< 2 Nyakati 35 >
1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
And Josiah kept, in Jerusalem, a passover unto Yahweh, —and they slaughtered the passover, on the fourteenth of the first month.
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
And he set the priests over their charges, —and encouraged them unto the service of the house of Yahweh;
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
and said to the Levites who gave instruction to all Israel as to the things which were hallowed unto Yahweh, Put the holy ark in the house which Solomon son of David king of Israel did build, it is not yours as a burden on the shoulder, —Now, serve ye Yahweh your God, and his people Israel;
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
and prepare yourselves by your ancestral houses, according to your courses, —by the writing of David king of Israel, and by what hath been written by Solomon his son;
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
and stand ye in the holy place, by the divisions of the ancestral house, for your brethren, the sons of the people, and the partitioning of an ancestral house, for the Levites.
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
So slaughter ye the passover, —and hallow yourselves, and prepare for your brethren, that they may do according to the word of Yahweh, by the hand of Moses.
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
And Josiah presented to the sons of the people—of flocks, young sheep and the young of the goats, the whole for the passover offerings, for all present, to the number of thirty thousand, and, of bullocks, three thousand, —these, out of the substance of the king.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
And, his rulers, willingly, to the people and to the priests and to the Levites, presented, —Hilkiah and Zechariah and Jehiel, chief rulers of the house of God, unto the priests, did give, for passover offerings, two thousand and six hundred, and, of bullocks, three hundred;
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
and, Conaniah, and Shemaiah and Nethanel his brethren, and Hashabiah and Jeiel and Jozabad, rulers of the Levites, presented to the Levites, for passover offerings, five thousand, and, of bullocks, five hundred.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
Thus was the service prepared, —and the priests stood in their place, and the Levites in their courses, according to the commandment of the king.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
So they slaughtered the passover, and the priests dashed [the blood received] at their hand, and the Levites were flaying [the offerings].
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
Then they removed the ascending-sacrifice, that they might give them—by the divisions of each ancestral house—unto the sons of the people, to offer unto Yahweh, as it is written in the Book of Moses, —and, in like manner, with the bullocks.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
And they cooked the passover with fire, according to the regulation, —but, the hallowed things, cooked they in cauldrons and in pots and in bowls, and then took quickly, unto all the sons of the people.
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
And, afterwards, prepared they for themselves and for the priests, because, the priests, the sons of Aaron, had been engaged in offering up the ascending-sacrifice and the fat pieces, until night, —the Levites, therefore prepared for themselves, and for the priests, the sons of Aaron.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
the singers also, the sons of Asaph, were in their place, according to the commandment of David, and Asaph, and Heman, and Jeduthun the seer of the king, and, the doorkeepers, were at the several doors, —there was no need for them to remove from their service, for, their brethren the Levites, prepared for them.
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Thus was all the service of Yahweh prepared on that day; to keep the passover, and to offer up the ascending-sacrifice, upon the altar of Yahweh, —according to the commandment of King Josiah.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
So the sons of Israel who were present kept the passover at that time, —and the festival of unleavened cakes, seven days.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
And there had not been kept, a passover like it, in Israel, since the days of Samuel the prophet, —yea, none of the kings of Israel, had kept such a passover as was kept by Josiah and the priests and the Levites and all Judah and Israel that were present, and the inhabitants of Jerusalem.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
In the eighteenth year of the reign of Josiah, was kept this passover.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
After all this—when Josiah had prepared the house, Neco king of Egypt came up, -to fight against Carchemish, by Euphrates, and Josiah went forth against him.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
But he sent unto him messengers, saying—What have I to do with thee, O king of Judah? not against thee, [have I come] this day, but against the house wherewith I have war, and, God, hath given word to speed me, —cease thou from [provoking] God who is with me, lest he destroy thee.
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Howbeit Josiah turned not his face from him, for, to fight against him, he had disguised himself, and he hearkened not unto the words of Neco, from the mouth of God, —so he came to fight in the valley of Megiddo.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
And the archers shot at King Josiah, —and the king said unto his servants, Take me away, for I am sore wounded.
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
So his servants took him away out of the war-chariot, and conveyed him in a second chariot which he had, and carried him to Jerusalem, and he died, and was buried in the sepulchres of his fathers, —and, all Judah and Jerusalem, were mourning over Josiah.
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
And Jeremiah chanted a dirge over Josiah, and all the singing men and singing women in their dirges have spoken concerning Josiah, until this day, and they appointed them by statute for Israel, —and, there they are, written among the dirges.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
But, the rest of the story of Josiah, and his lovingkindness, —according to that which is written in the law of Yahweh:
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
even his story, first and last, there it is, written in the book of the Kings of Israel and Judah.