden in her ordre, bi the comaundement of Dauid, and of Asaph, and of Eman, and of Yditum, the profetis of the kyng; but the porteris kepten bi ech yate, so that thei yeden not awei fro the seruice, sotheli in a poynt; wherfor and dekenes, her britheren, maden redi metis to hem.
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Therfor al the religioun of the Lord was fillid riytfuli in that day, that thei maden pask, and offriden brent sacrifices on the auter of the Lord, bi the comaundement of kyng Josie.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
And the sones of Israel, that weren foundun there, maden pask in that tyme, and the solempnite of therf looues seuene daies.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
No pask was lijk this in Israel, fro the daies of Samuel, the prophete; but nethir ony of the kyngis of Israel made pask as Josie dide, to preestis and dekenes, and to al Juda and Israel, that was foundun, and to the dwelleris of Jerusalem.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
This pask was halewid in the eiytenthe yeer of `the rewme of Josie.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
Aftir that Josie hadde reparelid the temple, Nechao, the kyng of Egipt, stiede to fiyte in Carcamys bisidis Eufrates; and Josie yede forth in to his metyng.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
And he seide bi messangeris sent to hym, Kyng of Juda, what is to me and to thee? Y come not ayens thee to dai, but Y fiyte ayens another hows, to which God bad me go in haste; ceesse thou to do ayens God, which is with me, lest he sle thee.
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Josie nolde turne ayen, but made redi batel ayens hym; and he assentide not to the wordis of Nechao, bi Goddis mouth, but he yede for to fiyte in the feeld of Magedo.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
And there he was woundide of archeris, and seide to hise children, `Lede ye me out of the batel, for Y am woundid greetli.
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
Whiche baren hym ouer fro the chare in to an other chare, that suede hym, bi custom of the kyng, and `baren out hym in to Jerusalem; and he diede, and was biried in the sepulcre of hise fadris. And al Juda and Jerusalem biweiliden hym,
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Jeremye moost, of whom alle syngeris and syngeressis `til in to present dai rehersen `lamentaciouns, ether weilyngis, on Josie; and it cam forth as a lawe in Israel, Lo! it is seid writun in Lamentaciouns.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
Forsothe the residue of wordis of Josie, and of hise mercies, that ben comaundid in the lawe of the Lord,
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
and hise werkis, `the firste and the laste, ben wryten in the book of kyngis of Israel and of Juda.

< 2 Nyakati 35 >