< 2 Nyakati 35 >
1 Yosia akaadhimisha Pasaka kwa Bwana katika Yerusalemu, mwana-kondoo wa Pasaka akachinjwa siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
Hina bagade Yousaia da Hina Godema nodone, Yelusalemega Baligisu Lolo Nasu hamoi. Eso ba: , oubi agega, ilia da Lolo Nasu hamoma: ne, ohe medole lelegei.
2 Akawaweka makuhani kwenye wajibu wao na kuwatia moyo katika utumishi wa Hekalu la Bwana.
E da gobele salasu dunu, ilia Debolo Diasu ganodini hawa: hamosu amo ilima ilegei. Amola amo noga: le hawa: hamoma: ne, e da ilia dogo denesima: ne sia: i.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Waisraeli wote na waliokuwa wamejiweka wakfu kwa ajili ya kazi ya Bwana, “Liwekeni hilo Sanduku takatifu katika Hekalu lile alilojenga Solomoni mwana wa Daudi mfalme wa Israeli. Halipaswi kubebwa huku na huko mabegani mwenu. Sasa mtumikieni Bwana Mungu wenu na watu wake Israeli.
Amola e da Lifai fi dunu (ilia da Isala: ili fi ilima olelesu dunu, Hina Gode Ea momogili gagai galu) ilima amane hamoma: ne sia: i, “Dilia Gode Ea Hadigi Gousa: su Sema Gagili amo Debolo Diasu (hina bagade Soloumane, Da: ibidi egefe ea gagui) amo ganodini ligisima. Dilia amo soge eno, soge enoga gaguli ahoasu hou fisili, guiguda: dilia Hina Gode amola Ea fi Isala: ili dunu ilima hawa: hamoma.
4 Jiandaeni kwa kufuata jamaa zenu katika migawanyo yenu, kufuatana na maelezo yaliyoandikwa na Daudi mfalme wa Israeli na mwanawe Solomoni.
Dilia sosogo fi defele, amola dilia hawa: hamosu amo hina bagade Da: ibidi amola egefe hina bagade Soloumane ela dilima ilegei, amo defele, Debolo Diasu ganodini hawa: hamoma.
5 “Simameni mahali patakatifu kwa kufuata migawanyo ya jamaa za baba zenu kulingana na koo zenu na pawepo Walawi kwa ajili ya kila mgawanyo wa nyumba ya baba zenu.
Dilia Isala: ili sosogo fi afae afae noga: le fidima: ne momagema.
6 Chinjeni mwana-kondoo wa Pasaka, jitakaseni, nanyi kwa niaba ya koo zenu fanyeni maandalizi, mkitenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Mose.”
Dilia Baligisu Lolo Nasu sibi mano amola goudi huluane medole legema: ne momagema. Amaiba: le, Isala: ili fi dunu da hamoma: ne sia: i amo Hina Gode da Mousese ea lafidili, ninima i, amo noga: le fa: no bobogema: ne, dilia nigima: dodofema, amola gobele salimusa: ohe momagema.”
7 Ndipo Yosia akawapa watu wote wana-mbuzi waliokuwepo jumla ya kondoo wapatao 30,000 kwa ajili ya sadaka ya Pasaka, pia na ngʼombe 10,000, vyote hivi kutoka mali binafsi ya mfalme.
Yuda fi dunu da Baligisu gobele salasu hamoma: ne, hina bagade Yousaia da hina: ohe fofoi wa: i amoga sibi, sibi mano amola goudi mano gilisi 30,000 agoane, amola bulamagau gawali 3,000 agoane i.
8 Pia maafisa wake, wakatoa kwa hiari yao wakawapa watu, makuhani na Walawi. Hilkia, Zekaria na Yehieli, waliokuwa maafisa wakuu wa Hekalu la Mungu, wakawapa makuhani sadaka za Pasaka wana-kondoo na wana-mbuzi 2,600 na mafahali 300.
Yousaia eagene ouligisu dunu da gobele salasu ohe mogili, dunudafa, gobele salasu dunu amola Lifai fi dunu ilima i. Amola Debolo Diasu ouligisu dunu amo gobele salasu dunuma sibi mano 2,600 agoane, goudi mano mogili amola bulamagau gawali 300 agoane amo gobele salima: ne ilima i.
9 Konania na nduguze wawili, Shemaya na Nethaneli, pamoja na Hashabia, Yeieli na Yozabadi waliokuwa viongozi wa Walawi, nao pia wakawapa Walawi wana-kondoo na wana-mbuzi 5,000 na mafahali 500, kwa ajili ya sadaka za Pasaka.
Lifai fi ouligisu dunu amo Gononia, Siema: ia, Nida: niele (Siema: ia eya), Ha: siabaia, Yiaiele amola Yosaba: de - ilia da sibi mano amola goudi waha debe mogili 5000 agoane, amola bulamagau gawali 500 agoane - amo Lifai dunu ilia gobele salimusa: ilima i.
10 Huduma ilipomalizika kuandaliwa makuhani wakasimama mahali pao na Walawi katika migawanyo yao kama mfalme alivyokuwa ameamuru.
Baligisu Lolo Nasu liligi huluane da momagei dagoloba, hina bagade da amo hamoma: ne sia: beba: le, gobele salasu amola Lifai fi dunu da ilila: sogebiga dadalei.
11 Wana-kondoo wa Pasaka wakachinjwa, nao makuhani wakanyunyiza ile damu waliyokabidhiwa, wakati Walawi wakiwa wanawachuna wale wanyama ngozi.
Ilia da sibi mano amola goudi medole lelegelalu, Lifai fi dunu da ilia gadofo houga: i. Gobele salasu dunu da maga: me oloda da: iya fogagaga: la: i.
12 Wakatenga sadaka za kuteketezwa ili waweze kugawia ili migawanyo kwa kufuata jamaa za baba zao ili watoe sadaka kwa Bwana kama ilivyoandikwa katika Kitabu cha Mose. Wakafanya vivyo hivyo kwa wale mafahali.
Amalalu, ilia da Mousese ea Sema dedei defele, Hina Godema gobele salimusa: , ilia da sosogo fi afae afae ilima amo ohe gogo fane i.
13 Wakawaoka wale wanyama wa Pasaka kwenye moto kama ilivyoamriwa, wakachemsha zile sadaka takatifu kwenye vyungu, masufuria makubwa na vikaango na kuwagawia watu wote upesi.
Lifai fi dunu da God Ea hamoma: ne sia: i dedei defele, Baligisu gobele salasu ohe liligi amo laluma gobele gala: i. Amola ilia da hadigi iasu liligi amo gobele nasu ofodo, sosobeni amola gaga ganodini gobei. Amalalu, ilia hedolowane hu gobei amola dunu ilima sagoi.
14 Hatimaye wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani, kwa sababu wale makuhani, yaani, wazao wa Aroni, walikuwa wanatoa sadaka za kuteketezwa pamoja na zile sehemu zilizonona mpaka usiku. Hivyo Walawi wakafanya maandalizi kwa ajili yao wenyewe na kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Aroni.
Amalu, Lifai fi dunu da ili manusa: , amola Elane egaga fi gobele salasu dunu ili moma: ne, hu momagele legei. Bai gobele salasu dunu da hawa: hamonanawane gasi. Ilia da ohe mogili gogo gobele sali, amola eno ohe amoga sefe duga: i, amo gobele sali.
15 Waimbaji, wazao wa Asafu, walikuwa katika nafasi zao, kama ilivyoagizwa na Mfalme Daudi, Asafu, Hemani na Yeduthuni mwonaji wa Mfalme. Mabawabu katika kila lango hawakuhitaji kuacha nafasi zao kwa sababu Walawi wenzao walifanya maandalizi kwa ajili yao.
Da: ibidi ea musa: hamoma: ne sia: i defele, Lifai fi amola A: isa: fe sosogo gesami hea: lala dusu dunu, ilia da ilila: hawa: hamosua lefulubi ba: i. Ilia dio da A: isa: fe, Hima: ne amola Yediudane (hina bagade ea balofede dunu). Debolo Diasu logo ga: su sosodo aligisu dunu da ilia sosodo aligisu sogebi fisili hame ahoasu. Bai Lifai fi dunu oda da Baligisu Lolo ilia moma: ne momagei.
16 Kwa hiyo wakati ule huduma yote ya Bwana ilifanyika katika kuadhimisha Pasaka, kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana kama alivyoamuru Mfalme Yosia.
Amaiba: le, hina bagade Yousaia ea hamoma: ne sia: i defele, ilia da Baligisu Lolo Nasu amola oloda da: iya gobele salasu hou, amo huluane ilia da Hina Godema nodomusa: hamoi.
17 Waisraeli waliokuwepo wakaadhimisha Pasaka wakati huo na Sikukuu ya Mikate Isiyotiwa Chachu kwa siku saba.
Eso fesuale amoga, Isala: ili fi dunu huluane Yelusalemega esalu, ilia da Baligisu Lolo Nasu amola Agi Yisidi Hame Sali Lolo Nasu hahawane hamoi.
18 Kulikuwa hakujafanyika Pasaka kama hii katika Israeli tangu siku za nabii Samweli wala hakukuwa na mfalme yeyote wa Israeli ambaye kamwe alishaadhimisha Pasaka kama ile aliyofanya Mfalme Yosia, akiwa na makuhani, Walawi na watu wote wa Yuda na watu wa Israeli waliokuwepo huko, pamoja na watu wa Yerusalemu.
19 Pasaka iliadhimishwa katika mwaka wa kumi na nane wa utawala wa Mfalme Yosia.
Balofede dunu Sa: miuele ea fifi misi eso amogalu, ilia agoane hamedafa hamosu. Isala: ili hina bagade musa: fifi masu, ilia da Baligisu Lolo Nasu amo hina bagade Yousaia, gobele salasu dunu, Lifai fi dunu amola Isala: ili amola Yuda amola Yelusaleme fi dunu ilia da Yousaia ea ouligisu ode 16 amoga hamoi, agoai afae hamedafa hamoi.
20 Baada ya haya yote, Yosia alipomaliza kulitengeneza vizuri Hekalu, Neko mfalme wa Misri, akapanda ili kupigana huko Karkemishi katika Mto Frati, naye Yosia akatoka kwenda kupigana naye.
Hina bagade Yousaia da Debolo Diasu hou noga: le hahamoi. Amogalu, Idibidi hina bagade Nigou da ea dadi gagui wa: i oule, Gagimisi moilai bai bagade (Iufala: idisi Hano bega: dialu) amo doagala: musa: wa: i misi. Yousaia da e gagabomusa: dawa: i.
21 Lakini Neko akamtumia wajumbe kusema, “Kuna ugomvi gani kati yangu mimi na wewe, Ee Mfalme wa Yuda? Si wewe ninayekushambulia wakati huu, bali ile nyumba ambayo nina vita nayo, Mungu ameniambia niharakishe, kwa hivyo acha kumpinga Mungu, ambaye yuko pamoja nami, la sivyo atakuangamiza.”
Be Nigou da Yousaiama amo sia: adoma: ne sia: si, “Yuda hina bagade! Amo gegesu na waha gegenanebe da dia liligi hame. Na da dima hame gegena misi. Be na da na ha lai dunuma gegena misi. Amola Gode da hedoloma: ne nama adoi. Gode da nama gaiba: le, E da di gugunufinisisa: besa: le, na logo mae hedofama!”
22 Lakini hata hivyo, Yosia hakukubali kumwacha, bali alijibadilisha ili kupigana naye vita. Hakusikiliza yale Neko aliyokuwa amemwambia kwa agizo la Mungu bali alikwenda kupigana naye katika tambarare ya Megido.
Be Yousaia da dafawane gegemusa: dawa: i. E da Gode Ea sia: , Nigou ea lafidili sia: be, amo nabimu higa: i galu. Amaiba: le, e da ea da: i afadenene, Migidou umi amoga gegemusa: asi.
23 Wapiga upinde wakampiga Mfalme Yosia, naye akawaambia maafisa wake, “Niondoeni, nimejeruhiwa vibaya sana.”
Gegenana, Idibidi dunu da gala: gonoba, hina bagade Yousaia da ludi dagoi. E da ea hawa: hamosu dunuma amane sia: i, “Na da se bagade nababeba: le, na enodi gaguli masa!”
24 Kwa hiyo wakamshusha kutoka kwenye gari lake la farasi, wakamweka kwenye gari lingine alilokuwa nalo na kumleta Yerusalemu, ambako alifia. Akazikwa katika makaburi ya baba zake, nayo Yuda yote na Yerusalemu wakamwombolezea Yosia.
Ilia da e sa: liode da: iya dialu, laleguduli, eno sa: liode da: iya ligisili, Yelusalemega gaguli asi. Amogawi, e da bogobeba: le, ilia da ea da: i hodo amo hina bagade ilia bogoi gele gelaba ligisila asi. Yuda fi dunu amola Yelusaleme fi dunu huluane da e bogoiba: le didigia: i.
25 Nabii Yeremia akatunga maombolezo kwa ajili ya kifo chake, nao waimbaji wote, wanaume kwa wanawake, hufanya ukumbusho wa Yosia katika maombolezo hadi leo. Haya yakafanywa desturi katika Israeli, nayo yameandikwa katika Maombolezo.
Balofede dunu Yelemaia da Yousaia dawa: musa: , fofagini gesami hahamoi. Wali, Isala: ili gesami hea: su dunu amola uda da Yousaia ea hou dawa: beba: le, didigia: sea, ilia da amo gesami hea: sa. Amo gesami hea: su da fofagini gesami hea: su dedei buga ganodini dedene legei dagoi.
26 Matukio mengine ya utawala wa Yosia na matendo yake mema, kulingana na yale yaliyoandikwa katika sheria ya Bwana:
Yousaia ea hamonanu huluane - ea Hina Godema asigi hou, ea Sema amoma nabasu hou,
27 matukio yote, kuanzia mwanzo hadi mwisho, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.
amola ea hawa: hamonanu hemosu asili dagosu - amo huluane da “Isala: ili amola Yuda hina bagade ilia Hamonanu Meloa”, amo ganodini dedene legei.