< 2 Nyakati 35 >
1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
Josiah ni Jerusalem vah BAWIPA hanlah ceitakhai pawi a sak. Thapa yung pasuek, hnin hlaipali hnin vah, ceitakhai pawi hanlah a thei.
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
Vaihma hah thaw a poe teh, BAWIPA im dawk thaw tawk hanlah tha a poe.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
Isarelnaw kacangkhaikung lah Cathut hanlah hmoun e Levihnaw koe, Isarel siangpahrang Devit capa Solomon ni im a sak e dawk kathounge thingkong hah hrueng awh leih. Na loung hoi hrawm hanlah ngai mahoeh toe. BAWIPA na Cathut hoi a tami Isarelnaw thaw hah tawk awh leih.
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
Isarel siangpahrang Devit hoi a capa ni thut e patetlah imthungkhu kahrawikungnaw hoi kamcu lah ahuhu lahoi o hanlah kârakueng awh.
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
Na hmaunawnghanaw imthungkhu kahrawikung hoi ka kamcu lah Levih taminaw hanlah hmuen ao e patetlah kathounge hmuen koe awm awh.
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
Ceitakhai pawi thuengnae hah thet awh nateh, kâthoung sak awh. Mosi hno laihoi BAWIPA ni a dei e patetlah sak thai awh nahan na hmaunawnghanaw hanlah kârakueng awh.
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
Josiah ni hote hmuen koe kaawm e taminaw han hoi ceitakhai pawi koe kaawm e tami pueng hanelah, saring dawk tu hoi hmaeca 30, 000 touh hoi maitotan 3, 000 touh a poe awh. Hotnaw teh siangpahrang hnopai dawk hoi e doeh.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
Hahoi, kahrawikungnaw ni ma lungtho lahoi tamipueng hane, vaihma hane, hoi Levihnaw hanelah a poe awh. Cathut im kaukkung Hilkiah Zekhariah, Jehiel tinaw ni ceitakhai pawi hanelah tu hoi hmaeca 2,600 touh hoi maitotan 300 touh vaihma koe a poe awh.
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
Konaniah hoi a nawngha Shemaiah, Nathanel hoi Levihnaw kaukkungnaw e kaukkung Hashabiah, Jeiel, Jozabad tinaw nihai, ceitakhai pawi hanlah Levihnaw hah tu hoi hmaeca 5, 000 touh hoi maitotan 500 touh a poe awh.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
Hottelah thaw tawknae teh a kârakueng awh teh, siangpahrang ni kâpoe e patetlah vaihmanaw teh amae hmuen koevah, a kangdue awh teh, Levihnaw haiyah ahuhu lahoi a kangdue awh.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
Hote ceitakhai pawi hanlah a thei awh teh, vaihmanaw ni a thi hah a kathek awh. Levihnaw ni a pho hah a ho awh.
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
Mosi cauk dawk kaawm e patetlah a imthungkhu lahoi lengkaleng thaw a rei e patetlah BAWIPA koe poe hanelah hmaisawi han satheinaw hoi maitonaw hah a kârei awh.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
Hote ceitakhai pawi ca hanelah, aphung patetlah kahmin lah a pâeng awh. Hateiteh, poe e moi kathounge hah hlaam, arai kaawm hoeh e hlaam hoi sum hlaam dawk a thawng awh teh, taminaw koe a ceikhai awh.
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
Hathnukkhu, amamouh hoi vaihmanaw hanlah bout a kârakueng awh. Bangkongtetpawiteh, Aron e capa vaihmanaw teh hmaisawi thuengnae khoungroe dawk moi thaw hah poe hoi tangmin totouh a tawk awh. Hatdawkvah, Levihnaw ni amamouh hoi Aron e capa vaihmanaw hanlah bout rakung hanlah a ngainae doeh.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
Hahoi, Devit, Asaph, Heman hoi siangpahrang profet Jeduthun naw ni kâ poe e patetlah la ka sak e Asaph capanaw teh amamae hmuen dawk a kangdue awh. Hote longkha karingkungnaw teh, longkha tangkuem koevah, ao awh. Bangkongtetpawiteh, a hmaunawngha Levihnaw ni a rakueng pouh dawkvah, a thaw hah ceitakhai awh han ngai hoeh.
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Hottelah, siangpahrang Josiah ni kâ poe e patetlah ceitakhai pawi sak han hoi, BAWIPA e khoungroe dawk hmaisawi thuengnae poe hanelah hote hnin dawk BAWIPA thaw tawknae hnonaw pueng hah a rakueng awh.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
Hote hmuen koe kaawm e Isarelnaw ni hote hnin dawk ceitakhai pawi hah a sak awh. Tonphuenhoehe vaiyei pawi haiyah hnin sari touh thung a hno awh.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
Profet Samuel se nahoi Isarel ram vah hot patetlah ceitakhai pawi sak awh boihoeh. Isarel siangpahrang apinihai Josiah, vaihmanaw, Levihnaw hoi Judah tami pueng hoi Isarelnaw ni a sak e patetlah sak awh boihoeh.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
Josiah a bawinae kum 18 nah ceitakhai pawiteh a sak awh.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
Hathnukkhu hoi Josiah ni bawkim be a pathoup hnukkhu, Izip siangpahrang Neko teh, Kakhemish tuk hanelah Euphrates palang a cei teh Josiah ni a tuk.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
Hatei, ahni ni nang Judah siangpahrang kai hoi nang bangmaw kâtuk hanelah kaawm. Sahnin vah nang na tuk hanelah, ka tho hoeh bo. Ka tuk lahun e tuk hanelah doeh ka tho. Cathut ni na huerang hanelah kâ na poe. Kai koe lah kampang e Cathut hah taran hanh. Na raphoe payon vaih telah laicei a patoun.
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Hatei, Josiah ni ban takhai hane ngai hoeh. A tuk thai nahan a meilam a kâthung teh, Cathut e a pahni dawk hoi ka tâcawt e Neko ni dei e hah tarawi ngai pouh hoeh. Megiddo tanghling vah, ahnimouh tuk hanelah a cei.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
Licung kapatuemnaw ni Josiah hah a kâ awh teh siangpahrang ni a sannaw koevah, kai hah na cetkhai awh leih. Bangkongtetpawiteh, hmâ puenghoi ka ca toe telah a ti.
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
A sannaw ni leng dawk hoi a la awh teh, alouke leng dawk a hruek awh. Jerusalem a ceikhai awh teh, a due hnukkhu a na mintoenaw e phuen dawk a pakawp awh. Judahnaw hoi Jerusalem kaawm e naw ni Josiah a khui awh.
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Jeremiah ni Josiah hah a khui. La ka sak e napui tongpa naw ni a na minca totouh Josiah khuinae a dei awh rah. Isarel ram dawk phung a tawn awh teh, khenhaw! khuinae la dawkvah a thut awh.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
Josiah a kâroenae dawk hoi kaawm rae pueng BAWIPA e kâlawk dawk ao e patetlah hnokahawi ka sak e,
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
ahmaloe hoi a hnukteng e hai khenhaw! Isarel siangpahrang hoi Judah siangpahrang lairui thutnae cauk dawk thut e lah ao.